Nguvu ya Biashara ya Forex, Ujasusi na yaliyo nyuma ya pazia

Forex ni kamari, na unapomshawishi mtu akacheze kamari ili upate comission na broker fee huo ndio utapeli wenyewe. Solution ni kufanya kazi za uzalishaji mali/ huduma, hakuna shortcut. Zingine ulizosema hapo ni 'senseless rubbish'.
Ukiacha muktadha wa forex mkuu, unadhani watu wote wanaofanya kazi ya uzalishaji mali ndio wanasonga mbele?

1. Wapo wakulima wanalima na bado wanapata hasara e.g rejea wakulima wa mbazi na choroko kusini mwa Tz mwaka huu

2. Wapo watoa huduma mbali mbali ambao wamekwama na kufunga shuguli za utoaji huduma rejea mashirika ya serikali yaliyokufa na makampuni kama home shopping center yalivyofungwa

3. Wapo ambao walikuwa na viwanda wanazalisha bidhaa na mwishowe viwanda vimekufa e.g kiwanda cha nyumbu na vilikuwepo national milling na mashine kibao but viko wapi?

4. Wapo waliofungua maduka na wameshindwa kutengeneza faida tena wamepata hasara hadi mtaji unakufa kwenye biashara hiyo hiyo ambayo wengine wanatusua na kula maisha,

5. Yapo makampuni ya kuchimba madini yamefunga migodi wakati mengine yakiendelea kuchimba madini na kutengeneza faida,

6. 75% ya watanzania sisi ni wakulima na ni wazalishaji mazao ya kilimo lakini ndio tunaongoza kwa umasikini (60%) ya masikini wa tanzania ni wakulima lakini kilimo hicho hicho ndicho kinawafanya wengine wang'are ktk anga za kimataifa wakitokea hapa tanzania,

MY TAKE
watu kukosa kufanikiwa kwenye jambo fulani iwe kilimo, biashara, ajira, ujasiriamali, teknolojia ama elimu does not guarantee kuwa hicho kitu ni kibaya na kamali! Kamali siku zote has no accepted body of knowledge u can get from school! Jambo lolote ambalo linahitaji kwanza maarifa na elimu ili ulifanye hilo jambo si la kubeza wala haliwezi kuwa kamari,

Sijui deeply kuhusu kutrade forex but mafanikio kwenye jambo lolote ni kitu ambacho hakina guarantee!!!

NI AJABU SANA KUSEMA KUWA MAFANIKIO AU UTAJIRI UPO KWENYE UZALISHAJI MALI AU UTOAJI HUDUMA ILIHALI WAPO WANAOZALISHA MALI NA KUTOA HUDUMA NA BADO WANAFELI KUPATA MAFANIKIO MIFANO IPO HAPO JUU!
 
Point
 
Forex ni kamari, na unapomshawishi mtu akacheze kamari ili upate comission na broker fee huo ndio utapeli wenyewe. Solution ni kufanya kazi za uzalishaji mali/ huduma, hakuna shortcut. Zingine ulizosema hapo ni 'senseless rubbish'.
Na kama forex ni kamari concetrate kwenye kutueleza tusiofahamu ni kwa namna gani hiyo forex ni kamari na ni kivipi kamari hii imefanikiwa kupata mitaala mavyuoni utakuwa umetusaidia wengi,

Tuelimishe from the scratch na tuambie ni kipi kinafichwa na hawa watetezi wa forex ambacho ndicho kinaonesha ni kamari kiasi kwamba akisoma mtu ambae hajui chochote aweze kupata mawazo ya pande mbili na ayaainishe na kujua ukweli,

Mfano, tuambie ni taarifa zipi ambazo wanaochelea forex wamezificha na ni za hatari ila hawataki tuzijue,

Andika maandishi yanayojitosheleza kama walivyofanya wale wanaochelea forex kama akina Ontario na wengine.

Mimi nilichojifunza hapa ni kwamba wanaochelea forex wanatoa maelezo ya kujitosheleza na mifano hai na rejea kuliko wale wanaosema kuwa forex ni kamari, ninejaribu kufuatilia kwa kina ili kupata maelezo ya kutosha nijiridhishe kuwa ni kamari ila hadi sasa naona vipande vipande tu na maandishi ya kuwapinga watoa maada na sio naandishi ya kuonesha kuwa ni kamari

Una lengo zuri la kuwataka watu wasijihusishe na kamari lakini hujui hata hiyo kamari ni nini kiasi kwamba unaweza kutueleza sisi tusioijua hiyo kamari.

1. Why wanaosema forex sio kamari wana maelezo na mifano ya kujitosheleza kuliko wanaosema ni kamari?

2. Why wanaosema forex ni kamari hadi sasa hawaanziasha uzi wa kutuelezea ni kwa namna gani forex ni kamri ili nasi tupate kujinasua maana tunaendelea kushawishika?

My Take

Anzisha uzi maalum kutuelimisha kuwani kwa namna ipi forex kuwa ni kamari na akina nani wanachezesha hii kamari, hii kamari imefanikiwaje kupata mitaala vyuoni, kwa nini kamari hii inahitaji usome na ina vitabu kibao mbona hatuoni vitabu vya kamari zingine ambazo inafananishwa nazo? Why this tu?
 
Swadakta kabisa umenena vyema
 
Uko vizuri sana chief
 
Ndo mana sisi kuendelea ni kazi sana mtu anaponda kitu asichokijua anaropoka tu...
 
Anakwambia ana miezi isiyozidi minne.
Yani bila Ontario kuandika kuhusu Forex sijui kama Jamaa alikua yuko aware.

Cha ajabu sasa, anasema eti watu walikua wanamuomba sana aandike kuhusu Forex.
Kwamba yeye Ndio mtabe, wanamtegemea.
Kubabake walay!!!!
[emoji86] [emoji86]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…