Ni biashara gani unaweza kufanya isiyohitaji uangalizi wa mara kwa mara?

Ni biashara gani unaweza kufanya isiyohitaji uangalizi wa mara kwa mara?

Uuzaji/kubadilisha mitungi ya gesi (ya matumizi majumbani) na vifaa vyake, Pia waweza kuweka plates za kupikia.
View attachment 2014764

Hii biashara usimamizi na hesabu zake sio pasua kichwa, hivyo itakufaa sana hii biashara, na hata kama utaweka mtu wa kusimamia wakati wewe ukiendelea na shughuli zingine zinazokufanya kuwa 'busy'.
Huna uzoefu na biashara bila shaka. Ni hivi: Hata hii gesi bado unaweza kupigwa tena vibaya sana. Kiti mfanyakazi atakachofanya ni ku-replace mitungi anayouza na mitungi yake na faida anachukuwa. Yaani wewe kila ukija unakuta idadi ya mitungi ni sawa ila eg akiuza mitungi 30 kwa siku, anachukuwa faida ya mitungi 20 anaweka mfukoni halafu ana-replace na mitungi mipya na kukuachia faida ya mitungi 10 tu. (of course wewe utadhani ameuza mitungi 10 tu.)
 
Fuga kuku wa kienyeji. Asubuhi unawafungulia wanaenda kupambana kutafuta msosi jioni wanarudi.
 
Kwa nchi za wenzetu inawezekana kufungua biashara alaf unamuachia mtu ana manage wewe unasafiri kwenda kula Bata....ila siyo bongo ambapo kila mtu anayetafuta ajira anatafuta kuiba. Ukimuachia tu mtu umeisha.
 
Kwa nchi za wenzetu inawezekana kufungua biashara alaf unamuachia mtu ana manage wewe unasafiri kwenda kula Bata....ila siyo bongo ambapo kila mtu anayetafuta ajira anatafuta kuiba. Ukimuachia tu mtu umeisha.
Ishu sio Mahali
Haiwezekani Bongo wala huko kwa wenzetu
Ishu ni kwamba unapoamua kufanya biashara ukamweka mtu akusaidie ujue kwamba huyo mtu ana malengo yake anataka kutimiza, hakuna anayetaka kutimiza malengo ya mwenzake na yake yasitimie.
Kama ni wa kiume au wa kike anahitaji kujenga, kuoa/kuolewa, kusomesha, kusaidia nduguze nk

Kwahiyo usipomsimamia kwa ukaribu atatumia mtaji na rasilimali zako kutimiza malengo yake sio yako.
Hata ungekuwa wewe mtu amekuweka dukani unauza milioni 3 kwa siku
Huna nyumba, huna familia, ndugu zako wanakulilia shida, hujui utaenda wapi boss akisema sasa inatosha... ungefanya the same.

Pia binadamu tuna hulka ya ubinafsi, unataka uchukue kwa mwingine uweke kwako that's nature, ndio maana tunasema
Biashara yoyote ili ikue, ni LAZIMA iwe na USIMAMIZI WA KARIBU.
 
Back
Top Bottom