Ngeleja awararua wapinzani Katiba Inayopendekezwa

Ngeleja awararua wapinzani Katiba Inayopendekezwa

Aloyce mk

Member
Joined
Nov 10, 2014
Posts
76
Reaction score
33
Ngeleja awararua wapinzani Katiba Inayopendekezwa

Friday, February 27 2015,

MBUNGE wa jimbo la Sengerema, Wiliam Ngeleja, amesema vyama vya upinzani havina hoja za msingi kugomea kura ya maoni Katiba inayopendekezwa, hivyo Watanzania wanapaswa kuwapuuza kwa kuwa wamelenga kusababisha machafuko nchini.

Alisema Katiba inayopendekezwa imezingatia maslahi ya Watanzania wote na kuwataka viongozi wa vyama vya upinzani kuacha kuwatisha wananchi badala yake wawaache watumie haki yao ya msingi ya upigaji kura kwa mujibu wa Katiba.

Aliyasema hayo juzi wakati wa ziara yake jimboni humo yenye lengo la kuwashukuru wananchi kwa kukipatia ushindi Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa, vijiji na vitongoji uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.

"Katiba inayopendekezwa imezingatia maslahi ya Watanzania walio wengi, hao wanaoipinga hawana hoja bali lengo lao kubwa ni kutaka kuleta machafuko hapa nchini, hakuna Katiba nzuri kama hii inayozingatia umuhimu wa kilimo ambacho ni uti wa mgongo wa Mtanzania," alisema.

"Wananchi kama mlivyotuamini kwa kutupatia ushindi wa asilimia 83 juu ya ile ya kitaifa, ipigieni kura ya ndio Katiba hii pindi muda utakapofika ili ipite kwa kishindo, wapinzani wameishiwa hoja ndio maana wakaweka mpira kwapani na kukimbia Bungeni wakati tukijadili, upotoshaji wao tuliubaini mapema wao waliamini watapata ushindi kumbe sivyo,"alisema Ngeleja.

Alisema, Katiba hiyo imejenga msingi mzuri wa uwajibikaji, kilimo, mazao ya chakula na biashara, wavuvi, watoto, kuzuia mianya ya rushwa kwa mafisadi na makundi mengine ndani ya jamii na kwamba Katiba hiyo si ya chama au kikundi kidogo cha watu, bali ni ya Watanzania.

"Wakati wa uchaguzi Serikali za mitaa, wapinzani walitumia sana hii hoja ya Katiba mpya na sakata la Escrow kuwalaghai wananchi ili wajipatie kura, bado tumewashinda, lakini mimi niwaombeni tuipigie kura ya ndio Katiba hii inayopendekezwa kwa kuwa ni msingi mkubwa wa maendeleo ya nchi," alisema.

Katibu wa Umoja wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM), wilayani Sengerema, Hassan Moshi, alisema kuwa viongozi vyama vya upinzani wanaikataa Katiba inayopendekezwa kwa kuwa lengo lao kubwa ni kugawana madaraka na kuvunja umoja na mshikamano uliopo miongoni mwa Watanzania.

Kwa upande wake, diwani wa kata ya Nyamatongo, Bw.Dickson Magili alisema kuwa hakuna Katiba kamilifu hapa duniani na kuwa nyingi zimekuwa zikirekebishwa mara kwa mara kulinga na mahitaji na kuwa Katiba inayopendekezwa imekidhi vigezo hivyo.

Alisema, Watanzania wanapaswa kuwaepuka wanasiasa wanaochochea kutokea kwa machafuko hapa nchini na kuwa umwagaji damu ya Watanzania kamwe usipewe kipaumbele.
 
sidhani kama anaelewa hata anachozungumza. muambieni aridhishe kwanza pesa zetu alizokwapua escrow na kisha amalizane na tume ya maadili ndo aje huku.
 
mwenye matokeo ya serikali za mitaa jimboni mwa huyu msaka tonge atuwekee humu tafadhali.
alichoniacha hoi ni kuwa na yeye anapinga ufisadi. hivi siku hizi maana ya neno fisadi imebadilika?
 
hivi kweli hii katiba pendekezwa ina bana mafisadi?kwa ufisadi ulioko ccm hawawezi kutunga ktk ya kuwabana,
 
CCM wamejitoa ufahamu kuhusu katiba pendekezwa wanafikiri watakaa milele madarakani,time will come and time will speak!!! Tumieni vema ujinga wa walio wengi ila siku wakijitambua mtatafuta pa kuficha sura zenu
 
CCM wamejitoa ufahamu kuhusu katiba pendekezwa wanafikiri watakaa milele madarakani,time will come and time will speak!!! Tumieni vema ujinga wa walio wengi ila siku wakijitambua mtatafuta pa kuficha sura zenu

Wee unayejiita “Babati Yetu”, vyama vinatoka wapi hapa, hapa tunazungumzia mustakabali wa nchi na sio chama. Toka hapo ulipo katika mawazo gandamizwa ingia kwenye utaifa bwana. Tanzania ni nchi huru uwe huru usipende kuegemea mawazo unayosikia. Uwe chachu ya mabadiliko kupitia Katiba Inayopendekezwa tupate Katiba Bora ya nchi yetu.
 
​Huyu mpokea rushwa, fisadi ex Waziri mzigo aache kubwabwaja na kutoa povu zito.
 
Wee unayejiita “Babati Yetu”, vyama vinatoka wapi hapa, hapa tunazungumzia mustakabali wan chi na sio chama. Toka hapo ulipo katika mawazo gandamizwa ingia kwenye utaifa bwana. Tanzania ni nchi huru uwe huru usipende kuegemea mawazo unayosikia. Uwe chachu ya mabadiliko kupitia Katiba Inayopendekezwa tupate Katiba Bora ya nchi yetu.

Hivyo vihela mnavyolipwa na Mafisadi ndiyo vinahamisha akili zenu mpaka kufikiri mnatumia makalio??? ..Eti nawewe unajiita mtu huru mwenye kuleta mabadiliko.. Mabadiliko gani wakati JAMBAZI KUU/FISADI Joka lenye Makengeza keshawakengeusha mmegeuka kuwa wapigadebe wa MAFISADI. Yaan maoni yetu kupitia Tume ya Warioba yatupwe leo unawaambia watu wawe chachu ya mabadiliko kupata Katiba bora,... Ipii.. Hii ya MAFISADI..??? Shame on you..

I remember during apartheid regime in South Africa walikuwepo watu kama ninyi ambao ni weusi lakini wakawa wanatumika na Serikali ya Makaburu kuwasaliti na kuwahadaa wa-africa wenzao juu ya Serikali ile dhalimu..!! Kilichokuwa kinawapata sio Mungu ni Shetani ndiyo alikuwa anakijua.

Traitor ni mbaya zaisi kuliko hata Oppressor mwenyewe!!..
Wewe ndiyo mbayazaidi kuliko hata Fisadi/Joka lenye makengeza..Na mtu kama wewe ndiyo ungekuwepo Afrika Kusini kipindi kile.. ungeshafukiwa siku nyingi na wazalendo wa nchi ile..
 
​Huyu mpokea rushwa, fisadi ex Waziri mzigo aache kubwabwaja na kutoa povu zito.

Porojo za nini hapa? Kazi iliyombele yetu ni moja tu na ya msingi sana kwa taifa. Tambua Katiba Inayopendekezwa si ya chama au kikundi kidogo cha watu, bali ni ya Watanzania. Acha kuwachanganya wananchi na mambo yasiyo ya msingi. Tanzania ni nchi ya amani kama inavyoainishwa kwenye Katiba Inayopendekezwa imezingatia misingi ya utu na udugu, uhuru, kujitegemea, haki, usawa, amani na utulivu, umoja na mshikamano katika nyanja zote za maisha yetu. "BAK" ungana na Watanzania wenzako kujenga nchi yetu.
 
Sidhani hata kama hanaelewa Maana ya katiba Mpya hili jizi
 
Hivyo vihela mnavyolipwa na Mafisadi ndiyo vinahamisha akili zenu mpaka kufikiri mnatumia makalio??? ..Eti nawewe unajiita mtu huru mwenye kuleta mabadiliko.. Mabadiliko gani wakati JAMBAZI KUU/FISADI Joka lenye Makengeza keshawakengeusha mmegeuka kuwa wapigadebe wa MAFISADI. Yaan maoni yetu kupitia Tume ya Warioba yatupwe leo unawaambia watu wawe chachu ya mabadiliko kupata Katiba bora,... Ipii.. Hii ya MAFISADI..??? Shame on you..

I remember during apartheid regime in South Africa walikuwepo watu kama ninyi ambao ni weusi lakini wakawa wanatumika na Serikali ya Makaburu kuwasaliti na kuwahadaa wa-africa wenzao juu ya Serikali ile dhalimu..!! Kilichokuwa kinawapata sio Mungu ni Shetani ndiyo alikuwa anakijua.

Traitor ni mbaya zaisi kuliko hata Oppressor mwenyewe!!..
Wewe ndiyo mbayazaidi kuliko hata Fisadi/Joka lenye makengeza..Na mtu kama wewe ndiyo ungekuwepo Afrika Kusini kipindi kile.. ungeshafukiwa siku nyingi na wazalendo wa nchi ile..

Nawe si wale wale tu wasio na busara, unapenda kwa jirani unasahau kujenga kwako? aibu iwe juu yako. Ili upate mabadiliko ni lazima uwe na msingi na msingi huo ndio Katiba! Umesinzia wapi sasa. Isome na uipigie kura muda utakapofika ili ulete mabadiliko ndani ya nchi yako. Usibaki kulalamika kama mtu asiye na mwelekeo.
 
Naona kuna jitihada kubwa ya kusema kuwa katiba pendekezwa si ya chama bali ni ya taifa. Wote tuliona jinsi Rasimu Ya Katiba ya Jaji Warioba ilivyopigwa vita na ccm na kutekwa na chama hicho, na baadae kulazimisha kutunga hiyo katiba bungeni ili kuipa sura ya utaifa. Hatujasau, si siku nyingi ambazo zimepita. Rasimu ya Katiba ya Warioba ndiyo iliyosheheni maoni ya wananchi, na kwa mantiki hiyo wananchi kwa wingi wao wataikataa katiba pendekezwa ya mafisadi.
 
Mie na porojo mbali mbali. Kamwe siwezi kuwaunga mkono wahuni ambao wamechakachua maoni mazuri ya Watanzania kama yalivyokusanywa na Tume ya Warioba ambayo ilipewa kazi ya kukusanya maoni hayo. Kisha wakafanya hila, wizi, vitisho na hata kuhesabu kura za wafu na wale ambao walikuwa hawapo kwenye Bunge lile. Katiba hii ya wahuni ambao wameipitisha ili wang'ang'anie madaraka na kuendeleza ufisadi wao mkubwa dhidi ya Watanzania inastahili kususiwa na Watanzania wote wanaojitambua na kuitakia mema nchi yetu.

Porojo za nini hapa? Kazi iliyombele yetu ni moja tu na ya msingi sana kwa taifa. Tambua Katiba Inayopendekezwa si ya chama au kikundi kidogo cha watu, bali ni ya Watanzania. Acha kuwachanganya wananchi na mambo yasiyo ya msingi. Tanzania ni nchi ya amani kama inavyoainishwa kwenye Katiba Inayopendekezwa imezingatia misingi ya utu na udugu, uhuru, kujitegemea, haki, usawa, amani na utulivu, umoja na mshikamano katika nyanja zote za maisha yetu. “BAK” ungana na Watanzania wenzako kujenga nchi yetu.
 
Mie na porojo mbali mbali. Kamwe siwezi kuwaunga mkono wahuni ambao wamechakachua maoni mazuri ya Watanzania kama yalivyokusanywa na Tume ya Warioba ambayo ilipewa kazi ya kukusanya maoni hayo. Kisha wakafanya hila, wizi, vitisho na hata kuhesabu kura za wafu na wale ambao walikuwa hawapo kwenye Bunge lile. Katiba hii ya wahuni ambao wameipitisha ili wang'ang'anie madaraka na kuendeleza ufisadi wao mkubwa dhidi ya Watanzania inastahili kususiwa na Watanzania wote wanaojitambua na kuitakia mema nchi yetu.
Heshima yako mkuu wala usipoteze muda wako kushindana na huyu mwehu wa ccm wanaipigia debe katiba iliyoandikwa na maharamia wenzake wa ccm.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom