DJ SEPETU
JF-Expert Member
- Apr 17, 2017
- 8,413
- 12,336
Usiku Wa 5 oktoba,2017 ulishuhudia kwa Mara nyingine nguli Wa fasihi barani Afrika,mkenya aishiye USA, Ngugi Wa Thiongo akienda kulala tena pasina tunzo ya Nobel!
Tunzo hiyo jopo la wataalamu wameamua kumtunuku mwandishi mwingereza mwenye asili ya Japan, Kazuo Ishiguro,anayetamba Na novel kama vile the remains of the day,never let me go,Buried grant Na nk.
Hii si Mara ya kwanza kwa Ngugi kukosa tunzo hii,licha ya kujitwalia tunzo kadhaa,tunzo ya Nobel imekuwa mwiba mkali Na kihunzi kisichomithirika kwa Baba Wa fasihi Afrika,Ngugi Wa Thiongo. Amekuwa akiorodheshwa kuwania Mara kadhaa pasipo mafanikio.
Tunzo hii inayoambatana Na kitita kinono cha dola za kimarekani 1.1 milioni,zimekuwa zikiibua fursa Na kukuza hadhi ya msanii Na eneo atakalo Na kufungua milango kwa waandishi wachanga.
Mwandishi Ken waribora akihojiwa Na kituo cha redio dutchievelle cha ujerumani alisema kuwa kasumba Na mtizamo Wa kibaguzi Wa jopo linaloteuwa mshindi hutazama kazi za waafrika kwa jicho hasi,Na hii ni kwa kuwa watu weupe hupenda kusikia wakitakacho.
Tujadili ni kweli alichosema Ken waribora!?au waandishi Wa kiafrika bado sana kwa uwanda Na sifa za kazi zao kuweza kupata tunzo ya fasihi ya Nobel!?
Tunzo hiyo jopo la wataalamu wameamua kumtunuku mwandishi mwingereza mwenye asili ya Japan, Kazuo Ishiguro,anayetamba Na novel kama vile the remains of the day,never let me go,Buried grant Na nk.
Hii si Mara ya kwanza kwa Ngugi kukosa tunzo hii,licha ya kujitwalia tunzo kadhaa,tunzo ya Nobel imekuwa mwiba mkali Na kihunzi kisichomithirika kwa Baba Wa fasihi Afrika,Ngugi Wa Thiongo. Amekuwa akiorodheshwa kuwania Mara kadhaa pasipo mafanikio.
Tunzo hii inayoambatana Na kitita kinono cha dola za kimarekani 1.1 milioni,zimekuwa zikiibua fursa Na kukuza hadhi ya msanii Na eneo atakalo Na kufungua milango kwa waandishi wachanga.
Mwandishi Ken waribora akihojiwa Na kituo cha redio dutchievelle cha ujerumani alisema kuwa kasumba Na mtizamo Wa kibaguzi Wa jopo linaloteuwa mshindi hutazama kazi za waafrika kwa jicho hasi,Na hii ni kwa kuwa watu weupe hupenda kusikia wakitakacho.
Tujadili ni kweli alichosema Ken waribora!?au waandishi Wa kiafrika bado sana kwa uwanda Na sifa za kazi zao kuweza kupata tunzo ya fasihi ya Nobel!?