Nguo na scaf yake vilionekana kuwa na damu na maji yaliyotokea puani wakati akibanwa na python, aliyekuwa mkosoaji wa elimu ya mfalme wa Beirut

Kumuua Ben na kujaribu kumuua Lisu ni absolutely unnecessary decisions.
Hakukuwa na ulazima!
Bado ilifaa hoja zao kujibiwa kwa hoja.
Halafu watu wanashangaa Rais Samia anaposema viatu vya Magufuli havinitoshi!! Hivyo ndiyo viatu vyenyewe
 
Unajua kuna watu humu jukwaani ukiwaeleza matukio ya Mfalme wa Beirut wanakataa wanasema eti chuki binafsi sijui eti utakuwa Mhujumu nk
Lakini laiti wangekuwa wanaona yanayofanywa na yule bwana nyuma ya pazia kwa kutoa maelekezo hakika wengi wenu mtapigwa na butwaa kama sio kuzimia kabisa... Ni maajabu na unyama wa hali ya juu.. Watu wamepoteza maisha kwa stroke / BP kwa mkono wake..
Ngoja niwape kisa kimoja alichokifanya mwaka 2017.... Kuna bwana mmoja anamiliki semi trailer kama 50 hivi.. Mfanyabiashara wa muda mrefu
Sasa kulitokea mzozo wa wamiliki wa malori kipindi cha nyuma kuhusu kero za mizani kwamba kuna rushwa sana..
Lakini kulikuwa na matatizo ya faini kubwa sana wanalipishwa.. Sasa Mfalme alikuwa Waziri wa Ujenzi akawaambia faini hizo ni ndogo na akalazimisha kupitisha sheria kali sana ndogo ndogo kuhusu wamiliki wa Malori.
Huyo mfanyabiasha pamoja na wenzao wakaenda kwa Pinda kipindi hiko ni PM.. Busara ikatumika mambo yakatatuliwa mgogoro ukaisha..
Kumbe katika vikao vya usuluhishi Mfalme alimnote yule bwana kwakuwa alikuwa anatoa hoja sana ambazo yeye kama waziri alionekana anaonea..
Alipopata ufalme yule Mfanyabiashara alipata cha mtema kuni.. 2017 alinyooshwa semi trailer 10..yaani zilitaifishwa..na jamaa alikaa kimya ili awe salama.. Maana alijua nikijifanya mjuaji nitapotea humu Duniani
 
Yaani kwenye haya maelezo yako ya kufafanua habari za huyo mfalme wa Beiruti kama alivyo muelezea mtoa mada, umeharibu tu hapo kwenye neno:-

'Huyo Mfanyabiashara pamoja na wenzao wakaenda kwa Pinda kipindi hiko ni PM...' Kwingine kote ulipatia na binafsi nilikuelewa vizuri. Kasoro hapo tu. Kama vipi unaweza kurekebisha.
 
Wauaji huwa wanasahau kama na wao ni marehemu wanaotembea?
 
Utashangaa wajinga flani wanasifu wauaji wa watu wasiostahili kuuwawa maana hawakuwa na hatua.
Mfalme wa Beiruti tayari, Mungu mwenyewe atakuwa na mpango na wengine waliodhulumu uhai wa innocent citizens.
Mbona aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani.sasa ni waziri wa fedha.
KARMA NI UONGO?
 
Maisha ya binadamu aliyezaliwa na mwanamke Ni miaka sabini, ikizidi Ni miaka sabini na Saba.
Wakati mfalme wa Beiruit anafanya haya alikua sana sana amebakisha miaka kumi ya ku enjoy.
Starehe ya miaka kumi inakufanya ujipalilie Moto jehanam ya miaka thenashara?
 
Rest In Peace Ben Saanane
Rest in hell Dikteta Mwendakuzimu
 
Mwedawazimu alikua na kichaa kikali

Ndio Tabia za Walebanon hizo hawataki ushauri na wanaujuaji
Kuna mtu alimshauri zile amonite walizozikarisha pale bandarini ni hatari ila Kwa ukatili wake akawa anawapoteza mwingine akapigwa risasi zilizojaa full magazine mchana kweupe lakini yule mtu akasurvive kimiujiza,
Kutokana na ubishi zile amonite zikaripuka pale bandarini Beirut na kumwangamiza na yeye now ashakua Mwendakuzimu!

Ujuaji na roho mbaya mbele kiza
Haya Leo Yu wapi?
 
Aiseeh
 
Alimtoa kafara kwa mungu wake ambae nae kashindwa kuzuia kifo
 
Unaua mtu kisha nae unakufa inasaidia nini sasa,sio KILA koo damu ya familia zao ni za kutoa kafara zingine ni lzm ikitoka damu lzm irudi damu ya kufidia damu yao.
Huwezi ukakosoa uumbaji na ubaki salama
 
Jamaa alikuwa anafanya mambo ya uonevu na kikatili sana
 
Safi sana!

Kale ka kijana kalikuwa kajinga
 
Ni wakati sasa ukweli ujulikane, familia nayo ipate tulizo la kiakili kwa kujua kilichotokea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…