Neymar hana tofauti na Pogba, utoto mwingi sana!!

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Naangalia mtanange wa Uefa hapa kati ya Real Madrid Vs Psg naona Neymar licha ya kuwa na kipaji kikubwa bado ndani ya uwanja ameshindwa kuonesha thamani yake zaidi ya kufanya utoto mwingi kama vile kujiangusha na kupiga chenga zisizo na faida kwenye timu yake. Hana na tofauti na mpaka rangi kwenye Nywele kutoka Manchester!
Kama PSG wanamtegemea Neymar awape mafanikio watasubiri sana!

Povu ruksa...
 
Sahihi kabisa, mpira wa "chenga tawala", atuachie sisi wadanganyika.....kanzu, tobo ahahahahahah!

Vyovyote atakavyoamua kuucheza mpira, kama hutikisi nyavu za wapinzani wako, hakuna atakaye kukumbuka kwa chenga na kujiangusha Ovyo. Wanasema, USA ndio kila kitu kwenye mambo mengi;
Understanding
Speed
Accuracy
 
Neymar aina ya mpira anaoucheza unaigharimu timu nzima, chenga zisizo na mashiko, kujiangusha kwingi, hana maamuzi kwa wakati sahihi.
La mwisho kubwa zaidi anataka kila goli au ushindi wa timu upitie kwake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…