Ngeleja badala ya kushughulikia matatizo ya umeme, aenda Tarime kwenye kampeni

Ngeleja badala ya kushughulikia matatizo ya umeme, aenda Tarime kwenye kampeni

Basi kwa taarifa yako tu.,CCM itaibuka na ushindi wa kishindo kati9ka jimbo la TARIME na usitegeemee CHADEMA hii ya Mbowe na Ukabila wao watapewa dhamana hapo TARIME.The same happening in Kiteto will happen in TARIME.

Screw CHADEMA and FMES na Ngelejha Ana jihamini kwa kuwa yeye ni Bora

I will hold you to your prediction.
 
Hii CCM inawalisha nini watu..........!! yani ukiingia tu huko, hata kama umesoma kiasi gani!ubongo una lala na kuanza kutetea ujinga unaoonekana dhahiri! angalia kina makamba, nchimbi, membe, na huyu GEMBE wote sijui wamepofushwa na nini?

kuona ukweli inakuwa taabu kwelikweli!! Chama na mtu havitenganishwi! mbona ni sawa na serikali na viongozi... wakiboronga viongozi ndio serikali imeboronga... wakiboronga kina lowasa na chenge na mkono, na mgonja ndo imeboronga CCM na serikali yake........unahitaji elimu gani kujua hii.... au ni ubishi na ukaidi usiokuwa na tija kwa taifa......Ole wenu wanafiki....siku zenu ni chache..... take my word....kizazi kipya kita wafunza adabu subirini kidogo tu mtadhihirisha hilo!!!!!!!!!
 
Lunyungu,

Nachookijua CCM Itashinda!

tell us more why this time and not in 2005.....??au umeoteshwa na mizimu!!!!tusaidie tujue! au ndo hizo mbinu za kununua shahada? pesa za EPA zilishidwa ndo itakuwa za ruzuku???tusaidie tafadhali mkuu gembe........
 
Hao ndio viongozi wetu, na hiyo ndiyo nchi yetu. Kila mtu anafanya jambo kufurahisha wanaompa ulaji.Tatizo la viongozi wetu wanapokuwa madarakani wanajijengea kacyst kiasi kwamba kisiingie kitu kutoka nje, na wao wenyewe wasitoke, wapo kujineemesha, na hawaoni umaskini uliotanda miongoni mwa watanzania. Huyu Ngeleja kama si limbukeni ni nani basi? Tarime kunahusiana nini na maisha ya watanzania? Badala ya kushughulikia mambo ya maana anaenda kudanganya watu, mbona kwenye jimbo lake bado kuna matatizo kibao,achana na matatizo ya umeme yaliyopo Tanzania nzima,akitoka huko ameshatia ndani per diem, alikuwa kazini, aibu hamna jamani? Kama watu hawawezi kazi, kwa nini wanataka madaraka? madaraka si kwa ajili ya kukenua meno ili watu wayaone, ni kazi. Tujilaumu sisi wenyewe watanzania, hatujawahi kuwa serious kutafuta viongozi watakaotupeleka mbele, tunataka viongozi watakaotugawa tisheti na kofia. Nilishangaa kuona mtaa mmoja ktk miji yetu ya Tanzania wazee kwa vijana wanakunywa kahawa waliyohongwa na CCM ili wakahudhurie maandamano ya kupongeza hotuba ya Raisi aliyoitoa bungeni. Watu wakafurahia na kuona CCM ni ya maana sana kwa kuwapa kikombe cha kahawa cha shilingi kumi,na kuuza utu wao, inanisikitisha sana. Tujenge system yenye nidhamu, viongozi waadilifu wenye lengo la kutumikia watu, watu wanaofanya kazi kwa bidii, kila mmoja akijua kazi yake. Tatizo watanzania tunapenda vitu vya bure, hivyo havipo duniani!! Ninasikitika wanadanganywa tena Tarime huko. Kingunge bado hana aibu kaumbuka mara ngapi kwa kauli zake zisizokuwa na maana, tofauti na umri wake?? Tchao!!
 
1
. Mkuu Fmes,

Suala la Wabunge kuhongwa na kunyamaza(hapa tunaongelea hata wabungwe wa CHADEMA) sio tatizo la waziri ni tatizo la wabunge which the samae thing applies to wanachi kipindi cha uchaguzi,wanahongwa ili wamchague flani..Nyani Ngabu I second you once again,waafrika ndivyo tulivyo.

Sasa unasema kwamba Ngeleja anajiamini sana, halafu unarudi tena na kusema kuwa it is ok kwa wabunge kuhongwa ili bajeti ya the very same confident minister Ngeleja ipite?

Mkuu Gembe kwa kawaida huwa ninakuaminia sana, lakini not on this one, hapa uko off the line kwa sababu, rushwa ni adui wa haki sasa haiwezi kutumiwa na waziri anayejiamini, sina tatizo na Ngeleja kama waziri lakini I have a problem waziri kijana kama yeye, anapoona umeme ni wa mgawo, halafu yeye anaenda kuomba kwenda Tarime kwenye kampeni za ubunge, CCM ina wabunge 90% ya wabunge wote sasa hivi, nini cha maana kilichofanyika mpaka yeye kuwa this excited na kukimbilia Tarime huku wananchi wanalala gizani?


2
. Ndio nilikuwa SA na nimerudi kwa muda kusalimia ndugu jamaa na marafiki na hili suala halikuhusu.Mimi kujau ahabarai za Tanzani ni jukumu langu na nafuatilia kila siku.

Baada ya kurudi si umeona umeme ulivyowa shida bro, sasa kweli unawezaej kumsifu waziri anayeacha wananchi wakiwa kwenye giza anakwenda kuwadanganya wananchi wengine wakichague chama kile kile kinachowaweka kwenye giza kuanzia la umeme mpaka wa akili?

3.
Suala la Utu uzima na ukali vimetoka wapi.Yes i love CCM beacuase haina ukabila no matter wat..Masuala yanaohusu Ufisadi ni ya watu Binafsi na ni kama walivyo viongozi wa chadema na Pesa Ya ruzuku ya CHAMA.

Mie naeleza ukweli tu
Ahsante Mkuu.

Mimi sio Chadema wala siifagilii Chadema, lakini haina maana ya kukimbilia CCM kichwa kichwa kama kondoo, Mayor Bloomberg yametokea matatizo ya uchumi amevunja safari zote na kubaki aki-monitor situation, Bush amevunja likizo Texas na kubaki Ikulu kwa sababu ya dharura ya uchumi,

Dar hatuna umeme ndio kwanza waziri anakimbilia Tarime kupiga domo wewe unamsifu kuwa anajiamini sana, Gembe this should not be coming from you sawa ipende sana CCM lakini kuwa na objectivity angalau kidogo, maana hata wananchi huko vijijini wanaoipenda sana CCM waliwazomea mawaziri wa CCM walipoenda kuwadanganya kuhusu bajeti, sasa iweje mkuu wewe na exposure yote hiyo uingie kichwa kichwa hivi mkuu?

Yaani na nyinyi vijana mkianza kuongea lugha za kina Makamba kweli kutakua na hope na taifa hili? Mimi sio Chadema, lakini siwezi kuitukana Chadema, kwa sababu ninajua for a fact kuwa bila Chadema saa hizi wananchi tungepigwa vioboko barabarani na kina Chenge! na Lowassa!

Bila Chadema saa hizi Lowassa bado angekua waziri mkuu tena, akijitayarisha kugombea urais, Ngeleja wako angeendelea kuwa waziri mdogo maana Msabaha angekua bado ni waziri, I mean kuipenda CCM ni haki yako, ila kama mawazo yako ni haya basi haina sababu ya kuja hapa JF, hapa tunakuja kuikosoa serikali na CCM chama changu, sio kuisifia tu hata kama wanatulaza na giza huku waziri wa umeme akienda Tarime kupiga domo la kura za ubunge, ambao CCM wanao wka 90% lakini mabadiliko wala maendeleo hakuna, huko nyuma tulisema tunataka viongozi vijana, ndio hawa kina Ngeleja, haoni tatizo wananchi kuishi kwa mgawo wa umeme na yeye kukimbilia Tarime, bila kuitwa na sad enough ni kwamba kuna member wa kumpa support hapa JF kwa kweli inasikitisha sana,

Gembe sikujua kua una mawazo kama ya Makamba kuwa eti wapinzani ni wasaliti, sasa hili taifa litakombolewa na nani? Gembe hata wewe mkuu?Hebu onneeni huruma kidogo wananchi walalahoi jamani!
 
Lunyungu,

Nachookijua CCM Itashinda!

Je utakubaliana na ushindi wa CCM, pamoja na kufahamu mambo mbali mbali ya kifisadi yanayofanywa na CCM? au wewe unachotaku kuona ni CCM inashinda bila kujali sifa za watendaji wakuu ndani ya chama hicho katika miaka ya karibuni?
 
Uchaguzi huu ni muhimu sana kwani hapo atakayeshinda ni wazi atakuwa na momentum nzuri kwasababu Taifa liko alarted kutokana na umaarufu wa siasa za jimbo hilo na utajiri wao.
Wananchi wa Tarime hawawezi kuichaguwa ccm hilo ni wazi....Sasa ccm kama wangekuwa waungwana...Basi wangewekeza kwa wananchi na si kuwatisha kwa kutumia dola na kuwanyanyasa...Hapo wameharibu sana kwasababu wanajuwa hawawezi kushinda..Ila pesa watakayotembeza hapo...Mhn mhn...Hivi JK kesharudi Bongo?
 
Mkuu FMES,

Kusadia Chama ni kujikomba?ina maana mawaziri wasisaidie Chama.najua huu ni mwiba wa moto kwa CHADEMA hasa baada ya kuona mbinu mpya ya CCM katika Uchaguzi huo.

Mie nina shaka na uanachama wako wa CCM,

1. Mawaziri kusaidia chama ni sawa, lakini sio wakati wa dharura ya umeme kama sasa, yaani wananchi wanalala kwenye giza viwanda vimesimama wewe waziri wa umeme unaenda Tarime, Gembe unasema hio ni kusaidia Chama au kukibomoa chama?

2. Unasema una wasi wasi na uanachama wangu wa CCM, hivi ulishwahi kuwa na wasi wasi na unachama wa CCM wa kundi zima la Mtandao, Ngeleja inculded, ambao walishapanga kuwa wakishindwa uchaguzi wa rais wangejitoa na kuingia Chadema? Hivi kunaweza kua dhambi kubwa dhidi ya chama kama hii? Yaani kuwa mwanachama objective kunakosesha usingizi lakini hukoseshwi usingizi na mafisadi kina Lowassa, Chenge, na Karamagi kuendela kuwa wanachama wa CCM??
Mbona hujawahi kuuliza kuhusu uanachama wao wa CCM? Lakini umekoseshwa raha na objectivity yangu ya ku-question political leadership wisdom ya waziri wa umeme, ya kuwakimbia wananchi wakiwa hawana umeme, na yeye kwenda kufanya kampeni za chama ambacho tayari kina wabunge 90% ya bunge letu na bado tunalala na giza?

Wewe bila aibu unasema huyu waziri ni babu kubwa sana na kwamba anajiamini sana! Mungu alisaidie tu taifa hili maana tunaongozwa na vipofu na baadhi yetu wananchi nao ni viziwi na vipofu ndani yake! LoL!
 
Mkuu FMES, Kwanza Acha mambo ya speculation za uongo,Mhe Ngeleja Anajiamini sana katika nafasi aliyopo kwa sasa na hata Mhe. Rais ana Imani naye katika hili.Usitumie Ushaifu wa kwamba wewe ni mtu wa data kusema lile ambalo unafikiri litakunufaisha wewe na wengine.


Rais alimuona Ngeleja Mwanzoni kabisa,akampa unaibu wa Wizara hiyo na baadaye akampa uwaziri kamili.Suala la Umeme litashughulikiwa na Songas na watendaji wengine wa wizara,suala ni dogo na ni la kifaa tu na siyo tatizo kama la kipindi kile cha RDC.Au unamtafuta ili ukalete mafundi wa hicho kifaa??


Kusema ana jikomba haumtendei haki kabisa,Yeye ni WMana CCM na ana Haki ya kutetea sera za chama chake bila kuingiliwa na Mtu yeyote.Na suala la viongozi wengi wa CCM wanapenda kampeni za |Mjini ni Uongo ulio kubuhu,Wartu walienda Kiteto na CCM ikashinda.

Basi kwa taarifa yako tu.,CCM itaibuka na ushindi wa kishindo kati9ka jimbo la TARIME na usitegeemee CHADEMA hii ya Mbowe na Ukabila wao watapewa dhamana hapo TARIME.The same happening in Kiteto will happen in TARIME.

Screw CHADEMA and FMES na Ngelejha Ana jihamini kwa kuwa yeye ni Bora

Yaani wewe badala ya kumuonea huruma NGELEJA ndio unampa ushujaa? Unadhani yeye kama waziri wa nishati na madini kwenda kupanda jukwaani sehemu kama NYAMONGO ambako umeme upo kwenye mgodi wa wazungu tu na wananchi wengine wote wakitumia koroboi miaka nenda miaka rudi wakiwa wamezunguka utajiri wao wa dhahabu unaokwapuliwa na wazungu ni uamuzi sahihi kweli? Waziri wa madini wa serikali iliyowapora Wananyamongo madini yao na kusimamia mauaji na mateso ya vijana wao kila kukicha awe ndio chaguo la kwenda kuokoa kiti Tarime?

Ni kweli kwamba NGELEJA anahitaji kujijengea base ndani ya CCM kuepuka msalaba wa kutegemea nguvu za Rostam but not in a stupid way like this.

Halafu ina maana hawakuwa na taarifa ya kuja kwa Zitto ambaye ni wazi angefunika ujio wa kijana mwenzao NGELEJA huko?

Halafu jana anaibukia VODACOM ambako ndio link kubwa kwake na ROSTAM? Hata kama alikuwa mwajiriwa pale lakini mazingira ya sasa na hatma yake inapaswa kuepuka hilo kwa nguvu zote....

Tafadhali mpeni mawazo mazuri kijana mwenzetu ambaye naamini personally ni kijana mzuri ambaye anaweza kuwa msaada mkubwa wa chama chenu huko mbeleni kama mtamlinda na hiki kimbunga cha sasa..........

Tanzanianjema
 
Mkuu MFES,

Umeme Umerdi sasa,Naomba tuwapongeze Mafundi kwa kufanya kazi kwa haraka na ufanisi.Mgao hakuana tena.

Mkuu FMEs,siyo kwamba mie sipendi mapinduzi ya ksisiasa,ila nimeshakerwa sana na jinsi hivi vyama bvinavyovunja umoja wao kwa sababu ya chama kimoja kujiona kiko juu zaidi ya chama kingine.

Lengo lao ni kutafuta fursa za madaraka nia siyo kutukomboa wapinzani,Mie niko katika upande wa kutetea jambo lenye Maslahi kitaifa,ila linalohusu kutetea chama siko kabisa na nitasimamia CCM.Hata mama Kilango huwa anasimamia CCM kipindi cha Kampeni ila akija Bungeni anakazia na kutetea Maslahi ya taifa.

Lengo hapa siyo kusema kwamba Ngeleja Alipuuzia,kama nilivyosema awali kipindi kile,Ninamfahamu mhe. ngeleaj zaidi ya miaka 20 iliyopita hivyo speculation za uongo hazisaidii popote.Umeme umerudi na Tumuache akissaidie chama kupata ushindi.

Mkuu FMES tupo pamoja katika kumkoma nyani Giladi mchana kweupe ila siyo kumchafua mtu kwa hoja dhaifu katika thread zetu.

Lunyungu??

Mod tufunge hii na turudi Tarime
 
siyo kwamba mie sipendi mapinduzi ya ksisiasa,ila nimeshakerwa sana na jinsi hivi vyama bvinavyovunja umoja wao kwa sababu ya chama kimoja kujiona kiko juu zaidi ya chama kingine.

Sawa sawa nimekusikia mkuu, unajua kama nilivyosema kuwa siku zote ninaheshimu sana msimamo wako, ingawa kwenye hii quote sina uhakika kama una all the facts au kama ni the truth, lakini heshima mbele tuendelee kukata ishus taifa liko njia panda Mkuu Gembe!
 
Hongereni kwa mjadala mkali sana... lau kama ninyi mngekuwa wapiga kura ningeheshimu sana maoni yenu... lakini lakusikitisha ni kwamba ninyi sio miongoni mwao. Kwa hivyo matokeo ya mjadala huu ni porojo tu za mtaani...

Nawatakia kila la kheri kwenye jamvi lenu.

Eid Mubaraka.
 
Back
Top Bottom