ZionGate
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 6,362
- 2,991
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Mulamu N'gambi amesema kanuni ya kutaka asilimia 49 za hisa kumilikiwa na watu kuanzia watatu, imekuja wakati Simba ikiwa tayari imepata muwekezaji
Akizungumza mapema leo, Mulamu amesema kwa kuwa utaratibu huo umekuja kwa kuchelewa, haitakuwa rahisi kwao kurudi nyuma
"Hii kanuni aliyosema Waziri imekuja wakati Simba tukiwa tayari tumevuka hatua hiyo, tulikuwa tumeshapata muwekezaji,"amesema
"Kwa hiyo leo tena hatuwezi kurudi kwa muwekezaji kumwambia atoke ili waje watatu, nafikiri ni jambo ambalo ni gumu kutekelezeka"
"Tulichokuwa tunafahamu awali, muwekezaji hakutakiwa kuwa na zaidi ya asilimia 49 ya hisa wakati asilimia 51 zinabaki kwa wanachama"
Jana Waziri wa habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Harrison Mwakyembe alisema sheria hiyo inataka wawekezaji waanzie watatu na kuendelea
Aidha Dk Mwakyembe alisema Sheria hiyo haikusimamiwa ipasavyo na TFF hivyo Serikali imeanza mchakato wa kutunga kanuni na marekebisho ambayo yatasimamiwa na BMT
Akizungumza mapema leo, Mulamu amesema kwa kuwa utaratibu huo umekuja kwa kuchelewa, haitakuwa rahisi kwao kurudi nyuma
"Hii kanuni aliyosema Waziri imekuja wakati Simba tukiwa tayari tumevuka hatua hiyo, tulikuwa tumeshapata muwekezaji,"amesema
"Kwa hiyo leo tena hatuwezi kurudi kwa muwekezaji kumwambia atoke ili waje watatu, nafikiri ni jambo ambalo ni gumu kutekelezeka"
"Tulichokuwa tunafahamu awali, muwekezaji hakutakiwa kuwa na zaidi ya asilimia 49 ya hisa wakati asilimia 51 zinabaki kwa wanachama"
Jana Waziri wa habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Harrison Mwakyembe alisema sheria hiyo inataka wawekezaji waanzie watatu na kuendelea
Aidha Dk Mwakyembe alisema Sheria hiyo haikusimamiwa ipasavyo na TFF hivyo Serikali imeanza mchakato wa kutunga kanuni na marekebisho ambayo yatasimamiwa na BMT