Ni afadhali mwanaume kuwa na Ghubu kuliko mwanamke….!

Kwauelewa wangu mdogo, ghubu ni hali ya mtu kuwa na kisirani, hasira, kununanuna hata kama mmekosana ndani hasamei, mataongea mtamaliza lakiani ikitokea mmekorofishana tena lazima atakumbushia makosa yale ya nyuma, siku ile ulifanya hivi, ck ile tena ukafanya vile, yaani sijui nielezeje ni mtu wa kunung'unikanung'uka tu, Mtambuzi ataelezea vizuri

Tuambieni jamani, hilo ghubu ni nini? mtoa mada tufafanulie basi
u
 
Baba hapa mwanao ntakuomba radhi nipingane nawe tu.....Ghubu la mume! utende jema, ghubu, uiname ghubu, ugeuke ghubu..............usiombee kukutwa.
Kuna wanawake wengine bila kuwa na GHUBU japo kidogo ndoa hainogi kabisaaaaaa.............Kama vile Mboga bila chumvi..............LOL

 
Ghubu si jema hata kidogo iwe ni mume au mke na hayatakuwa mapenzi bali karaha, ila linaposimama kwa mtoto ni kheri ya ghubu la kiume kuliko la kike maana mama ndiye mwenye kuwa na mtoto huyo kwa muda mwingi zaidi ya baba
 

Mtambuzi ni kheli mwanamke mwenye gubu, kuliko mwanaume. Husiombe ukutane na mwanaume mwenye gubu kha!!! utajuta, maana baadhi ya wanawake ni kawaida sana kulalamika, gubu na ulalamishi vinaendana. Mwanaume anayelalamika, lalamika ni kero haswa, ebu fikiria upo nyumbani na marafiki zako wewe mwanamke mume wako anatoka kazini/kwenye mihangaiko yake anakuta labda umembadilisha mtoto pampers, akaikuta hapo chini, haukuwa umeiacha makusudi labda ndo tu umetoka kuitoa, ile kuiona tu anaanza, we mwanamke haya makitu ya mtoto unayaacha, acha hapa kwa sababu gani? Au dada kwa nini huwa mnakuwa wachafu hivi mna acha, acha vitu hovyo, lakini kwa mwanamke kuulizia kwa nini hiyo kitu ipo hapo chini ni sawa kabisa kwa maana ni jukumu la mwanamke kuangalia usafi wa nyumbani japo itakuwa ni gubu ila itaonekana tu kwamba ni moja ya majukumu, nimetoa mfano huu sababu mtu mwenye gubu huwa hachagui kitu cha kuongea, na ni wakati gani wa kuongea, kila kitu yeye kwake ni kibaya yaani ni kero tu, afadhali mwanamke awe na gubu maana bwana anaweza kumbadilisha si unajua wanawake huwa ni wepesi wa kutii, ila baba akiwa na gubu, mama yangu!!! Si ndo mama na watoto wakimwona tu kila mtu anatafuta mahali pa kutokea ili hasikumbane na dhahama za jamaa.
 
Afadhali na wewe umeuliza maana watu wana arrogance ya ajabu sana humu. Swali limeulizwa kwa nia njema lakini hakuna hata aliyejibu - wanaliruka tu.

Ukiona hivyo ujue huenda na wao hata hawajui.....

Hata wewe hujui hee!
 

Cjui 2tumwelewe yupi hapa maana hapo juu kuna mwingine kaelezea tofauti kabisa
 
Sijui kama mi ndo sijaelewa hapa ghubu linalosemwa ni mke kwa mme au ni mmoja wa wazazi kwa mtoto, mwongotho tasavali.
 
Ghubu si mchezo, hasa kwa mwanamme.

kongosho aksante.

Kuna wanawake wengine bila kuwa na GHUBU japo kidogo ndoa hainogi kabisaaaaaa.............Kama vile Mboga bila chumvi..............LOL

Labda kama unazungumzia wivu Baba yangu but wivu!? utajuta kuzaliwa mtoto wa kike.

Aksante ram................... mie leo nbi kushkuru tu maana nilishajaaliwa kuwa victim wa hili.
 
kongosho aksante.


Labda kama unazungumzia wivu Baba yangu but wivu!? utajuta kuzaliwa mtoto wa kike.


Aksante ram................... mie leo nbi kushkuru tu maana nilishajaaliwa kuwa victim wa hili.
Niliyajua hayo na ndio maana sikudai hata mahari yangu...............LOL
 
Niliyajua hayo na ndio maana sikudai hata mahari yangu...............LOL

Hahahah aksante Baba yangu kweli uliona mbali ndo mana wanasema alotangulia kuliona jua duniani kakuzidi mengi. Nakushukuru kwa hili maana kama na mahari angelipa sijui ningetolewa mlango gani yarabi mie! Maana bila ya mahari tu nlikiona cha mtema kuni, na mahari si ndo ingekuwa soko la watumwa Kilwa masoko!
 
Naona umeanza kujifunza nahau zangu.....................LOL
 
Kuna wanawake wengine bila kuwa na GHUBU japo kidogo ndoa hainogi kabisaaaaaa.............Kama vile Mboga bila chumvi..............LOL

ok........................................
 
aisee hata kama gubu linadumisha ndoa lakini likizidi mmh! inakera,mimi ilinishinda bwana nikasepa mapemaaa!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…