NHIF itafilisika, masikini hawekewi bima

NHIF itafilisika, masikini hawekewi bima

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Watu wetu wengi ni maskini sana na wajinga wasiofuata kanuni za afya kujilinda dhidi ya maradhi. Nchi haina maji, umeme, barabara, chakula na nyumba Bora za kuishi toshelezi kumudu kupambana na maambukizi. Elimu ya afya na huduma za afya haziwafikii watu wote.

Watu wetu wanazo tabia nyingi mno ambazo ni hatarishi kwa afya zao zinazowafanya waugue wakati wowote na kuhitaji kutibiwa.

Huwezi kumuwekea bima ya afya mtu ambae Hana maji safi, umeme, chakula, choo Wala chandarua. Huwezi kumuwekea bima mtu ambae anapanda pikipiki bila kuvaa helmet, havai viatu, aña chumba kimoja yeye na watoto na mifugo yake, asiyetumia condom, choo, kunawa mikono, nk. Watu wa aina hii wanaugua familia nzima kila siku na kuhitaji matibabu ya kila siku na kila wakati kwenye hospitali tofauti tofauti.

Serikali lazimà ipunguze umaskini, itoe elimu ya afya na iboreshe maisha ya wananchi ili wasiugue mara kwa mara kabla ya kupanua wigo wa wadau wa NHIF, vinginevyo mfuko uta collapse.

Maskini hawekewi bima
 
Umesema vema
Mkuu usijaribu kuingia kwenye kikundi cha kufa na kuzikana chenye watu maskini utafirisika kwa michango, Watu hawa utasikia mara anahaarisha na kutapika, mara mtoto kaungua na uji jikoni, mara ana malaria, minyoo, kipindupindu, anabanwa kifua, nk kafa au amelazwa hospital mumchangie, mumsafirishe, nk
 
Mkuu usijaribu kuingia kwenye kikundi cha kufa na kuzikana chenye watu maskini utafirisika kwa michango, Watu hawa utasikia mara anahaarisha na kutapika, mara mtoto kaungua na uji jikoni, mara ana malaria, minyoo, kipindupindu, anabanwa kifua, nk kafa au amelazwa hospital mumchangie, mumsafirishe, nk
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Watu wetu wengi ni maskini sana, wajinga wasiofuata kanuni za afya kujilinda na maradhi. Nchi haina maji, umeme, barabara, chakula na nyumba Bora za kuishi toshelezi. Elimu ya afya haiwafikii watu wote...
Hela tunazo katwa kila monthly unadhani ni zakununulia vyuma chakavu? Mimi nakatwa hela kila mwezi lakini ninamwaka wa 6 sijaenda hospital hata kuchukua Panado hiyo hela yangu inafanya kazi gani? Wacha ikatibie maskini wengine
 
Watu wetu wengi ni maskini sana, wajinga wasiofuata kanuni za afya kujilinda na maradhi. Nchi haina maji, umeme, barabara, chakula na nyumba Bora za kuishi toshelezi. Elimu ya afya haiwafikii watu wote...
NHIF kitu wanachofanya kwa UFANISI zaidi Ni KUJILIPA MISHAHARA MIKUBWA, KUTAFUTA sana MAKOSA ili WASILIPE PESA na KUKOMOW Wanachama WAKE.

NHIF Ni TAKATAKA KABISA.

Sasa hivi Watoa Huduma walikuona una Kadi ya NHIF wanakuona Kama uchafu.

Na huwa nashangaa sana NHIF na iCHF bado ujinga, halafu Kuna Genge la VILAZA eti linahadili BIMA KWA WOTE.
 
Watu wetu wengi ni maskini sana, wajinga wasiofuata kanuni za afya kujilinda na maradhi. Nchi haina maji, umeme, barabara, chakula na nyumba Bora za kuishi toshelezi. Elimu ya afya haiwafikii watu wote...
Shida ipo hapa, serikali inang'ang'ania wafanyakazi wake wawe wanachama wa NHIF.

Watumishi wa umma waamue shirika la bima wachangie makato yao, ni wachache sana wangechagua NHIF. Mfuko umejaa ujinga
 
Hela tunazo katwa kila monthly unadhani ni zakununulia vyuma chakavu? Mimi nakatwa hela kila mwezi lakini ninamwaka wa 6 sijaenda hospital hata kuchukua Panado hiyo hela yangu inafanya kazi gani? Wacha ikatibie maskini wengine
Hela yako Kuna inatumiwa na maskini wasiokula matunda, wasionawa mikono baada ya choo, wasiolala kwenye vyandarua, bodaboda wasiokuwa na leseni wasiovaa helmet, wagonjwa wa TB, HIV, BP, kisukari ambao idadi Yao inazidi kuongezeka.
 
Watu wetu wengi ni maskini sana, wajinga wasiofuata kanuni za afya kujilinda na maradhi. Nchi haina maji, umeme, barabara, chakula na nyumba Bora za kuishi toshelezi. Elimu ya afya haiwafikii watu wote...
Serikali itengeneze ajira za viwandani,badala ya kuwa na ma halmashauri,mikoa,mashirika kibao yasio zalisha kitu,serikali inunue tekinolojia ya kilimo,ufugsji tuuze mazao Afrika nzima,tuwe na mradi wa kulima wa kisasa kama Ukraine,kiasi kwamba tufikie tuilishe Afrika nzima.

Tutengeneze,piki piki,bajaji,bettey,taa za majumbani,ifikie mahali hatuagizi zao lolote kutoka nje,sukari,mafuta,matairi ya magari,viti vya maofisini,
 
Watu wetu wengi ni maskini sana, wajinga wasiofuata kanuni za afya kujilinda na maradhi. Nchi haina maji, umeme, barabara, chakula na nyumba Bora za kuishi toshelezi. Elimu ya afya haiwafikii watu wote...
Very well said. 👌👌
Nadhani hatuhitaji kuwa na uchumi mkubwa au mzuri sana. Kitu kikubwa ni ufahamu wa kuishi kwa kulinda afya zetu.

Nilishuhudia bibi yangu kijijini akiishi maisha ya kuilinda afya yake kwa mazingira yanayomzunguka.
1: Kunywa maji yaliyochemshwa.

2: Kutokuchanganya vyombo vya chakula na kufuria, au vya bafuni na kuchotea maji ya kunywa, au chooni na matumizi ya kawaida.

3: Mazingira safi.

4: Matumizi ya chandarua

5: .....👇

Suala kubwa ni kufanya preventive/kuzuia approach iwe kubwa kuliko subiri uumwe ili tutibu. Kujielekeza kubadili mentality zinazoeneza magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza, haya ya lishe ndo yatahitaji kuingia mfukoni sana.
 
Watu wetu wengi ni maskini sana, wajinga wasiofuata kanuni za afya kujilinda na maradhi. Nchi haina maji, umeme, barabara, chakula na nyumba Bora za kuishi toshelezi. Elimu ya afya haiwafikii watu wote.

Watu wetu wanazo tabia nyingi mno ambazo ni hatarishi kwa afya zao zinazowafanya waugue wakati wowote na kuhitaji kutibiwa.

Huwezi kumuwekea bima ya afya mtu ambae Hana maji safi, umeme, chakula, choo Wala chandarua. Huwezi kumuwekea bima mtu ambae anapanda pikipiki bila kuvaa helmet, havai viatu, aña chumba kimoja yeye na watoto na mifugo yake, asiyetumia condom, choo, kunawa mikono, nk. Watu wa aina hii wanaugua familia nzima kila siku na kuhitaji matibabu ya kila siku na kila wakati kwenye hospitali tofauti tofauti.

Serikali lazimà ipunguze umaskini, itoe elimu ya afya na iboreshe maisha ya wananchi ili wasiugue mara kwa mara kabla ya kupanua wigo wa wadau wa NHIF, vinginevyo mfuko uta collapse.

Maskini hawekewi bima
📌📌📌
 
Mkuu usijaribu kuingia kwenye kikundi cha kufa na kuzikana chenye watu maskini utafirisika kwa michango, Watu hawa utasikia mara anahaarisha na kutapika, mara mtoto kaungua na uji jikoni, mara ana malaria, minyoo, kipindupindu, anabanwa kifua, nk kafa au amelazwa hospital mumchangie, mumsafirishe, nk
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Serikali itengeneze ajira za viwandani,badala ya kuwa na ma halmashauri,mikoa,mashirika kibao yasio zalisha kitu,serikali inunue tekinolojia ya kilimo,ufugsji tuuze mazao Afrika nzima,tuwe na mradi wa kulima wa kisasa kama Ukraine,kiasi kwamba tufikie tuilishe Afrika nzima,
Tutengeneze,piki piki,bajaji,bettey,taa za majumbani,ifikie mahali hatuagizi zao lolote kutoka nje,sukari,mafuta,matairi ya magari,viti vya maofisini,
Huo ndio ukweli wenyewe. Tanzania ina watu tegemezi wengi sana. Wanaofanya kazi ni 10% tu ya watu wote. Ndio maaana rushwa haiishi hata uongeze vipi mshahara kwa watumishi, maana 90% (extended families, jamaa na marafiki) ya watu wanahitaji kupewa mahitaji na hawa 10% Dawa ni kuboreaha hali za watu wote.
 
Back
Top Bottom