Nguvu yetu ipo katika umoja wetu, tukumbushane hili tunapoikaribia miaka 60 ya uhai wa taifa letu

Nguvu yetu ipo katika umoja wetu, tukumbushane hili tunapoikaribia miaka 60 ya uhai wa taifa letu

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Tarehe 9 mwezi wa kumi na mbili mwaka huu inatimia miaka 60 ya uhuru wetu. Itakuwa ni siku maalum yenye kila sababu ya kupambwa na nyimbo za furaha na zenye kukumbusha maana pana ya uhuru wetu.

Ni lazima tukumbushane kuwa umri huu tunaoufikia mwaka huu haujaweza tu kwa bahati kuweza kufikiwa, tukiwa ni nchi yenye makabila zaidi ya 120 tumeweza kuendelea kujitanguliza katika utanzania kabla ya kutanguliza makabila na dini zetu.

Ni lazima tuwaenzi viongozi wenye maono kama Hayati Julius Nyerere na Mzee Karume na wengine wote waliofanya kazi nzito ya kuunganisha watu na kukumbusha juu ya kutunza ile tabia ya kuvumiliana na kutazamana kama wamoja kabla ya kutanguliza viburi vyetu vya asili.

Tunapoelekea kutimiza miaka 60 ya Tanzania ni bora tukakumbushana maana ya uwepo wa viongozi wa dini wakati wa shughuli za kiserikali, wale wanasimamia umoja wetu. Tunapoyasikia maombi ya shekhe, yakafuatiwa na yale askofu au yule kiongozi wa wahindu, tunakumbushwa maana ya kuvumiliana, maana ya kuchukuliana kindugu licha ya wingi wa tofauti tunazoishi nazo.

Na kuvumiliana kuna maana pana zaidi, ni ule uwezo wa kumkubali mwenzako hata kama huamini katika imani yake. Ni ule uwezo wa kuvumilia vipindi vya dini vinavyorushwa runingani hata kama hukubaliani kiimani na kile kinachohubiriwa. Siku hizi kuna neno utangamano (compatibility), lenye kumaanisha uwezo wa watu kuishi pamoja na kutengeneza jamii moja. Unaingia ndani ya basi unakutana na wamasai, wagogo, wasambaa, wazinza na wazigua wakiongea kiswahili na wakijadiliana maswali ya kitaifa.

Ni vyema tukawakumbusha watanzania wenzetu haswa wale wenye umri mdogo juu ya umuhimu wa kuvumiliana, umuhimu wa kutozitangulia zile jeuri zetu za asili (prejudices) kama tunataka kuona Tanzania siku moja inasherehekea miaka 100 ya uhai wake. Kuna wanaojenga hoja kwamba maadam wanalipa kodi basi hata vipindi fulani vya dini visipewe kipaumbele siku za ijumaa na jumapili, hii ni hoja yenye kwenda kinyume na msingi wa kuvumiliana.

Tajiri kama RIP Subhash Patel kodi aliyokuwa anailipa kwa mwezi mmoja tu ni nyingi kulinganisha na ile inayolipwa na watanzania wengi kwa maisha yao yote, alikuwa ni mhindu, hivyo wahindu wasipewe haki ya kuwa na uhuru wa kuabudu na vipindi vya dini visiwepo radioni kisa mtu au watu fulani wanaona kama haviwahusu?.

Tunapokaribia kutimiza miaka 60 ya uhai wetu na uwe ni wajibu wa wote wenye kufahamu faida za kuvumiliana kitaifa kuingia kazini kwa nguvu zao zote ili waweze kuwapa elimu watanzania wa vizazi vya sasa juu ya suala zima la kukwepa aina zote za fikra zinazozaa ubaguzi na udhaifu wa utaifa.

Kuna mataifa mengi maarufu ambayo kwa nje yanayoonekana kuwa ni imara lakini kwa ndani utaifa wao ni teketeke sana. Wanatazamana kiukabila na kimaeneo na msingi wa udhaifu wa utaifa wao ni kutokukubaliana na hoja za kuvumiliana.

Mungu aibariki Tanzania ili wengi wetu tuweze kuuelewa ujumbe alioujenga Mwalimu Nyerere kwa muda mwingi wa uhai wake, ujumbe wa kupiga vita ukaburu wa kule afrika ya kusini na ukaburu kwa maana ya mawazo ya uzawa wenye kuzaa usisi.

Mungu ni mwema na aendelee kulitunza taifa hili.
 
Ivi ni Kwa nini Uhuru wa Tanganyika ndio huitwa Uhuru wa Tanzania? na sio ule wa Zanzibar?
Kwa nini usiifanye sku ya Muungano kuwa ndiyo siku Muhimu kwa Tanzania badala ya Dec 9.?

nashauri
Siku ya Uhuru wa Tanganyika iitwe Tanganyika Day.
Siku ya mapinduzi ya Zanziba iitwe Mapinduzi Day
Siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iitwe Tanzania day
Pasiwepi kabisa siku inayoitwa Uhuru wa Tanzania, maana haipo.
 
Ivi ni Kwa nini Uhuru wa Tanganyika ndio huitwa Uhuru wa Tanzania? na sio ule wa Zanzibar?
Kwa nini usiifanye sku ya Muungano kuwa ndiyo siku Muhimu kwa Tanzania badala ya Dec 9?...
Mawazo yako ni mazuri lakini yanaweza kuchangia katika kudhoofisha utaifa. Ni jamhuri ya muungano wa Tanzania, ukianza kutenga hizo siku maalum zikawa ni nyingi unaua Utanzania.
 
Mawazo yako ni mazuri lakini yanaweza kuchangia katika kudhoofisha utaifa. Ni jamhuri ya muungano wa Tanzania, ukianza kutenga hizo siku maalum zikawa ni nyingi unaua Utanzania.
Hamna lolote zaidi ni hofu isiyo na maana yoyote.
 
Ivi ni Kwa nini Uhuru wa Tanganyika ndio huitwa Uhuru wa Tanzania? na sio ule wa Zanzibar?
Kwa nini usiifanye sku ya Muungano kuwa ndiyo siku Muhimu kwa Tanzania badala ya Dec 9.?

nashauri
Siku ya Uhuru wa Tanganyika iitwe Tanganyika Day.
Siku ya mapinduzi ya Zanziba iitwe Mapinduzi Day
Siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iitwe Tanzania day
Pasiwepi kabisa siku inayoitwa Uhuru wa Tanzania, maana haipo.
Wanaosema Uhuru wa Tanzania, ni kutokana na kuvimbiwa ugali wa mahindi
 
Vipindi vyote vya dini visipewe jukwaa katika vyombo vya habari vya kitaifa kama TBC .Sio vipindi fulani tu. Dini zina vyombo vyake vya habari na zinaweza kulipia vipindi katika vyombo vya habari binafsi.
 
Zanzibar wana serikali yao ya mapinduzi tuambie umoja wa kitaifa unakujaje wakati huo kuna serikali mbili
 
Tarehe 9 mwezi wa kumi na mbili mwaka huu inatimia miaka 60 ya uhuru wetu. Itakuwa ni siku maalum yenye kila sababu ya kupambwa na nyimbo za furaha na zenye kukumbusha maana pana ya uhuru wetu...
You are very suitable! These are things people need to discuss. Some people don't understand the history of this country, where we came from and where we should be. These days people are driven by what they see virtually.
 
Mwaka 1884 hadi 1885 wakoloni mabeberu wa kizungu walikaa huko Berlin wakagawana bara la Africa kulingana na vigezo mbalimbali.
Lakini kikubwa ilikuwa ni kuwahi eneo/kuwa wa kwanza kufika katika eneo fulani na kuwa na uwezo wa kulitawala na kulitiisha hilo eno.
Ndio sababu unaona mipaka mingi ya mataifa ya Africa imenyooka kama imechorwa na rula na unaweza kukuta kabila moja likiwa katika nchi mbili au tatu tofauti.Mataifa yetu yalagawanywa mezani kama keki ya birthday.

Kwa vigezo hivyo eneo letu lilioitwa Tanganyika liliangukia mikononi mwa Wajerumani na Zanzibar chini ya Uingereza huku Sultan akiachiwa kuwa mtawala wake. Baadaye 1920 tukawekwa chini ya Uingereza .

Mwaka 1961 Tulikabadhiwa uhuru Tanganyika na Waingereza na 1964 Zanzibar ikafanya mapinduzi kumuondoa Sultan mwaka huo huo 1964 Nyerere na Karume wakaunganisha haya mataifa mawili kuwa Tanzania tuliyo nayo leo.
You are very suitable! These are things people need to discuss. Some people don't understand the history of this country, where we came from and where we should be. These days people are driven by what they see virtually.
 
Ivi ni Kwa nini Uhuru wa Tanganyika ndio huitwa Uhuru wa Tanzania? na sio ule wa Zanzibar?
Kwa nini usiifanye sku ya Muungano kuwa ndiyo siku Muhimu kwa Tanzania badala ya Dec 9.?...
Uko sahihi kabisa. Lakini mwana CCM hawezi kukuelewa. Hawapendi watu welevu. Kipindi kile cha mwendazake ungeambiwa huna uzalendo na una lengo la kuvunja muungano. Ulichoandika hapo ndiyo ukweli wenyewe hata kama haupendezi kwa wana CCM.
 
Mawazo yako ni mazuri lakini yanaweza kuchangia katika kudhoofisha utaifa. Ni jamhuri ya muungano wa Tanzania, ukianza kutenga hizo siku maalum zikawa ni nyingi unaua Utanzania.
Tanzania gani iliyopata uhuru tarehe 9 December 1961. Hakukua na hilo jina. Limelazimishwa liwepo kabla ya muda lilipopatikana na watanzania tumekubali.
 
Back
Top Bottom