Ni changamoto zipi zinazikumba car wash za hapa bongo?

Ni changamoto zipi zinazikumba car wash za hapa bongo?

chiziwafursa

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2024
Posts
558
Reaction score
827
Kuna jamaa aliniuliza kuna changamoto gani au kero zinakumbananazo car wash za hapa bongo kwa maana yeye alitaka siku moja aanzishe automated car wash kama hio hapo chini


View: https://youtube.com/shorts/gp6_tX0no50?si=VHD5CWh6KZ_epVth


Nikaona isiwe tabu wacha niulize huku JF labda kuna watu wenye uzoefu kuhusu hili biashara labda naweza pata kitu nikamsanua jamaa

Sasa wadau msiniangushe basi plz!!!!!!!!
 
Kuna jamaa aliniuliza kuna changamoto gani au kero zinakumbananazo car wash za hapa bongo kwa. Maana yeye alitaka siku moja aanzishe automated car wash.kama hio hapo chini


View: https://youtube.com/shorts/gp6_tX0no50?si=VHD5CWh6KZ_epVth





nikaona isiwe tabu wacha niulize huku jf labda kuna watu wenye uzoefu kuhusu hili biashara labda naweza pata kitu nikamsanua jamaa

Sasa wadau msiniangushe basi plz!!!!!!!!

Nishawahi kufanya biashara ya car wash lakini haikuwa automated, biashara yangu ilikufa mwaka jana kipindi cha mgao wa umeme.

Kwahiyo naweza nikasema changamoto ya kwanza ni umeme wa kusuasua, jamaa yako atatakiwa kuwa na nishati mbadala sio kutegemea umeme wa tanesco tu.
 
Nishawahi kufanya biashara ya car wash lakini aikua automated, biashara yangu ilikufa mwaka jana kipindi cha mgao wa umeme kwaiyo naweza nikasema changamoto ya kwanza ni umeme wa kusuasua kwaiyo jamaa yako atatakiwa kuwa na nishati mbadala sio kutegemea umeme wa tanesco tu
Maji ulikuwa nayo ya uhakika? Tupo calculation za mahesabu yako kwa mwezi ni vipi ili utupatie japo experience kwenye hili
 
Maji ulikuwa nayo ya uhakika? Tupo calculation za mahesabu yako kwa mwezi ni vipi ili utupatie japo experience kwenye hili
Kuhusu maji nilivuta kwa gharama zangu(laki mbili) mwanzoni kabisa wakati nafanya ukarabati wa location, niliunganisha bomba kwenye simtank la lita 1000 ambapo maji yanaenda kwenye simtank halafu mashine ya water pressure naiunganishia kutoka kwenye simtank maji yalikuwepo ya kutosha sikuwahi kupata changamoto.

Umeme nilikuwa nachangia na wengine ila niliweka meter ya kusoma unit ninazotumia mimi peke angu., gharama za uendeshaji nilikuwa nazitenga kwa siku maana kukaa na hela mwezi mzima hapo kati unaweza kutumia kwa mambo mengine halafu ukija muda wa kulipa bills hela haipo.

Kila siku natenga 20k pembeni ambapo maji 5000, umeme 5000, sabuni na spray 4000. Hizo gharama zote hazibaki hivyo hivyo kila siku mfano maji kwa siku naweza kutumia ya 3000 tu, au spray naweza kununua ya elfu 10 nikatumia hata wiki nzima kwahiyo nilikuwa naweka gharama kima cha juu kidogo maana bora hela ibaki kila kitu kikiwa kimefanyika kuliko iishe huku mengine hayajafanyika.

Vile vile nilikuwa natenga 1000 kila siku kwa ajira ya ulinzi na 5000 ya kodi(nilikua nalipa 150k/month kwaiyo 5000×30=150k). Haikua car wash ya hadhi ya juu naweza kusema ni ya hadhi ya chini kuelekea hadhi ya kati. Siku ambayo biashara haikua nzuri nilikua nalaza 20k baada ya kutoa costs zote kuna siku ambazo nilikuwa nalaza mpaka 50k sana sana siku za wikiendi.

Matarajio yangu yalikuwa mengi ikiwemo kuongeza mashine ili nihudumie magari mengi kwa pamoja na kuongeza eneo ili niweze kuhudumia mpaka magari makubwa kama mabasi ya mikoani ni mpaka pale mgao wa umeme ulipoanza biashara ikawa inasuasua umeme unakatika saa 2 asubuhi unarudi saa 1 usiku, nikalazimika kufunga biashara.

Kwahiyo kwa upande wangu changamoto iliyoniangusha ni mgao wa umeme.
 
Kuhusu maji nilivuta kwa gharama zangu(laki mbili) mwanzoni kabisa wakati nafanya ukarabati wa location, niliunganisha bomba kwenye simtank la lita 1000 ambapo maji yanaenda kwenye simtank halafu mashine ya water pressure naiunganishia kutoka kwenye simtank maji yalikuwepo ya kutosha sikuwahi kupata changamoto. Umeme nilikua nachangia na wengine ila niliweka meter ya kusoma unit ninazotumia mimi peke angu., gharama za uendeshaji nilikua nazitenga kwa siku maana kukaa na hela mwezi mzima hapo kati unaweza kutumia kwa mambo mengine halafu ukija muda wa kulipa bills hela haipo. Kila siku natenga 20k pembeni ambapo maji 5000, umeme 5000, sabuni na spray 4000. Izo gharama zote hazibaki ivyo ivyo kila siku mfano maji kwa siku naweza kutumia ya 3000 tu, au spray naweza kununua ya elfu 10 nikatumia hata wiki nzima kwaiyo nilikua naweka gharama kima cha juu kidogo maana bora hela ibaki kila kitu kikiwa kimefanyika kuliko iishe huku mengine hayajafanyika vile vile nilikua natenga 1000 kila siku kwa ajira ya ulinzi na 5000 ya kodi(nilikua nalipa 150k/month kwaiyo 5000×30=150k). Haikua car wash ya hadhi ya juu naweza kusema ni ya hadhi ya chini kuelekea hadhi ya kati. Siku ambayo biashara haikua nzuri nilikua nalaza 20k baada ya kutoa costs zote kuna siku ambazo nilikua nalaza mpaka 50k sana sana siku za wikiend. Matarajio yangu yalikua mengi ikiwemo kuongeza mashine ili niudumie magari mengi kwa pamoja na kuongeza eneo ili niweze kuhudumia mpaka magari makubwa kama mabasi ya mikoani ni mpaka pale mgao wa umeme ulipoanza biashara ikawa inasuasua umeme unakatika saa 2 asubuhi unarudi saa 1 usiku, nikalazimika kufunga biashara. Kwaiyo kwa upande wangu changamoto iliyoniangusha ni mgao wa umeme
Pambana urudi mzee, tafuta generator Mungu ni mwema utainuka tena... Nimependa unaijua kazi na unaipenda kazi na unaiheshimu kazi...
 
Pambana urudi mzee, tafuta generator Mungu ni mwema utainuka tena... Nimependa unaijua kazi na unaipenda kazi na unaiheshimu kazi...
Nilipambana mkuu niliweka sokoni kiwanja changu ili nipate hela ya kununua mashine inayotumia mafuta bahati mbaya sikupata mteja kwa wakati, kwa sasa napambania ugali kivingine mkuu ila kwa sababu nina ujuzi na uzoefu nikipata hela nafikiri biashara ya car wash itakua ya kwanza kuifikiria
 
Nishawahi kufanya biashara ya car wash lakini aikua automated, biashara yangu ilikufa mwaka jana kipindi cha mgao wa umeme kwaiyo naweza nikasema changamoto ya kwanza ni umeme wa kusuasua kwaiyo jamaa yako atatakiwa kuwa na nishati mbadala sio kutegemea umeme wa tanesco tu
Na maji
 
Kuna jamaa aliniuliza kuna changamoto gani au kero zinakumbananazo car wash za hapa bongo kwa. Maana yeye alitaka siku moja aanzishe automated car wash.kama hio hapo chini


View: https://youtube.com/shorts/gp6_tX0no50?si=VHD5CWh6KZ_epVth





nikaona isiwe tabu wacha niulize huku jf labda kuna watu wenye uzoefu kuhusu hili biashara labda naweza pata kitu nikamsanua jamaa

Sasa wadau msiniangushe basi plz!!!!!!!!

Mimi nilikufungua car wash ya ki local, nilinunua ndoo kubwa na madumu mawili brush mbili, sabuni na shampoo na vitambaa. Nilikuwa naingiza elfu 25 mpaka 40 na siku nyingine nachoka kuosha magari.

Kuosha gari nje na ndani siyo kazi rahisi tena kwa mikono bila machine. Bei zangu kwa gari dogo elf 5. Niliacha kwasababu nilikuwa nafanya nikitoka kazini na wateja wangu walikuwa maeneo ya kazini.

Nilipoenda mkoa mwingie kazi ya car wash nikaiacha. Kujiari luxurious sana muda wote unashika pesa. Yaani mimi nilikuwa sikosi pesa elf 15 kwa siku ni kawaida hapo nimeshakula na kuweka vocha ya elf 2 kwa kila siku.
 
Huduma unayotoa ni ya aina gani?

Mbali na hiyo je huwa una offer promotion? ( Weekend promotion n.k )

Mtoa huduma wako ni competent kwenye hiyo kazi? Maana biashara is a war kati yako na mpinzani wako.
Jamaa anataka ndo aanze biashara so ndo anajifunza kupitia kwa wazoefu kupitia Jf, mambo ya promotion anataka awe anatoa full service kabisa
 
Naona nikamwambie jamaa yangu atafute mtu mwenye uzoefu na biashara hii washirikiane pamoja kuendesha biashara ili iwe rahisi kupambana na changamoto hizo
 
No mie sina uzoefu nikatika tustori tu ndio nikaja huku kwa wazoefu walau nipate cha kumwambia jamaa yangu
 
Meaning that unatakiwa uwe na chanzo cha maji kama kisima na vyanzo vingine vya maji ili biashara isonge ?
Ni kweli mkuu katika biashara lazima uwe na plan B., mimi nilivuta maji ya dawasco nikaweka meter yangu kabisa lakini bado nilikua na simtank la lita 1000 kila siku ninapofunga ofisi nahakikisha limejaa, na likijaa ni maji ambayo naweza kuyatumia mpaka wiki mbili sasa hapo hata maji yakikatika wiki nzima kazi inaendelea kama kawaida. Changamoto ilikua umeme maana sina jenereta na mashine ya water pressure haitumii mafuta sasa hapo tanesco wakifanya yao sina ujanja
 
Kuhusu maji nilivuta kwa gharama zangu(laki mbili) mwanzoni kabisa wakati nafanya ukarabati wa location, niliunganisha bomba kwenye simtank la lita 1000 ambapo maji yanaenda kwenye simtank halafu mashine ya water pressure naiunganishia kutoka kwenye simtank maji yalikuwepo ya kutosha sikuwahi kupata changamoto.

Umeme nilikuwa nachangia na wengine ila niliweka meter ya kusoma unit ninazotumia mimi peke angu., gharama za uendeshaji nilikuwa nazitenga kwa siku maana kukaa na hela mwezi mzima hapo kati unaweza kutumia kwa mambo mengine halafu ukija muda wa kulipa bills hela haipo.

Kila siku natenga 20k pembeni ambapo maji 5000, umeme 5000, sabuni na spray 4000. Hizo gharama zote hazibaki hivyo hivyo kila siku mfano maji kwa siku naweza kutumia ya 3000 tu, au spray naweza kununua ya elfu 10 nikatumia hata wiki nzima kwahiyo nilikuwa naweka gharama kima cha juu kidogo maana bora hela ibaki kila kitu kikiwa kimefanyika kuliko iishe huku mengine hayajafanyika.

Vile vile nilikuwa natenga 1000 kila siku kwa ajira ya ulinzi na 5000 ya kodi(nilikua nalipa 150k/month kwaiyo 5000×30=150k). Haikua car wash ya hadhi ya juu naweza kusema ni ya hadhi ya chini kuelekea hadhi ya kati. Siku ambayo biashara haikua nzuri nilikua nalaza 20k baada ya kutoa costs zote kuna siku ambazo nilikuwa nalaza mpaka 50k sana sana siku za wikiendi.

Matarajio yangu yalikuwa mengi ikiwemo kuongeza mashine ili nihudumie magari mengi kwa pamoja na kuongeza eneo ili niweze kuhudumia mpaka magari makubwa kama mabasi ya mikoani ni mpaka pale mgao wa umeme ulipoanza biashara ikawa inasuasua umeme unakatika saa 2 asubuhi unarudi saa 1 usiku, nikalazimika kufunga biashara.

Kwahiyo kwa upande wangu changamoto iliyoniangusha ni mgao wa umeme.
Wakati na comment uzi huu sikuwahi kutegemea kama nitafikiria kuanza biashara ya car wash. Niko nafanya utafiti hapa katika hii biashara na nafikiria kuianzisha. Mashine yakuosha gani ni ipi nzuri ambayo unaweza recommend mtu. Asante
 
Back
Top Bottom