Ni ajabu! Account za FB, Instagram na Twitter za Rais Donald Trump wa U.S.A zafungwa kwa muda usiojulikana

Ni ajabu! Account za FB, Instagram na Twitter za Rais Donald Trump wa U.S.A zafungwa kwa muda usiojulikana

Kuvamiwa kwa Bunge na Watu wanne kuuwawa ndiyo demokrasi kumbe? Mbona wakiuwawa huku wahuni kama hao mnapiga kelele?
Hiyo siyo demokrasia, bali ni ujinga kwa sababu unafanywa na "a sitting president" mwenye njia zote za kificho kutekeleza agenda zake chafu...

Mbona John Pombe Magufuli na CCM yake wapo madarakani kwa kuwa "smart enough" kufanya ujinga wao wa wizi wa kura na kujishindisha kwa nguvu hata kuifanya dunia iamini kuwa ni mshindi kweli wakati ukweli ukiwa siyo?

Tatizo la Trump ni nini?

Ni hili: Hawezi kufanya ujinga huo USA labda aje kuwa Rais wa Tanzania....!!

Sina hakika kama umeelewa wewe..
 
Wewe mada imekuzidi uwezo,subiri za level yako ndio ujadili!

Unadhani tatizo ni Marekani au tatizo ni Trump?Unadhani ingekuwa Tanzania,Rais aliyeko madarakani afanye kama anayofanya Trump,nani angeweza kumtoa?Hapo nchi za Africa ndipo zinapaswa kujifunza umuhimu wa kuwa na taasis imara!

Angalia tu hapo Museven anavyobadili katiba kama anavyojisikia ili aendelee kutawala! Hata akishindwa uchaguzi,akagoma kuachia madaraka,nani atamgusa?Vyombo vyote vitamnyenyekea!
Mkuu mbona umeenda mbali kwa Miseven, huku kwenu mkulu anavyoikwepa katiba je
 
"Kila kitu kina mikakati yake ilimradi watu wachache wameona mbele ya siku mbili zinazofuata kabla ya siku hizo kutimia”
 
View attachment 1671159
View attachment 1671498
Sasa ni wazi kabisa Urais wa Donald Trump unaisha kwa aibu na fedheha kubwa...

Kitendo cha kuhamasisha wafuasi wake jana kuvamia jengo la Bunge la Congress (Capitol Hill) ili kuzuia bunge lisifanye kazi yake kumwidhinisha Rais Mteule Joe Biden (D) na makamu wake Kamala Harris ilikuwa ni ishara ya mwisho kuwa huyu mzee ni "mentally unfit" na hafai kukalia kiti cha Urais hata kwa siku 14 zilizobaki...

Sasa kwa sababu ya "uropokaji" wake bila ya kupima madhara ya kauli zake hizo, amefungiwa kutumia mitandao yote mikubwa ya kupashana habari duniani ikiwemo Facebook, Instagram na Twitter...

Inasemekana kwa sasa, yumo kifungoni cha kutopiga wala kupokea simu yoyote kwa yeyote...

Aidha, tayari utaratibu wa kumng'oa White House kabla hata ya tarehe 20/1/2021 siku ya kuapishwa Rais Joe Biden maarufu kama "impeachment" unaandaliwa kwa mujibu wa sheria za Marekani. Na hii ni dharura na itafanyika kwa udharura pia..

Tayari pia mawaziri wengi na maafisa wa taasisi nyeti za serikali kama FBI, CIA nk baadhi wameachia ngazi na wengine wanajiandaa kwa kuwa wamechukizwa na tabia ya Rais Trump isiyojali sheria na katiba ya nchi na hata kuhatarisha usalama wa RAIA na NCHI kwa ujumla..

Naye Makamu wa Rais, Bw. Mike Pence, amechukizwa sana na tabia ya Rais na katika hali ya kushangaza, akasema wazi kuwa, hakubaliani naye....

Na Republicans wenzake wamemtaka kuitisha baraza la mawaziri haraka iwezekanavyo ili kuweka njia ya kumwondoa Donald Trump madarakani kwa kutumia Article 25 ya katiba ya Marekani inayoweka utaratibu wa VP kuchukua madaraka ya Rais iwapo ameshindwa ku - discharge majukumu yake ya Urais kwa sababu zozote zile kabla ya mambo kuharibika zaidi...

Kwa kifupi Wamerekani wamechukizwa sana na kilichotokea jana tendo lililochagizwa na kauli za Rais. Hawatamani hata awe Rais kwa kwa siku mbili zijazo...

For sure kabisa, ni wazi sasa, kuwa Donald Trump hamalizi wiki moja ijayo akiwa Rais wa Marekani...!!
Define "ajabu".

Ame violate terms of services, zinazokataza ku promote violence.

Akafungiwa.

Watu wanaangalia sheria na kanuni.

Hapo ajabu iko wapi?
 
Define "ajabu".

Ame violate terms of services, zinazokataza ku promote violence.

Akafungiwa.

Watu wanaangalia sheria na kanuni.

Hapo ajabu iko wapi?
" Ajabu" yangu ina maana ya "kumbe hata Rais ktk nchi za wenzetu haogopwi, inaangaliwa sheria na sheria hiyo kuchukua mkondo wake..."

Kwetu Afrika hii ni "ajabu" na watu wanashangaa kweli nikiwemo Mimi, maana Afrika Rais daima yuko juu ya sheria...!!
 
Huyu Mzee Trump anaondoka madarakani vibaya.
 
Tanzania is closely monitoring the situation in the United States and have expressed our concern. If matters escalate we will send a peacekeeping force to Washington to restore order and protect 'democracy'.
 
Tanzania is closely monitoring the situation in the United States and have expressed our concern. If matters escalate we will send a peacekeeping force to Washington to restore order and protect 'democracy'.
Hahaaah,
Yote nlipobaki hoi Ni to restore democracy

Umenifurahisha
 
" Ajabu" yangu ina maana ya "kumbe hata Rais ktk nchi za wenzetu haogopwi, inaangaliwa sheria na sheria hiyo kuchukua mkondo wake..."

Kwetu Afrika hii ni "ajabu" na watu wanashangaa kweli nikiwemo Mimi, maana Afrika Rais daima yuko juu ya sheria...!!
Unatakiwa ushangae wanaoweka sheria halafu hawaifuati.

Sio wanaoweka sheria na kuifuata.
 
Mkuu acha kukopi na kupesti.

Ulisikia wapi kahamasisha??

Hivi unajuaga hata kinachoongelewa kweli??
 
Back
Top Bottom