Ngoja niandike kidogo kuhusu Kariakoo Derby

Matanga

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2019
Posts
2,281
Reaction score
3,976
KARIAKOO DERBY 'THE AFRICAN EL CLASSICO' NA KUTUNZA INARUHUSIWA
.
Imenichukua miaka kushuhudia punching saves Kama za Leo Alizofanya Shikalo, imenichukua muda kuona crazy footwork Goalkeeper Kama Huyu Shikalo , huyu Farouk Shikalo ni sweeper hatari mno Kajitahid Sana Na Hapa Anaonekana Vile pia Kutokana Na Performance Mbovu ya Manula Mpaka Nikajiuliza Benno Kwanini Bado Yupo Njee
.
Imenichukua muda kushuhudia Kocha wa Kitanzania mwenye uwezo mkubwa wa kuusoma mchezo na kufanya twists za akili, Yanga waliingia na 4-2-3-1 ila kipindi cha pili wakajivua kwenda 4-4-2, lengo ni kujilinda ila kuminya uwanja kufanya Simba wasitanuke
.
Itanichukua muda kumshuhudia The Darling Football Maestro Haruna Fadhili Hakizimana Niyonzima Fabregas wa Majengo Gisenyi pale Rwanda, alianza kama winger, akamaliza kama central midfielder, aliutanua uwanja zile piercing passes, wing switcher passes na mwishoni alitumika kwenye recycling
.
Simba walikuwa na mpira, wakimiliki na viungo wengi ila walikosa last man, mtu wa kuzitumia vizuri zile nafasi zao, plan nyingi zilifia kabla ya kuigusa 18, plan B ya Simba ni kasi za wings Ni wazi Kabisa Tulimhitaji Ibrahim Ajibu Migomba Fundi
.
Deo Kanda is one hell of a brilliant footballer, miguu ya almasi, akili ya dhahabu, jicho la Mwewe na mnuso wa bundi, anaujua mpira, anazijua nafasi na mwishoni ni goal getter mzuri, Kahata alipungua baada ya Deo kutoka Na Hapa Ndipo kasi ya Wings Ilipungua Kwa Maana ya Kubaki na mtu Wa Mbio na Mwenye Uwezo Wa Kuchukua Wawili Watatu Ambae ni Dilunga Sukari hii Kwasababu Tayari Kahata Energy Ilikua Imepungua Hakuweza Tena Kukimbia na Kuludi kwa Kasi Sahihi
.
Adeyum imenichukua muda kuziona Parabola crosses, imenichukua muda kuona mchimbo kama ule Uliozaa Bao kupitia kwa Mo Banka
.
MO Banka amenikumbusha Athuman Chuji, sikumbuki lini Tanzania imekuwa na kiungo mwenye mapafu ya mbwa, alikuwepo kila eneo, alikaba, alichezesha na kufunga, aliwatanya Simba atakavyo Pamoja Na Tshishimbi Good performance Kaonyesha tena Haswa Baada ya Kuludi Kiungo cha chini
.
Kuna kitu kilikosekana kwenye kiungo cha Simba, Patten ya Mkude na Mzamiru haziendani, wana ladha tofauti za pass na marking, wana shida kwenye coordination, muda wa kukaa na muda wa kuitoa timu Hapa Sasa Nilimhitaji Fraga kwa Maana ya Kukata Umeme Kisha Mkude Akabaki Kusambaza Upendo So Far So Bad Makosa Yapo Kwa Mpira na Lazima Uadhibiwe Ukiyatenda Maeneo Sahihi kwa Mpinzani
.
Sema Wananchi[emoji1] pale kati leo, kuna muda wanakaa triangle, kuna wakati parallel pattern, kuna muda trapezium, wanakuita unakuja wanasepa [emoji38] Romantic

.
Yule mtoto Balama ni wa Iringa kweli, long range bullet Ile, sukari sana kama ile text 'Baby nishukie Wapi.


Sven Kuna Mda Alionekana kama Anataka Kushindwa Kutuliza Ile Presha ya Yanga Pindi Walipoinuka na Kupata Nguvu ya Kushambulia Lakin Alikuja Kupata Idea Ambayo Kidogo Ilituliza Presha Kidogo na Simba Wakaanza Kutembea Vizuri.

All in all Football Ndivyo Ilivyo Simba Tulihitaji Point Tatu Lakin Zimekosa na Tumepata Moja Same to Yanga Lakin Ukweli Utabaki Pale pale Kua Simba Game Ilikua Mikononi Mwake Kajinyima Haki Aliyostahiki, Tuendelee Kuuheshimu Mpira Utatuheshimu Pia It Was a Kariakoo Derby Baby Wacha Nikuache Nichukue Zangu Urojo Niendeleze Kutuliza Presha ya Kupata Mrembo mkali Toka Mitaa ya Kigali Rwanda Kwa Utulivu Mzuri
Usiku mwema kwenu wote[emoji120]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakubaliana na wewe kwenye kumuacha Fraga, kwa sababu Mkude hawezi kucheza majukumu ya Fraga.

Kwenye mechi ya nguvu kama ile walimhitaji sana Fraga, angeweza kuwatuliza sana Yanga.

Pia ni kosa la pili wanafanya Simba kumpanga Manula kwenye mechi kubwa. La kwanza ni UD Songo na leo tena.
Big mechi mpeni Kakolanya, huwezi kumfunga magoli ya kitoto.

Kwangu mimi Beno ni one of the best goalkeepers TZ, ni makosa sana kumuweka bench.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Noted [emoji120]
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naongezea, Simba hawana pumzi ya kucheza dk 90 kwa kasi ile, hivyo kukosa fiziki haswa kipindi cha pili. Ila Kanda yuko vizuri yule MTU.
Huo ni muendelezo wa kocha Aussems, hakuwa anawapa mazoezi ya kutosha, bata zilikuwa nyingi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huo ni muendelezo wa kocha Aussems, hakuwa anawapa mazoezi ya kutosha, bata zilikuwa nyingi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hukosi pakushika, haya mshaurini Hutu wa sasa awapunguzie kula bata. Ila Kanda jamani....Hugo Kagere baada ya kuchomolewa power bank na nguvu zikamuishia kabisaa
 
Naongezea, Simba hawana pumzi ya kucheza dk 90 kwa kasi ile, hivyo kukosa fiziki haswa kipindi cha pili. Ila Kanda yuko vizuri yule MTU.
Hahahaha na pale ndio kaja kachuja ,enzi zake huyo balaa ,ila tu asianze pozi zake zile za kamalondo

MTC | 101| [emoji769]
 
Manula yuko vizuri kuliko Kakolanya acheni kujidanganya. Yale magoli ya Yanga goalkeeper yeyote including Degea anafungwa.
 
Hii mada ni ya kipumbavu sijawahi ona

Sema nimeipenda sehem moja tu (baby nishuke wapi?) Hii msg hakika huwa ni Asali

Sema punguzen kutumia power bank

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kifupi kocha wa simba na matola wake ni wehu kumuweka kenedy katika benchi kulikuwa na maana gani.wakati tayari.nyoni yupo.
Kuwa kwanini shiboub n fraga wasingechukua hiyo nafasi maana kuna muda chama alionekana kuhitaji msaada.
Kifupi droo wameipanga benchi la ufundi la.simba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hukosi pakushika, haya mshaurini Hutu wa sasa awapunguzie kula bata. Ila Kanda jamani....Hugo Kagere baada ya kuchomolewa power bank na nguvu zikamuishia kabisaa
Dunia ni eneo la wazi huhakikishie ilikuwa powerbank? Maana wote tumeona ilikuwa ni nini?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fraga Alistahili mechi hii
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hicho ki fraga nnakuhakikishia mngekifukuza Jana. Hakina uwezo wa kucheza game yenye presha kama ile
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…