Uchaguzi 2020 Ni dhahiri kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, Watanzania tulishajifunza

Uchaguzi 2020 Ni dhahiri kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, Watanzania tulishajifunza

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
6,404
Reaction score
6,969
Kwa namna mambo yanavyoendelea hivi sasa hapa nchini ni wazi kuwa hakuna dhuluma iliyofanyika kwenye uchaguzi mkuu Oktoba 28 2020.

Ushahidi pekee wa picha zilizopigwa kihuni na watu kuchoma kura zilizokamatwa Kawe hauna mashiko,watu waliupuuza mapema. Na mpaka sasa Halima amethibika kuwa mhuni wa kisiasa,maana makamanda wenzake wamepigwa na butwaa. Amewathibitishia kuwa hakuibiwa kula bali ni msanii.

Aliyegonga msumari wa mwisho ni Zitto maana sasa huku ni kuonyesha watanzania na jumuia ya kimataifa,kuwa mwanzoni walipika uongo ili kupata huruma ya watu na jumuia za kimataifa. Picha ya mtu aliyechomwa,kuvunjwa mkono alafu anateuliwa na kuwa mjumbe wa baraza la wawakilishi kisha anakubali kiulaini,imeshangaza sana.

Watanzania sio wajinga muwafanyie upuuzi kila chaguzi zinapokuja. Ndio maana hawataki kusikia habari ya maandamano au kuunga mkono upinzani uchwara.

Fikiria nani mwenye akili timamu kwa sasa atakubali kuwa kuwa upinzani ulidhurumiwa? Dhuruma ambazo zinaletwa na wafuasi wachache wa upinzani mitandaoni! Huku kiuhalisia wananchi walipiga kura na kusubiri matokeo,dhuluma hizo hawakuziona kwa macho

Watanzania walishajifunza jambo ambalo upinzani unatakiwa ujue kuwa walishashutukiwa,ili kujenga imani tena kwa watanzania itachukua muda mrefu.
 
Unadhani hatukuwepo wakati wa uchaguzi?
Chadema ndiyo kete mlutibaku naye, endelea na usanii wenu.Kama kweli mliibiwa mmepeleka malalamiko manfapi mahakamani.Mnavyopenda kesi mngekuwa na ushahidi, siku nyingi kibatala angekuwa keshalamba advance
 
Kuwepo kwenu ndio mtudanganye kwa video za uongo mnachoma kura?
Je kama no video za Uongo kwa nini Polish hawawakamata kina Mdee kwa kusambaza hizo videos?
Kwa mujibu wa sheria ya Cybercrime ni kosa kusambaza taarifa za Uongo kwenye mitandao
 
Je kama no video za Uongo kwa nini Polish hawawakamata kina Mdee kwa kusambaza hizo videos?
Kwa mujibu wa sheria ya Cybercrime ni kosa kusambaza taarifa za Uongo kwenye mitandao
Hilo swali waulize polisi.
 
Chadema ndiyo kete mlutibaku naye, endelea na usanii wenu.Kama kweli mliibiwa mmepeleka malalamiko manfapi mahakamani.Mnavyopenda kesi mngekuwa na ushahidi, siku nyingi kibatala angekuwa keshalamba advance
CCM ya CHADEMA imesema ule haukuwa uchaguzi. Utafungua Election petition wakati huna documents za muhimu mfano karatasi za matokeo ya uchaguzi?

Je, unaweza kufungua kesi kupinga matokeo ya Uchaguzi wa Rais?
 
Haukuwa uchaguzi bali ulikuwa ni uchafuzi wa demokrasia!
709081.jpg
12460.jpg
098765.jpg
 
Sio la kuuliza Polisi peke yao tafsiri take ni kwamba kilichotokea ni kweli ndiyo mana hawajawakamata
Kutokamatwa na polisi ndio kuwa sababu hakuna kosa?
 
Kutokamatwa na polisi ndio kuwa sababu hakuna kosa?
Hakuna kosa ndio kwa sababu ile issue ina public interest kubwa sana hivyo polisi wangewakamata haraka ili kulinda image ya taifa letu.
 
Kama ni ushahidi kweli,mlipaswa kuutunza mfungue kesi. Lakini mbona Halima amefanya uhuni? Uhuni ambao umethibisha wapinzani ni wahuni.
Utafungua election petition bila nakala ya matokeo?
 
CCM tuna takataka za kutosha. Mjinga analewa wanzuki anarukia kupost tuu. Wapinzani hawa wameangalia Taifa na maskini wake wakiendelea kugoma tunakosa wote misaada na sifa nzuri kimataifa....
Siasa haina muda,siasa ni maisha ya kila siku ya wananchi ambayo yanajumuisha upatikanaji wa maendeleo na huduma za jamii. Huwezi kuwa na siasa safi kama una wapinzani njaa na matapeli. Bora wagome tukose misaada kama kweli wameonewa kuliko kufanya upuuzi kama huu. Haujui lolote unakurupuka kufoka bure.
 
Kama ni ushahidi kweli,mlipaswa kuutunza mfungue kesi. Lakini mbona Halima amefanya uhuni? Uhuni ambao umethibisha wapinzani ni wahuni.
Yaani kesi ya Tumbili nipeleke kwa Ngedere?Hapo kuna kutolewa haki kweli?Unaelewa kuwa kwa sasa hivi mahakama imewekwa mfukoni na mtu mmoja?Inahitaji degree ya PhD kujua ya kwamba mhimili wa mahakama pamoja na bunge umewekwa mfukoni na mtu mmoja?
5678901.jpg
87659087.jpg
 
Acha hasira kamanda, naeleza ukweli wa mambo.
Haahaa ukweli gani mkuu? Nani kamanda? Wako wasimamizi waligeuka watiki vibuti kwenye vituo vya kupigia kura badala ya kuwaongoza wapiga kura kupiga kura.uchafu uliofanyika kwenye uchaguzi wa mwaka huu hata shetani alitushangaa
 
Back
Top Bottom