Ngonjera za Mwigulu Kuhusu Tozo Hazikubaliki

Ngonjera za Mwigulu Kuhusu Tozo Hazikubaliki

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Leo wananchi tumesikia kile kilichoitwa kuondoa na kupunguza tozo, kama Serikali ilivyofafanua kupitia waziri wake wa Fedha, Bwana Mwigulu.

Ukweli kilichofanyila ni ubabaishaji. Serikali haijajibu hoja ya msingi ya wananchi.

Tumetamka wazi kuwa tozo ni wizi. Ni unyang'anyi wa pesa ya mwananchi. Tuna sheria ya kodi. Sheria hiyo ya kodi inatamka wazi juu ya kodi ambazo mwananchi anastahili kulipa. Na viwango hivyo vya kodi hubadilishwa kila inapobidi kwa kupeleka mswada bungeni (bahati mbaya awamu hii hatuna wabunge wa wananchi, wapo waliopachikwa baada ya kuvuruga uchavuzi wa 2020).

Kila raia, anastahili kuipa Serikali sehemu ya mapato yake, kama sheria ya kodi inavyoanisha. Kwa hiyo kodi ni sehemu ya faida/mapato ambayo mlipa kodi ameyapata. Sasa ninapomtumia fedha kidogo mama yangu huko kijijini, nimetengeneza faida gani au ni mapato gani nimeyatengeneza? Au nimeambiwa kuna msiba umetokea, naamua kutuma mchamgo kwaajili ya kusafirisha mwili wa marehemu, au kununulia jeneza, au fedha ya kumtibia ndugu yangu, mimi nimetengeneza faida gani kwa hilo tendo mpaka nilipe kodi?

Tozo inaweza kuwepo kama dharula. Kwa mfano kumetokea maafa ndani ya nchi yetu, Serikali inataka kuwasaidia walioathririka au kurudisha miundombinu iliyoharibiwa na janga fulani, tunaweza kukubaliana kuchangia kupunguza makali ya maafa kwa kuweka tozo ya muda mfupi kwenye huduma fulani, LAKINI HAISTAHILI KUFANYWA KAMA NDIYO CHAMZO CHA MAPATO YA SERIKALI.

MAPATO YA SERIKALI YABAKIE KWENYE KODI. TOZO ZOTE ZIONDOLEWE.

Kubadilisha badilisha majina, wakati hela inaenda kule kule, ni kuwapumbaza wananchi. Hizo tozo zipelekwe kwenye kodi, ili tujue kwa uwazi kuwa pengine VAT imepanda mpanda mpaka 25% badala ya 18%. Lakini tusipumbazwe akili kwa kuweka majina tofaiti wakati kiuhalisia Serikali imeamua kupandisha viwango vya kodi.
 
Kiufupi, hayo marekebisho ya kisanii aliyofanya Mwigulu hayajamsaidia chochote mtanzania wa kawaida, na anaposema anaenda kufidia kwa kuondoa chai zao ofisini, badala ya kusema wanapunguza idadi ya v8, hapo ndipo inaonesha kile walichoondoa kwenye tozo ni kidogo sana.
 
Mwigulu ajiuzulu,asisubiri kutolewa!
Kazi imemshinda,amsaidie/amrahisishie Mama
 
Mwigulu ajiuzulu,asisubiri kutolewa!
Kazi imemshinda,amsaidie/amrahisishie Mama
Kwanza, ka laiti tumgekuwa tuna Serikali inayoheshimu umma, Mwigulu hakustahili hata kujiuzulu, bali alitakiwa kufukuzwa.

Watu wanalalamikia tozo, wanatoa maoni yao, yeye kwa jeuri ya madaraka anathubutu kuwaambia wananchi eti wasiotaka tozo wahamie Burundi!! Ala! Yaani yeye ni nani hata afikie kuwaambia wananchi wahame nchi?

Tunamwambia Mwigulu, kama hataki kufanya ambayo umma unataka, ahamie Somalia.

Mtu mmoja Mwigulu, hawezi kuwa bora kuzidi sisi Watanzania wote katika umoja wetu. Sasa hiyo jeuri ya Mwigulu ya kutuambia sisi wote eti tuhame nchi anaitoa wapi?

Na Rais Samia, kwa nini hujamfukuza Mwigulu uwaziri mpaka leo, licha ya yeye Mwigulu, mara mbili kuwadharau wananchi?
 
Mwigulu anampotosha Mama makusudi kwa kujidanganya kwamba yeye ndio atatufaa zaidi kwa urais 2025!
Maskini akipata daima huwa ni shida kwa jamii!!.
Kwa nini amekubali kupotoshwa? Acheni hizo anajua kila kitu na labda ndio mwanzilishi yule ni mtekelezaji tu
 
Hii serikali ya mama inajitafutia yenyewe laana. Watu wanalalamikia hizi tozo moaka vijijini! Siyo vijana, siyo wazee! Wote ni vilio tu.
 
Hii serikali ya mama inajitafutia yenyewe laana. Watu wanalalamikia hizi tozo moaka vijijini! Siyo vijana, siyo wazee! Wote ni vilio tu.
Watu wanapoambiwa umuhimu wa katiba inayolinda mamlaka ya wananchi, mara nyingi hawaelewi. Kama tungekuwa ni nchi huru inayoheshimu misingi ya demokrasia, watawala wangekuwa wanajali sana malalamiko ya umma. Lakini kwa sasa, hata wananchi walalamike vipi, watawala wanaweza kuamua kupuuza, wananchi watafanya nini? Kama ni kura wakati wa uchaguzi,watazipata kura toka Tume yao ya uchaguzi.
 
Leo wananchi tumesikia kile kilichoitwa kuondoa na kupunguza tozo, kama Serikali ilivyofafanua kupitia waziri wake wa Fedha, Bwana Mwigulu.

Ukweli kilichofanyila ni ubabaishaji. Serikali haijajibu hoja ya msingi ya wananchi.

Tumetamka wazi kuwa tozo ni wizi. Ni unyang'anyi wa pesa ya mwananchi. Tuna sheria ya kodi. Sheria hiyo ya kodi inatamka wazi juu ya kodi ambazo mwananchi anastahili kulipa. Na viwango hivyo vya kodi hubadilishwa kila inapobidi kwa kupeleka mswada bungeni (bahati mbaya awamu hii hatuna wabunge wa wananchi, wapo waliopachikwa baada ya kuvuruga uchavuzi wa 2020).

Kila raia, anastahili kuipa Serikali sehemu ya mapato yake, kama sheria ya kodi inavyoanisha. Kwa hiyo kodi ni sehemu ya faida/mapato ambayo mlipa kodi ameyapata. Sasa ninapomtumia fedha kidogo mama yangu huko kijijini, nimetengeneza faida gani au ni mapato gani nimeyatengeneza? Au nimeambiwa kuna msiba umetokea, naamua kutuma mchamgo kwaajili ya kusafirisha mwili wa marehemu, au kununulia jeneza, au fedha ya kumtibia ndugu yangu, mimi nimetengeneza faida gani kwa hilo tendo mpaka nilipe kodi?

Tozo inaweza kuwepo kama dharula. Kwa mfano kumetokea maafa ndani ya nchi yetu, Serikali inataka kuwasaidia walioathririka au kurudisha miundombinu iliyoharibiwa na janga fulani, tunaweza kukubaliana kuchangia kupunguza makali ya maafa kwa kuweka tozo ya muda mfupi kwenye huduma fulani, LAKINI HAISTAHILI KUFANYWA KAMA NDIYO CHAMZO CHA MAPATO YA SERIKALI.

MAPATO YA SERIKALI YABAKIE KWENYE KODI. TOZO ZOTE ZIONDOLEWE.

Kubadilisha badilisha majina, wakati hela inaenda kule kule, ni kuwapumbaza wananchi. Hizo tozo zipelekwe kwenye kodi, ili tujue kwa uwazi kuwa pengine VAT imepanda mpanda mpaka 25% badala ya 18%. Lakini tusipumbazwe akili kwa kuweka majina tofaiti wakati kiuhalisia Serikali imeamua kupandisha viwango vya kodi.
Wauzieni wazungu makaa ya mawe kwa Bei nzuri tutapata pesa nyingi
 
Rais Samia kwa kulinda heshima yako tafadhari Sana mwaka 2025 usichukue form nenda kapumzike zenjibia
 
Tozo=wizi hilo halina ubishi...

Hawa jamaa wamevuruga sana biashara za watu, miamala imepungua sana...

Kama mimi nafanya transaction mara moja kwa mwezi inakuwa imeisha...

Nikitaka kutuma hela nampa wakala anatuma,, wanaumiza watu bila kujua...

Faida za tozo ni ndogo kulinganisha na hasara yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom