Pre GE2025 Ngara: Walimu Wakuu wa Shule za Wilaya ya Ngara, Wachangishana Fedha kwaajili ya Fomu ya Urais ya Rais Samia 2025 na kwaajili ya Mbunge Ndaisaba

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hao wamelazimishwa kutoa kwenye mafungu wanayogawiwa kila mwezi. Siasa chafu za mbunge wa ngara
 
Mimi kwa mawazo yangu naona walimu kama hawana upeo wa kufikiria,kwan walopandishwa madaraja ni wao tu
 
Naona wengi mmeanika upumbavu wenu kuwashambulia walimu wote pasipo kujua mchezo ulioko hapo. Hakuna mwalimu wa kawaida wa kufanya ujinga huo. Walimu waliofanya ujinga huo ni walimu wakuu ambao wao ni miongoni mwa watu wanaoiba pesa za serikali.

Wanafurahi sana kwa jinsi utawala wa sasa hivi ulivyo maana pesa yote ya Elimu bila Malipo inayotoka serikali kuu inaliwa na hao hao ikiwemo wakuu wa shule, maafisa elimu kata na maafisa Elimu na baadhi ya walimu wachache walioko karibu na wakuu wa shule. Zaidi ni kwamba hakuna tena ufuatiliaji asilimia kubwa wa pesa inayotoka serikalini kuja shule inaliwa na hao wanajifanya kuwa wanampenda Samia.

Hakuna mkuu wa shule mjinga wa kuacha kuchangia elfu kumi wakati kwa mwezi nje ya mshahara anao uhakika wa kupiga hata milioni. Hata ungekuwa ni wewe usingeshindwa kutoa elfu kumi wakati unapata takribani milioni moja nje ya mshahara. Kumbuka hakuna mwalimu wa kawaida anaye ikubali CWT hapa Tanzania. Ukihukumu walimu wote unakuwa unakosea.
 
Hapo viongozi CWT lazima walishupalie hili maana wanakwenda kupiga pesa ndefuu.
Maskini hii kada sijui ni vile wengi wapo vijijini ndanindani ndo maana hata hawawezi goma.
Mpaka uchaguzi unaisha watu watakuwa wamepiga sana pesa......2025 ni uchaguzi utakaokuwa na pesa sana wazee wa kuchomeka mirija kazi kwenu
 
Umaskini wa akili mbaya sana.
Ndio maana tunasema kada ya walimu imejaa utahira.
Mkuu wa shule analipwa posho around 250k per month tena inaingia kwa kusuasua. Unamchangia mtu pesa ya form ambaye analipwa mamilioni na akistaafu within 5 yrs of his /her duty analipwa billion kwa Rais na mbunge around milioni 300.
Walimu wakuu nyie ni viongozi na mnastahili stahikinza viongozi, piganieni haki zenu, wenzenu mameneja TARURA, TPA, TRA, TEMESA, SIDO n.k wanalipwa mamilioni na gari nzuri ya kuwapeleka kazini na kuwarudisha home. Nyie mnaendeshwa na wajinga mnachangia tajiri pesa ya form. Mshahara wa MWALIMU wa daraja E ni mdogo kuliko mshahara wa mlinzi wa Bandari anayeanza kazi leo. Huyo mlinzi ana posho nyingi.
Dereva wa TRA anamzidi mshahara mwalimu.
Fundi Tanesco anamzidi mshahara MWALIMU mwenye degree.
Walimu ni wapumbavu
 
Na hao waalimu ndio waathirika wakubwa wa kikokotoo cha pension zao; nadhani wana kichaa au wamelogwa na mama S.
 
Hiki ni chama cha siasa kama vilivyo vyama vingine
 
Umefunga uzi
 
Hawa ndio tunategemea wawaondoe au wawapunguzie ujinga watoto.

Tuna safari ndefu sana hii nchi.
 
Nasikitika kwa mwandishi kuacha taarifa yake bila maswali haya:
1. Mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbj uliojengwa nyjmbani kwa mbunge ulikuwa na washiriki/ walimu wakuu wangapi?

2. Ulifanyika lini? Na Jumla ya Pesa iliyokusanywà ilikuwa kiasi gani, huku mbunge akipewa kiasi gani na gedha za gharama za fomu za urais zilipatikana kiasi gani na ziko wapi?
 
Wakuu waliitwa kugaiwa mitungi ya ges wawe wanapika Chai shuleni [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Aiseeee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…