MDAU TZ
Member
- Jun 9, 2023
- 12
- 53
HUZUNI KUBWA.
---
Tafadhali rejea somo tajwa hapo juu
2. Mfuko husajili vituo vya kutolea huduma za afya kuwawezesha wanufaika wake kupata huduma hizo nchi nzima. Hadi sasa Mfuko umesajili jumla ya vituo 9,920 vya kutolea huduma za afya kuanzia ngazi ya Zahanati hadi ngazi ya Hospitali ya Taifa ya Rufaa kwa umiliki wa Serikali, Binafsi na Madhehebu ya Dini.
3. Miongoni mwa vituo ambavyo Mfuko umesajili vinamilikiwa na Taasisi ya Aga Khan vinavyojumuisha Hospitali ya Aga Khan Dar es Salaam na Kliniki zilizoko katika maeneo mbalimbali nchini. Hivi karibuni, Mfuko umepokea taarifa kutoka Taasisi ya Aga Khan kuwa imekusudia kutokuendelea na mkataba kati yake na Mfuko kwa vituo 11 kati ya 24 nchini ikiwemo hospitali ya Aga Khan Dar es salaam kwa sababu ya changamoto za kiuendeshaji.
4. Wakati majadiliano na mtoa huduma yakiendelea na kuepusha usumbufu kwa wanachama wake, Mfuko unatoa taarifa kuwa, kuanzia tarehe 14 Agosti 2024 utasitisha huduma katika vituo vya Aga Khan nchini. Katika kuhakikisha mwendelezo wa huduma kwa wanufaika wake hususan waliokuwa wanapata huduma katika hospitali ya Aga Khan Dar es Salaam Mfuko umefanya makubaliano na kituo hicho ambapo:-
. Wajawazito wanaohudhuria kliniki katika hospitali ya Aga Khan ambao wametimiza majuma 35 wataendelea kupata huduma katika hospitali hiyo hadi watakapojifungua na kuruhusiwa. Kuhusu wajawazito ambao hawajatimiza majuma 35 wanashauriwa kutumia vituo mbadala vilivyosajiliwa na Mfuko ambapo pia baadhi ya madaktari katika vituo hivyo walikuwa wanawahudumia wakiwa Aga Khan;
Wagonjwa watakaokuwa wamelazwa kufikia tarehe 13 Agosti 2024 wataendelea kupata huduma katika hospitali ya Aga Khan hadi watakapopata nafuu na kuruhusiwa;
. Wagonjwa wengine wote wakiwemo wa kliniki za saratani na kusafisha damu (dialysis) watapata huduma katika vituo vingine vilivyosajiliwa na Mfuko. Tayari Mfuko umewasiliana na wagonjwa wa kliniki ya kusafisha damu na kuwahamishia kupata huduma hiyo katika vituo vilivyopendekezwa kwao;
5. Aidha, Mfuko umesajili vituo vingine vyenye hadhi sawa au zaidi ya hospitali Aga Khan Dar es Salaam ambavyo ni Saifee Hospital na Shifaa Pan African Hospital vyote vilivyo jijini Dar es Salaam. Vilevile wanachama pamoja na wategemezi wao wanaweza kupata huduma za haraka katika vituo vingine vikiwemo vituo vikubwa kama Hospitali ya Taifa Muhimbili, Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu Muhimbili (MOI) na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI). Kwa mikoa mingine, Mfuko umehakikisha kuna vituo vilivyosajiliwa katika maeneo jirani kumhakikishia mwanachama huduma bila usumbufu.
6. Hivyo kwa barua hii, Mfuko unawaomba kuwataarifu wafanyakazi kutumia vituo mbadala kwa ajili ya kupata huduma za matibabu kuanzia tarehe 14 Agosti 2024. Maofisa wa Mfuko katika kitengo cha wateja wakubwa pamoja na ofisi zake nchi nzima wako tayari kutoa usaidizi kwa wanachama kuhakikisha wanapata huduma kikamilifu bila usumbufu katika kipindi cha mpito.
7. Tunakushukuru kwa ushirikiano wako
===
---
YAH: TAARIFA KUHUSU KUSITISHA HUDUMA KWA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA VYA AGA KHAN
Tafadhali rejea somo tajwa hapo juu
2. Mfuko husajili vituo vya kutolea huduma za afya kuwawezesha wanufaika wake kupata huduma hizo nchi nzima. Hadi sasa Mfuko umesajili jumla ya vituo 9,920 vya kutolea huduma za afya kuanzia ngazi ya Zahanati hadi ngazi ya Hospitali ya Taifa ya Rufaa kwa umiliki wa Serikali, Binafsi na Madhehebu ya Dini.
3. Miongoni mwa vituo ambavyo Mfuko umesajili vinamilikiwa na Taasisi ya Aga Khan vinavyojumuisha Hospitali ya Aga Khan Dar es Salaam na Kliniki zilizoko katika maeneo mbalimbali nchini. Hivi karibuni, Mfuko umepokea taarifa kutoka Taasisi ya Aga Khan kuwa imekusudia kutokuendelea na mkataba kati yake na Mfuko kwa vituo 11 kati ya 24 nchini ikiwemo hospitali ya Aga Khan Dar es salaam kwa sababu ya changamoto za kiuendeshaji.
4. Wakati majadiliano na mtoa huduma yakiendelea na kuepusha usumbufu kwa wanachama wake, Mfuko unatoa taarifa kuwa, kuanzia tarehe 14 Agosti 2024 utasitisha huduma katika vituo vya Aga Khan nchini. Katika kuhakikisha mwendelezo wa huduma kwa wanufaika wake hususan waliokuwa wanapata huduma katika hospitali ya Aga Khan Dar es Salaam Mfuko umefanya makubaliano na kituo hicho ambapo:-
. Wajawazito wanaohudhuria kliniki katika hospitali ya Aga Khan ambao wametimiza majuma 35 wataendelea kupata huduma katika hospitali hiyo hadi watakapojifungua na kuruhusiwa. Kuhusu wajawazito ambao hawajatimiza majuma 35 wanashauriwa kutumia vituo mbadala vilivyosajiliwa na Mfuko ambapo pia baadhi ya madaktari katika vituo hivyo walikuwa wanawahudumia wakiwa Aga Khan;
Wagonjwa watakaokuwa wamelazwa kufikia tarehe 13 Agosti 2024 wataendelea kupata huduma katika hospitali ya Aga Khan hadi watakapopata nafuu na kuruhusiwa;
. Wagonjwa wengine wote wakiwemo wa kliniki za saratani na kusafisha damu (dialysis) watapata huduma katika vituo vingine vilivyosajiliwa na Mfuko. Tayari Mfuko umewasiliana na wagonjwa wa kliniki ya kusafisha damu na kuwahamishia kupata huduma hiyo katika vituo vilivyopendekezwa kwao;
5. Aidha, Mfuko umesajili vituo vingine vyenye hadhi sawa au zaidi ya hospitali Aga Khan Dar es Salaam ambavyo ni Saifee Hospital na Shifaa Pan African Hospital vyote vilivyo jijini Dar es Salaam. Vilevile wanachama pamoja na wategemezi wao wanaweza kupata huduma za haraka katika vituo vingine vikiwemo vituo vikubwa kama Hospitali ya Taifa Muhimbili, Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu Muhimbili (MOI) na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI). Kwa mikoa mingine, Mfuko umehakikisha kuna vituo vilivyosajiliwa katika maeneo jirani kumhakikishia mwanachama huduma bila usumbufu.
6. Hivyo kwa barua hii, Mfuko unawaomba kuwataarifu wafanyakazi kutumia vituo mbadala kwa ajili ya kupata huduma za matibabu kuanzia tarehe 14 Agosti 2024. Maofisa wa Mfuko katika kitengo cha wateja wakubwa pamoja na ofisi zake nchi nzima wako tayari kutoa usaidizi kwa wanachama kuhakikisha wanapata huduma kikamilifu bila usumbufu katika kipindi cha mpito.
7. Tunakushukuru kwa ushirikiano wako