Ni aibu sana kwa mwanaume kushindwa kumiliki gari

Huyu siyo JAMES DELICIOUS kweli?,bila shaka ndiwe maana kwa huu uzi sina mashaka kabisa wewe ndiwe
 
Toka nifike Dar miaka ya 2000 nilikuta kuna magari 67893 kati ya hayo magari 10987 yalikuwa ya watu binafsi nikawaza nikinunua gari moja wakati sina nyumba nitasaidia nini nikajenga nyumba sasa hivi wenye magari yao wanalala kwangu na magari yao, wamenipa kodi kesho niaenda kununua Kichwa cha Treni.
 
Naona babu seya kawachanganya sana.
 
Jf imevamiwA na vilaza ,yani mtu na akili zake anaona gari ndo asset ya maana.
 
Duh Tanzania bado sana, mtu badala ya kufikiria kuinvest ili kuweza kuajiri watu kuwa na kiwanda au business kubwa unafikiria kununua Gari. Ukishanunua Gari bado utaendelea kuwa maskini wa kipato. Hiyo mil 5 ni nyingi sana kwa mjasiliamali kuinvest.
 
naomba uninunulie,, utakuwa umenisaidia Sana nisionekane mshamba
 
Kwahiyo ukiwa na gari, umemaliza kilakitu?kuna MTU anazo nyumba za kupanga 6 za milioni 120 kilamoja na anapanda daladala.utasema huyo ni mshamba wa maisha?akili finyu sana.
 
Daahhh upo DSM nini
Maana daahhh ni washamba sna wa maisha
 
Kwahiyo ukiwa na gari, umemaliza kilakitu?kuna MTU anazo nyumba za kupanga 6 za milioni 120 kilamoja na anapanda daladala.utasema huyo ni mshamba wa maisha?akili finyu sana.
huyo atakuwa na pesa za ushirikina
 
acha uongo bahresa tu magari yake yana fika 1000
 
Ukute unajisifu hivyo halafu mwisho wa mwezi unakimbizana na mwenye nyumba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…