Ngoma na miziki yote kwa sasa inapigwa Lumumba, Ufipa wamebaki kudemka tu!!

Ngoma na miziki yote kwa sasa inapigwa Lumumba, Ufipa wamebaki kudemka tu!!

"Tumewaondoa" mimi na nani? Tatizo mnafikiri kila anaetoa ushauri ambao hamjaupenda basi ni upande wa CCM. Hizo siyo siasa ni ushabiki, na CDM wengi wapi hivyo. Sawa mmeminywa uhuru wa kujieleza lakini bado mmeweza kuongelea katiba mpya. Jukwaa mliloongelea katiba mpya ndiyo hilo mngeongelea unyonyaji kwa wakulima wa korodho, kahawa na mahindi, tatizo la ajira nk. Mambo yanayogusa wananchi.
Mbowe anafanya nini kwa kesi ya ugaidi kule mahabusu kama siyo swla kuongelea katiba mpya??
 
Mbowe anafanya nini kwa kesi ya ugaidi kule mahabusu kama siyo swla kuongelea katiba mpya??
Kama mtoa maada alivyosema, ishu ya katiba mpya haimgusi mwananchi na ni kazi mwananchi kuielewa. Unafikiri mkulima huko Namtumbo anajua chochote juu ya katiba mpya.
 
Mbona Dua lishampata mkuu, saizi yuko pale chato anaoza tu[emoji91][emoji91][emoji91]
Hayo ni mawazo finyu na inaonesha ulipo na nafasi yako katika jamii ya wastaarabu! Zungumzia walio HAI achana na siasa za TOBO za kuzungumzia HAYATIs! Au ukipenda na kama unaweza basi zungumzia your MAREHEMUs! Naamini unajua tofauti kati yao!
 
Kama mtoa maada alivyosema, ishu ya katiba mpya haimgusi mwananchi na ni kazi mwananchi kuielewa. Unafikiri mkulima huko Namtumbo anajua chochote juu ya katiba mpya.
Kwa hiyo mkaamua kumsingizia Mbowe kesi ya ugaidi ili kuzima mchakato wa Katiba mpya yenye faida kwako na kwa mkulima wa Namtumbo pamoja na ccm wote wa kizazi cha leo na kizazi kijacho.
 
Hayo ni mawazo finyu na inaonesha ulipo na nafasi yako katika jamii ya wastaarabu! Zungumzia walio HAI achana na siasa za TOBO za kuzungumzia HAYATIs! Au ukipenda na kama unaweza basi zungumzia your MAREHEMUs! Naamini unajua tofauti kati yao!
Chanzo cha matatizo ya leo ni Marehemu,haongelewi kama kebehi bali mfano kwa walio hai wasije rudia upumbavu wa mwendazake.
 
Kwa hiyo mkaamua kumsingizia Mbowe kesi ya ugaidi ili kuzima mchakato wa Katiba mpya yenye faida kwako na kwa mkulima wa Namtumbo pamoja na ccm wote wa kizazi cha leo na kizazi kijacho.
Wakulima huku Namtumbo hatujui jinsi katiba mpya itakavyoongeza bei ya mahindi yetu na kushusha gharama za mbolea. Msimu wa kilimo unaanza, tunahitaji mbolea ya bei ndogo.
 
Kwa hiyo mkaamua kumsingizia Mbowe kesi ya ugaidi ili kuzima mchakato wa Katiba mpya yenye faida kwako na kwa mkulima wa Namtumbo pamoja na ccm wote wa kizazi cha leo na kizazi kijacho.
Hivi kwa akili yako unadhani kelele za mbowe zingeweza kutisha kwa kiwango cha kusababisha serikali irudishe mchakato wa katiba mpya!?
 
Hivi kwa akili yako unadhani kelele za mbowe zingeweza kutisha kwa kiwango cha kusababisha serikali irudishe mchakato wa katiba mpya!?
Na kwa bahati mbaya ni kwamba ccm hujitetea kwamba serikali yake iliruhusu mchakato wa kuandika katiba mpya na ikatumia mabilioni ya pesa ila haohao wapinzani walisusia mchakato leo hii wanataka nini ni wasumbufu tu!!
 
Itatuchukua muda mrefu kupata tena kizazi chenye uthubutu wa kufanya siasa za upinzani za kinchi
 
L

Lete hoja na uthibitisho kuwa "matatizo" ya leo yaliletwa na shujaa wetu JPM, mnaye muita hayo majina! Lete hoja twende kazi!
Hoja ni hiyo hiyo mkuu usilete ubabaishaji,kwanza wabunge wa vyama vya upinzani wam
Wakulima huku Namtumbo hatujui jinsi katiba mpya itakavyoongeza bei ya mahindi yetu na kushusha gharama za mbolea. Msimu wa kilimo unaanza, tunahitaji mbolea ya bei ndogo.
Wakulima wa Namtumbo hawawezi elewa hatima yao ya bei za mazao yao kama hawana katiba imara inayotambuwa haki na wajibu wa kila mwananchi kuanzia raia wa kawaida hadi viongozi wakuu wa Serikali,kumbuka katiba imara chanzo cha maendeleo endelevu.
 
Hivi kwa akili yako unadhani kelele za mbowe zingeweza kutisha kwa kiwango cha kusababisha serikali irudishe mchakato wa katiba mpya!?
Ndiyo maana wakamfungulia kesi ya ugaidi ili kumpotezea muda na kuwavuruga chadema kisaikolojia.
 
Anzisheni kampeni zinazogusa hisia za wananchi walio wengi na si hoja za kufikirika kama vile chadema dijito mara katiba mpya twende na mambo ambayo hata wanaccm wa kawaida kabisa yatawaingia kichwani mf. Ukimuambia mtu napigania tozo iondolewe au napambana machinga warudishwe maeneo yao au walipwe fidia baada ya kuondolewa hapo hata raia wa kawaida awe ccm au chadema ataona unapigania maslahi yake lkn hii mambo yenu itaua chama
KWANI weye waanza na ipi hapo? Lini?
 
Inavyoonekana siasa za nchi hii zimeelemewa na CCM maana pamoja na wapinzani kuwa katikati ya changamoto lukuki, bado habari zao hazipewi nafasi kubwa ya kuzungumzwa hasa humu mitandaoni.

Kwa muda mrefu sana majina yaliyovutia mijadala mingi ni pamoja na Samia, Polepole, Nape, Sabaya, Shaka, Ndugai, Msukuma, Mwendazake, nk.

Hawa wote ni makada wa CCM.

Kwenye siasa kutajwatajwa na kujadiliwa na watu whether positively or negatively ni afya.

Ukiacha Covid-19 na kesi ya ugaidi ya mwenyekiti hakuna jina lingine Kutoka upinzani linalovutia mijadala ya watanzania.

Cha ajabu ni kwamba kumetokea fursa za wapinzani kuibukia ila hawajazitumia sijui kwa nini.

Masuala kama machinga,kupanda kwa bei, tozo, ukosefu wa mbolea, nk. Haya yalikua jukwaa rahisi sana kwa wapinzani, ila nadhani kufanya siasa za mazoea kunawafanya wakomae na madai hewa ya katiba mpya.
Utasikia wapi habari za chadema wakati habari zinazotamba ni za ndugai kubwabwaja kuhusu udhaifu wake hadi kutishia kuwashughulikia wanaomsema na habari za mkurugenzi mkuu wa TPDC kukana tamko lake la uhaba wa mafuta?
 
Inavyoonekana siasa za nchi hii zimeelemewa na CCM maana pamoja na wapinzani kuwa katikati ya changamoto lukuki, bado habari zao hazipewi nafasi kubwa ya kuzungumzwa hasa humu mitandaoni.

Kwa muda mrefu sana majina yaliyovutia mijadala mingi ni pamoja na Samia, Polepole, Nape, Sabaya, Shaka, Ndugai, Msukuma, Mwendazake, nk.

Hawa wote ni makada wa CCM.

Kwenye siasa kutajwatajwa na kujadiliwa na watu whether positively or negatively ni afya.

Ukiacha Covid-19 na kesi ya ugaidi ya mwenyekiti hakuna jina lingine Kutoka upinzani linalovutia mijadala ya watanzania.

Cha ajabu ni kwamba kumetokea fursa za wapinzani kuibukia ila hawajazitumia sijui kwa nini.

Masuala kama machinga,kupanda kwa bei, tozo, ukosefu wa mbolea, nk. Haya yalikua jukwaa rahisi sana kwa wapinzani, ila nadhani kufanya siasa za mazoea kunawafanya wakomae na madai hewa ya katiba mpya.
Hakuna wapinzani now
 
Back
Top Bottom