Ni aibu Hospitali za Kanda Kukosa MRI

Ni aibu Hospitali za Kanda Kukosa MRI

Mpingamkoloni

Member
Joined
Feb 14, 2021
Posts
13
Reaction score
33
Asubuhi hii niko Idodomya. Nilitumwa na daktari wa Hospitali ya rufaa Mbeya kuja kufanya MRI. Alinipa chaguo la kufika Dodoma au Dar es Salaam. Idodomya ni jirani sana kwangu. Ni mwendo wa masaa matatu.

Kinachonihuzunisha sana ni hiki, hivi inakuwaje Hospitali kubwa kama ya Rufaa Mbeya yenye madaktari bingwa kama mia, ikose MRI? Ikose PET scan? Nasikia ndio hospitali kubwa zaidi iliyopo chini ya Wizara ya Afya ambao bado haijaanza kujitegemea.

Naambiwa bei ya MRI na PET vyote havizidi bilioni kumi, na hapo umenunua zile bora zaidi kwenye soko. Na kifaa kinategemea kutumika zaidi ya miaka 10.

Halafu nasikia pia hospitali ya Rufaa Mbeya wana CT Scan moja tu, yaani ikigoma basi hamna kitu tena. Tunazungumzia luku kukosa backup, wakati kwenye afya tunanunua kifaa kimoja kimoja.

Hivi huwa twashindwa nini kujaza vifaa na utaalam kwenye hizi hospitali kubwa za kitaifa? Hivi malengo yetu ni yapi kwanza? Tukumbuke sasa India hakuendeki.
 
E0NhMwdXIAAW0HL.jpeg
 
Mwendazake alituonea saba watu wa Mbeya. Hata barabara kuu ya Iringa-Tunduma aliisitisha ilipofika Igawa Hadi Leo kimya. Hospitali ya Rufaa Mbeya wanategemea watu zaidi ya mil 18,wa mikoa ya Mbeya, songwe, Ruksa, katavi na Njombe, wakati mwingine hadi Iringa .Kwa sass kuna hospitali ya Ifisi Ndio wanaisaida Rufaa baadhi ya idara.

Kuna hospitali ya mkoa haisikiki kabisa. Ila Ndio hivyo mtu akikuchukia ufanye Nini hadi akupende? Bwana Litwaa, jina lake lihimidiwe, Labda nasi tunaonja maendeleo maana saizi naona ubaguzi umepungua. Jiwe alikuwa mfuasi wa apatheid policy.
 
Nadhani watainunua mwaka ujao wa fedha kwa mujibu wa bajeti ya afya.

Ila ni mambo ya kijinga , hospital kama hizo zilitakiwa kuwa fully equipped na kila kifaa but hakuna cha maana wizara wanafanya kuiwezesha hiyo hospital ukilinganisha na hospital zingine za kanda.

Wenzetu wa bugando na kcmc kinachowasidia kuna mikono ya kanisa ,wakati za dar na Ben mkapa Dom zinatazamwa kama za Kitaifa kwa vile ni maeneo viongozi wako mda mwingi.
 
Ni shida sana. Tunadanganywa sana na wanasiasa walioko madarakani kuwa mambo yako vizuri huku ukweli ukiwa kinyume chake...

Huduma za afya hazijafikia kiwango cha ubora unaotakiwa. Tatizo ni vipaumbele ktk allocation ya pesa za wananchi.

Haingii akilini kuona Rais wa nchi akimpa mtu mmoja tu (Rais Mwinyi) eti "zawadi ya birthday" gari aina ya Mercedes Benz lenye thamani ya zaidi ya Tshs. 600,000,000 huku mamilioni ya wananchi masikini wa kipato wakiteseka na wakati mwingine kufa kwa ukosefu wa huduma bora za afya ktk hospitali zetu.

Hebu tu - assume kuwa pesa hii ingelekwa kwa Hospitali hii yenu ya Mbeya, si kwamba ingesaidia sana kuokoa maelfu ya maisha ya watu? Lakini badala yake anapewa mtu mmoja tu tena asiyekuwa na uhitaji nazo.. This is one of the very stupid decision to be made by Samia Suluhu’s prematurely administration!

Hebu tufikiri kwa akili kidogo. Kwamba, Rais Mstaafu Ally Hassan Mwinyi alikuwa anahitaji gari tena tukiambiwa ni "zawadi tu ya birthday" yake kwa gharama ya fedha za walipa kodi?

Mafao yake na marupurupu mengine ambayo sisi walipa kodi tunamlipa kwa heshima ya Utumishi wake anayapeleka wapi? Kwanini asitumie hayo kujinunulia gari analopenda yeye?

Moja ya fyongo aliyoanza kuifanya Rais Samia Suluhu Hassani ni hii. Kumbe ni kweli MADARAKA YANALEVYA SANA.

Lakini kwa akina mama kulewa madaraka huwa ni nadra sana, lakini cha ajabu huyu mama ndani ya siku 60 tu za kutwaa madaraka ya U - Rais kaanza kulewa chakariii kwa ishara ya tendo hili!
 
Tunajenga viwanja vya ndege vya kufugia ng'ombe na taa za barabarani za kuongozea punda wenye mikokoteni lakini tunaacha mambo yenye manufaa na yanayoweza kusaidia watu wengi.

Hakika utawala wa awamu ya 5, ilikuwa ni laana. Tuendelee kuomba Rais Samia aingiwe na hekima ili tupate katiba bora mpya itakayozuia mianya ya kiongozi yeyote kufanya uongozi wa kiharamia.
 
Tuna Ndege tatu tumezilipia, subirini kwanza watu wa Mbeya.
 
Tufanye harambee watu wa Mbeya tuwanunulie hizo machine madaktari wetu. Pesa ndogo sana hiyo tukiamua wenyewe. Kwa mfano tuchange nusu serikali imalizie nusu.

Wananachi inabidi tuonyeshe kukerwa kwa vitendo badala ya kunung'unika mitaani. Hakuna tofauti na wananchi kujitolea kujenga shule na serikali kuchangia mabati.
 
Ukistaajabu ya huko kwenu mbeya basi utayaona ya hospital ya rufaa ya ruvuma. Eti hospital ya rufaa haina ultra sound hivi hawa jamaa wako serious kweli?
 
Kupanga ni kuchagua, tumechagua kununua ndege na kujenga flyovers kwanza.
 
Ni shida sana. Tunadanganywa sana na wanasiasa walioko madarakani kuwa mambo yako vizuri huku ukweli ukiwa kinyume chake...
Na yule dikteta ile billion mia Tano aliyonunulia ndege aina ya Dreamliner, si ilitosha kabisa kununua Mashine za MRI na CT SCAN za kutosha hospital Kama hamsini zile za rufaa
 
Ni shida sana. Tunadanganywa sana na wanasiasa walioko madarakani kuwa mambo yako vizuri huku ukweli ukiwa kinyume chake...
Ile gari thamani yake sio mil. 600 kama ulivyosema. Lakini Bando mama kugawa Hilo gari sio kigezo Cha ugumu wa maisha yetu
 
Back
Top Bottom