Ngoma ngumu kwa Mamelody, washusha kiingilio. Injinia awashika pabaya

Ngoma ngumu kwa Mamelody, washusha kiingilio. Injinia awashika pabaya

Yanga na Mamelodi wamekutana wajanja kwa wajanja wote Njano-Kijani.

Wote wanaogopana. Mwazoni mara baada ya droo kupangwa, Yanga iliiogopa sana Mamelodi ndipo wakaanza kampeini ya kujijengea confidence kwa nguvu sana. Ila sasa hivi baada ya mechi ya kwanza kibao kimegeukia kwa Mamemodi ndio wanaonyesha kuigopa sana Yanga.

Leo nilikuwa nasikiliza commentaries za wachambuzi wa mchezo huo kwenye TV moja ya Afrika ya kusini, inaonyesha kuwa mamelodi wanaogopa Stamina, teamwork na kasi ya Yanga. Kwa sasa hivi mbinu yao kubwa ni kuanza mchezo kwa kasi sana na kupata bao moja la harakaharaka halafu walilinde. Wanaonyesha kuwa ikifika dakika 30 hawajapata bao basi wajichukulie wamepteza mchezo kwani wana hofu kuwa huenda hawataweza kuhimili kasi ya Yanga katika kipindi cha pili.
Hili ndilo nawaambia washkaji tangu jana kuwa ikifika mpaka dakika 30 kipindi cha kwanza Mamelody hajapata goli watakuwa frustrated sana na hapo ndipo watapoteza mchezo.
 
Yanga haiwezi kufunguka, mechi itaisha mapema. Yanga atacheza kwa umakini na kujilinda
Ile game ya Lupaso plan yao ilifeli ila acha tuone leo maana kila timu itakua inatafuta goli,,,na wao plan ilikua jamaa wasogee,leo sidhani kama Yanga itapaki bus
 
Mpaka ninapoandika sasa hivi zimebaki dakika 70 gemu lianze. Ninapata kiherehere chenye mchanganyiko wa furaha na hofu.

Ninafuraha kuwa huenda nafasi yetu imefika kwenda nusu fainali hadi fainali za CAF na kuleta medali nyingine tena, na pia napata hofu kuwa huenda furaha yetu ikafikia ukingoni kwa kukatiriwa na refa. Najaribu kuvuta kiti nikae halafu naishia kusimama tu, nikichukua glassi ya bia, najikuta naichanganya na sukari halafu ninaimwaga yote chini.

Basi kiherehere kimenizidi sana kutokana na kusubiri mchezo huu.

Mikono imeanza kunitetekemeka naangusha vitu bila mpangilio, moyo unakwenda kasi navuta pumzi harakaharaka, kijasho chembamba kinanichuruzika uso wote. Mwenzenu kiherehere cha mchezo kimenizidi nguvu.


Nasubiri kuwafungasha Mamelodi kwenye bahasha ya plastiki, kuiwekea stemp na kuituma
PO Box 8713, Edleen, 1625, South Africa ikasubiri tutakapokutana tena mwakani
 
mfuga majini anajifariji kweli mara mamelody wanatetemeka mara mamelody atafungwa jamaa ata haeleweki point yake ni ipi baada aendelee kulisha majini yake anaangaika na Sun down
Na hawa jamaa wakishinda,na wale wa kule Uarabuni washindwe, sijui kama TUTAPUMUA!
 
Mwanzoni Mamelody waliweka kiingilio Rands 20 .

Then Injinia wa mpira, Hersi Said akatangaza kiingilio bure kwa kila shabiki wa Yanga atakae ingia uwanjani loftus kuwaspoti Yanga ( umewekwa utaratibu wa kuwalipia mashabiki wote wa Yanga watakao ingia uwanjani leo)

Mamelody wametangaza kushusha kiingilio na sasa imekuwa Rands 10.

Ni wazi kuwa wameshusha kiingilio baada ya kuona muitikio mdogo huku Yanga wakionekana kuzidi kupata sapoti kubwa kutoka kwa:

1. Mashabiki wa Yanga ( mabaharia wanao ishi Dizonga ambao wapo wengi sana)


2. Mashabiki wa Yanga kutoka Dsm( waliolipiwa na serikali) pamoja na wengine walio enda wao kama wao kutoka sehemu mbalimbali Tanzania huku wengi wao wakitoka Mbeya.

3. Mashabiki wa Kaizer Chiefs ambao wanakuja kulipa fadhili za mashabiki wa Yanga walivyo wasapoti kwenye mechi yao dhidi ya Taifa Lupaso.


4. Mashabiki wa the Pirates

Leo Soweto yote ni kijani na njano ya Yanga. Bahati nzuri kutoka Joburg hadi Pretoria ni kama Dar na kibaha ( only one hour )


Halla Young Africans
Hata uwanja wote ukijazwa na mashaabiki kutoka Tanganyika kipigo kiko palepale.
 
Yanga na Mamelodi wamekutana wajanja kwa wajanja wote Njano-Kijani.

Wote wanaogopana. Mwazoni mara baada ya droo kupangwa, Yanga iliiogopa sana Mamelodi ndipo wakaanza kampeini ya kujijengea confidence kwa nguvu sana. Ila sasa hivi baada ya mechi ya kwanza kibao kimegeukia kwa Mamemodi ndio wanaonyesha kuigopa sana Yanga.

Leo nilikuwa nasikiliza commentaries za wachambuzi wa mchezo huo kwenye TV moja ya Afrika ya kusini, inaonyesha kuwa mamelodi wanaogopa Stamina, teamwork na kasi ya Yanga. Kwa sasa hivi mbinu yao kubwa ni kuanza mchezo kwa kasi sana na kupata bao moja la harakaharaka halafu walilinde. Wanaonyesha kuwa ikifika dakika 30 hawajapata bao basi wajichukulie wamepteza mchezo kwani wana hofu kuwa huenda hawataweza kuhimili kasi ya Yanga katika kipindi cha pili.
Kaka kaka haya mambo hayana mwenyewe lakini all in all tunaiombea Young Africans.
 
Yanga haiwezi kufunguka, mechi itaisha mapema. Yanga atacheza kwa umakini na kujilinda
Sema kwa kujilinda Yanga kupata goli ishu labda iende penalt , ila mpira dakika 90 lolote linawezekana,,ishu kwa kujilinda kama wangekua na mtu clinical kwenye umaliziaji ingekua uhakika, maana ukiwa unalinda ukipata chance chache lazima uzitumie shida Yanga kwa game tulizoona anakua na attempt nyingi ndo apate goli,, kwa kujilinda wacheze kama al ahly alivyokua Lupaso kapata chance kapiga goli karudi kulinda kamuacha Simba acheze, hata leo labda wapate goli mapema halaf wawaache Sundowns wanahangaika ila wasipokua clinical kumalizia ni kilio
 
Hamu yangu ni kujua kikosi cha Yanga kitachooanza leo.
hiki hapa
20240405_201744.jpg
 
Mpaka ninapoandika sasa hivi zimebaki dakika 70 gemu lianze. Ninapata kiherehere chenye mchanganyiko wa furaha na hofu.

Ninafuraha kuwa huenda nafasi yetu imefika kwenda nusu fainali hadi fainali za CAF na kuleta medali nyingine tena, na pia napata hofu kuwa huenda furaha yetu ikafikia ukingoni kwa kukatiriwa na refa. Najaribu kuvuta kiti nikae halafu naishia kusimama tu, nikichukua glassi ya bia, najikuta naichanganya na sukari halafu ninaimwaga yote chini.

Basi kiherehere kimenizidi sana kutokana na kusubiri mchezo huu.

Mikono imeanza kunitetekemeka naangusha vitu bila mpangilio, moyo unakwenda kasi navuta pumzi harakaharaka, kijasho chembamba kinanichuruzika uso wote. Mwenzenu kiherehere cha mchezo kimenizidi nguvu.


Nasubiri kuwafungasha Mamelodi kwenye bahasha ya plastiki, kuiwekea stemp na kuituma
PO Box 8713, Edleen, 1625, South Africa ikasubiri tutakapokutana tena mwakani
Zimebaki dakika 35.

Bia imeanza kuwa chungu mdomoni mwangu kwa vile kiherehere cha mchezo kiazidi kupanda joto
 
haya sasa; mchezo umeanza. Nimefunga mdomo wako na kukodolea box lenye sinema mebel yangu. Sina amani kabisa moyoni baada ya kugudua kuwa Aucho na Pacome hawamo hata kwenye list ya substitutes.
 
Back
Top Bottom