Nguli wa Gitaa Afrika, Diblo Dibala " Machine Gun"

........kuna Mtu anaitwa Saladin, alipiga na Soukous Star ya kina Shimita na Yondo Sister, solo yake ni ya umeme !
Jamaa alitambaa vizuri sana kwenye hiyo albam 'Soukous Star in Holywood'


Ebana Saladin humo aliitendea haki kiila nyimbo na ndio maana Shimita el Diego hakuchoka kumuita
 

diblo mwisho wa yote tafuta nyimbo ya diblo akiwa na bendi yake iliyoitwa machacha, wimbo wenyewe unaitwa machacha wetu,kuna solo imepigwa huko ni balaaa.
daly kimoko alianza kuvuma akiwa na ngouma lokito baadaye akiwa na alain nkonkou na sokous star level ya daly kimoko ni marehemu nene chakuu katika solo na sio diblo
 


Kama unataka kuzungumzia Kavasha basi usiache kuwataja Orcherster Veve, Orchester Shama, Orchester Fuka, Orchester Soliso, Orchestre Kiama nk nk nk nk...

Ila kuna kavasha mbili huwa nikizisikia hata kama ni msibani basi ni lazima ninyanyuke na kuacha kunyema..
1. Photo Madjest
2. Mikolo mileki mingi
 
ni kitu ya ukweli saana pia mkuu, ni Original Afirca Jazz music style..Bavon Marie..kaka yake na Afranco...alifariki mapema saana mwanzon wa miaka 70..
nadhan angekuwepo
 
Mkuu tafuta dvd ya "ok madame" kuna mwimbo unaitwa "2eme dance" kuna wadada wanakata mbungi kama hawana mfupa
 
Tafuta "2eme dance " nadhani ni wimbo wa 4 ktk album yake. Utafurahi na roho yako mkuu
 
Binafsi Diblo ndani ya The group loketo album Extra Ball alitisha sana. Dally Kimoko ndani ya Embargo album ya Aurlus Mabele pia alitisha mno pamoja na Stop! Arretez nayo album ya Aurlus Mabele.

Ni wazi kila mmoja wao ana ngoma ambazo amepewa shavu na amefunika kiasi kwamba unaona kabisa kama asingekuwa yeye wimbo ungekuwa tofauti.

Ndio maana ni ngumu kusema hasa nani ni mkali Wa jumla kwa kuwa hakuna version tofauti za wimbo mmoja mmoja ambazo labda version A kagonga Diblo kisha versionB kagonga Kimoko Dally.
 
Kwangu mie bingwa ni Dali kimoko
 
Asee hv hii namba 2 ndio ile ya John Bokila nn, akina baba na mama zetu walikuwa wanajiachia na marinda yao[emoji1]
 

Ndugu umenisononesha sana yaani King Diblo unamfananisha na Kimoko kweli??? hebu tulia relax halafu kamata kitu Mondo Ry hicho cha diblo....halafu utafakari tena kauli yako!!...

 

Mkuu Extra ball ziko version mbili ila zote za Aurlus Mabele na Loketo yake ..diblo kapiga mpini tuu ila nyimbo sio zake. ....alipoanzisha matchacha ndio akatoa zile ok madame ambazo pia zilikua kali!..diblo alitumika sana na loketo na kina bongoman na pepe kale alikuja kuanzisha bendi yake wakati keshaanza kuchoka na kuzeeka
 
Kuna Nene tchaku! Hyo nayo ni habari ingine katika solo
 
Mkuu upo sawa, lakini Dally Kimoko alipoulizwa alikiri Diblo anatisha
 
hivi huyu jamaa Ngou'ma loketo alikua anapiga gitaa la bass au lipi manake nyimbo nyingi za Aurlus Mabele Loketo alikua hamalizi wimbo bila kumtaja.
Ngou'ma lokito anapiga bass guitar
 
Kuna Nene tchaku! Hyo nayo ni habari ingine katika solo
Nene tchakou amehusika kwenye hits song nyingi za Kanda bongo man, kama vile Isambe, Wallow, yokela, bill, Sana, Liza, n.k pia kahusika kwenye nyimbo nyingi za soukous masters (Alain kounkou,) wenge alie Paris, solo sita, Code niawu, na nyingine nyingi.. gitaa lake lina vibe sana Aiseee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…