dgombusi
Senior Member
- Sep 3, 2017
- 141
- 200
Kama ndiyo mgeni umefika Kariakoo mara ya kwanza kuna kale ka hofu sijui nitatapeliwa,
Mi mara ya kwanza naenda Kariakoo nilikua natafuta simu nikawa naulizia simu kwenye duka Fulani hivi.
Jamaa alikuwa karibu nalile duka lile kama kijana wa hapo akadakia kuna chimbo simu used hadi elfu 30 tu unapata, Mimi nikaona tiyari fursa hii kumbe mimi ndiyo nilikuwa fursa, tukawa tunaongozana nae kuelekea kunako hilo chimbo.
Ile nageuka kumuaga yule mdada wa kwenye lile duka akaniita kwa ishara nikaenda akaniambia utatapeliwa mimi simjui huyo kijana kwahiyo kuwa makini au tafuta mwenyeji akutafutie.
Hapo ndipo nikakumbuka ule usemi usemao za kuambiwa changanya na maji nikapanda zangu dalala kurudi nyumbani.
Je wewe ulipata changamoto gani ulipokuwa unatafuta chimbo la bidhaa yako Kariakoo kwa mara ya kwanza.
Share nasi
Mi mara ya kwanza naenda Kariakoo nilikua natafuta simu nikawa naulizia simu kwenye duka Fulani hivi.
Jamaa alikuwa karibu nalile duka lile kama kijana wa hapo akadakia kuna chimbo simu used hadi elfu 30 tu unapata, Mimi nikaona tiyari fursa hii kumbe mimi ndiyo nilikuwa fursa, tukawa tunaongozana nae kuelekea kunako hilo chimbo.
Ile nageuka kumuaga yule mdada wa kwenye lile duka akaniita kwa ishara nikaenda akaniambia utatapeliwa mimi simjui huyo kijana kwahiyo kuwa makini au tafuta mwenyeji akutafutie.
Hapo ndipo nikakumbuka ule usemi usemao za kuambiwa changanya na maji nikapanda zangu dalala kurudi nyumbani.
Je wewe ulipata changamoto gani ulipokuwa unatafuta chimbo la bidhaa yako Kariakoo kwa mara ya kwanza.
Share nasi