Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu nikuulize, hapo si unatumia mtandao wa simu? Sitaki kujua mtandao gani ila ni mara ngapi unasikia matangazo ya huo mtandao wa simu yako? Hujui marketing wewe, hivyo katika mambo mengine ukae kimya.
Kadhalika hakuna uscammer katika TMT au JP Markets. Hiyo link na tafsiri ya scammer uliyoweka hapo haihusiani na haya ninayoandika hapa. Wacha wale wanaohitaji kusikia kinachoelezwa wasikie na watekeleze. Wakienda huko na kuona matarajio yao hayakutimia ndio wafanye wanavyoona ni sahihi
Kazingua sana huyu jamaa kaandika bandiko lefu kinoma halafu ndani umejaa utumbo m***ckMleta mada kama hajui namna ya kumtambua fake forex broker na anajiita amehitimu training ya forex hii ni aibu ya kiwango cha lami. Kujua broker bora ni basic knowledge kwa trader yoyote mwenye kuijua forex.
Kuanzia kichwa cha habari mpaka uzi mzima sijaona mahali popote umejbu walau hoja moja ya kashfa anazotupiwa huyo Jp Markets.
Kwa aina ya forex trader kama ya mleta mada sishangai kuona kila siku watu wanalia na kusema forex ni utapeli.
Sasa kumbe na wewe bure tu? Kama unajua kuna huo utapeli kwenye simu kwa nini usipige kelele uone ni kawaida wakati wengine wakipromot kazi zao ndio uone utapeli? Tuliza mpira mkuuJust to alert you .. Matangazo mengi mengi ya mitandao ya simu ni wizi... Wanatumia kila njia wakuchomoe sh 100 au 200 ktk tangazo wanalotaka ujiunge.. Sometimes unakuta kama tigo wanakuunga ktk huduma hata hujajiunga ww then wanaanza deduction zao monthly kama 200 hv bila ww kujua, multiply watu 1 mil tu utajua wanaiba kiasi gani. Likewise Forex mnatumia uelewa mdogo wa watu kuwaibia kiaina tht is what a scammer does..!!
Kama ulikuwa hujui pia utapeli wa kimtandao hasa ktk mitandao ya simu kutumia data kuibia wateja thru MBs ukiacha huduma za kujiunga bila kujua za sms ni mkubwa sana au hiyo Forex ni mwingi sana sana, biashara kuwa halali haimaanishi hakuna scammers, wapo, na kukosa uaminifu na kuanza kuwadokolea wateja fedha zao bila wao kujua ni scamming, so acha kutumia nguvu hivyo kuaminisha watu TMT au JP ni exceptional, you are all under the same trend, wizi wa kiaina bila wateja kushtuka.. Labda nyie mnafanya wizi kidogo kidogo baadae mtaongeza.. Na kwanini [HASHTAG]#Ontario[/HASHTAG] uje na ID nyingine humu?
Sasa kumbe na wewe bure tu? Kama unajua kuna huo utapeli kwenye simu kwa nini usipige kelele uone ni kawaida wakati wengine wakipromot kazi zao ndio uone utapeli? Tuliza mpira mkuu
Clap Clap Clap... Sasa unangoja nini kwenda kupeleka mashitaka ya hao scammer wengine?Did you know how we strictly squeezed TCRA na mchezo huo wa makampuni ya simu umekoma kwa 90%..? Au ulijua watu kama mm ni wa kutulia ? Once nikiwa na concrete evidence there is NO WAY UTAPONA.. Why? Sbb jua ukiwa na ushahidi wa kutosha hata mmoja tu wa kampuni ya simu kukuibia mfano, ukawashtaki utalipwa millions sbb sio mtu mmoja tu watakuwa walimchezea huo mchezo, compensation ni kubwa utalipwa kuwa mfano. Most internet businesses scamming ndio njia kubwa ya kujipatia fedha za haraka haraka na kuwaibia wateja, huo ndio ukweli
Clap Clap Clap... Sasa unangoja nini kwenda kupeleka mashitaka ya hao scammer wengine?
Mkuu siungekuja tu na ile id yako pendwa?Kuna usemi mpya unasema “Heri walimkavu kuliko walimwengu.” Penye walimwengu pana pana mengi. Nasema hivi kwa nini. Kiuhalisia tuliletewa hii fursa na kijana mwenzetu ambaye naweza sema si mhangaikaji tu, bali anajua anachokihangaikia. Si mwingine ni Sirjeff, almaarufu kama Ontario. Sina sababu ya kurudia kile alichowahi kuandika kuhusu namna gani aliweza kuileta na kuitangaza forex hapa nchini.
Kabla sijaenda sana napenda kutangaza maslahi kuwa name ni mmojawapo wa wanufaika wa fursa hii ya forex. Tangu batch ya kwanza kabisa pale mwaka jana mwezi wa tisa hadi leo miezi sita naendelea na forex huku nikiendelea kujifunza mengi kila siku maana forex ni forest kweli. Baada tu ya ujio wa forex nchini ni mengi yamefanyika ikiwa ni pamoja na kusemwa, kuandikwa, na kutendwa.
Kwa kipindi chote hiki cha kuandikwa na kuzungumziwa kwa forex kwa mema na mabaya, nimewahi kuchangia tu mara chache. Aghalabu huwa nasoma kila kinachoandikwa. Walianza kuandika kuhusu forex kuwa ni utapeli. Ni DECI mpya. Ni pyramid scheme, na kwamba siku itafika watu wataficha nyuso zao na kwa kuwa yaliyosemwa yametimia. Haitokaa itokee. Bado wako watu wengi sana wanaamini kuwa forex ni kama ile michezo ya kubahatisha. Well, ukiamua kwenda kwa staili hiyo haujakatazwa. Wapo pia wanaoendelea kuamini kuwa forex ni DECI. Ni ponzi scheme. Well, wako wajanja wanaoitumia forex kuendesha hizo DECI. Hivyo forex ni kama kisu ulichonunulia kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Sasa akaja mtu akakitumia kumuumiza mwenzie haimaanishi kisu kibaya bali matumizi hayakuwa sahihi, hivyo aliefanya matumizi yasiyo sahihi ndiye mwenye matatizo.
Baada ya baadhi ya wale wadau wa mwanzo kupata elimu ya forex (basic knowledge) kupitia kampuni ya The Million Team (TMT) chini ya JP Markets ambaye ndiye broker tunayemtumia hadi sasa, kelele zilianza. Ukweli ni kuwa kila kitu kipya kina changamoto zake. Yawezekana malalamiko yao yalikuwa yana ukweli ila wakakosa staha na uvumilivu katika kuwasilisha na kuona wanachokitaka kinachelewa.
Yaani u introduce forex mwezi wa tisa, na baada ya miezi mitano kila kitu kiwe kama wateja wanavyotaka? Ni ngumu. Wako waliokuja humu jukwaani kukiri kuwa hakika forex ni mkombozi. Wanatengeneza pesa ambayo walikuwa hawajafikiri kutengeneza hapo awali. Kwamba forex sio imekuja wakati mwafaka, bali imechelewa sana. Forex haikuchelewa. Kutokana na ukwasi uliopo kwenye hii biashara, wako watu hapa nchini waliijua mapema na wakawa wanafanya yao kimya kimya bila kutaka wengi wajue haya. Wapo watu binafsi pamoja na taasisi za kifedha. Sasa kati ya hao ambao wameona maslahi yao yanaingiliwa na TMT basi rafu nazo zikaanza.
Sasa turudi kwa wale wafaidika wa forex ya TMT. Ni hulka ya binadamu kutaka zaidi ya kiasi, na kuwa mdadisi na kutaka kujiongeza. Sasa baada ya hawa wenzetu kuona kasi wanayoitaka na mambo wanayoyataka hayaji kwa kasi waliyojipangia, wakaanza kunena mabaya kuhusu TMT pamoja na broker husika.
Kiukweli mabaya mengi yameandikwa kuhusu TMT pamoja na JP Markets. Kwa mtu asiyependa kutafakari atasema basi tena, pale hamna kitu. Lakini sisi ambao bado tupo tunajua nini tunataka, nini tunapata, na tufanye nini panapotokea changamoto kadhaa. Matatizo yalianzia na broker, kisha TMT. Mbaya zaidi ikashuka hadi kwa CEO wa TMT – Ontario. Yote hii ikiwa ni harakati za kuvuruga na kuona jamaa wanakufa kibiashara na kupotea. Si rahisi hivyo. Nitaeleza kwa nini.
Broker
Suala la broker ni suala tete sana, watu hawajui tu. Wengi wa brokers tunaowatumia, nje ya huyu ambaye wawakilishi wake wapo hapa nchini, tunafanya nao miamala kwa ile tunaita mutual trust. Lolote laweza kutokea na hela yako ikapotelea huko nje. Kwenye forex kuna brokers wengi sana! Inatakiwa upembuzi wa kutosha kujua unafanya biashara yako na broker wa aina gani. Wengi wamepoteza hela zao huko nje bila kujua wanafanya biashara na broker wa aina gani. Wengi wa waliokuwa wanakuja hapa jukwaani kuiponda TMT, CEO wake, pamoja na JP Markets walikuwa/wanatoa mbadala wa brokers wao ambao kwa namna moja ama nyingine wana maslahi nao.
Hatukatai kuna ushindani. Waswahili wanasema usiache mbachao kwa msala upitao. Tena wakasema usitukane mamba ungali hujavuka mto. Singependa sana kuwazungumzia brokers hao ambao wamekuwa sababu ya huyu waliyekuwa naye mwanzo kunenewa mabaya. TMT walituletea JP Markets. Tunawajua TMT na ofisi zao tunazijua. Kwa tatizo lolote ofisi zao ziko wazi, hivyo hakuna namna yoyote unaweza kufanya miamala yako na broker akashindwa kukulipa halali yako wakati TMT tuko nao.
Tuko na JP kwa kuwa waliingia makubaliano na TMT, na kwa lolote wako tayari kushughulikia. Yako mambo kadhaa ambayo kati ya hayo ndiyo yalipelekea wadau kufitini na kuja huku na kuanza kumwaga ugali na mboga. Mambo waliyoona kwao ni kero sasa yapo ambayo yameshafanyiwa kazi, ikiwa ni pamoja na spreads kupunguzwa. Kama si mdau wa forex itakusumbua kujua baadhi ya masuala. Wapo ambao waliona urahisi wa kufanya miamala yao kwa njia ya mobile money kama mpesa, tigopesa na airtel money kupitia kwa hao broker wengine. Uzuri ni kuwa wakati sio mwingi huduma hiyo itaanza kufanya kazi kupitia JP Markets. Hata hivyo kwa sasa ukihitaji kuwithdraw cash yako toka JP Markets inakuchukua saa kadhaa tu.
TMT
The Million Team ambao ndio wanaoiwakilisha JP Markets uzuri tunawajua. Tunakutana nao na kuwasiliana nao wakati wowote. Wao kama kampuni wana wajibu wa kuhakikisha kuwa sie wateja wao tunapata kile tunachohitaji, ikiwa ni pamoja na urahisi wa huduma ya uwekaji na utoaji pesa toka kwa broker. Kingine kupata elimu ya forex na mafunzo endelevu hadi hapo mtu atakapoona anaweza kujisimamia.
Kama kuna tatizo limetokea, suluhu si kutoka na kwenda pembeni kutukana na kuleta ujuaji. Mtu mzima, tena mwanaume unakuja kupandisha uzi humu kuwasema watu wengine, kisa hujulikani, ni uzezeta tu. Mtu anakuvusha mto kwa kukubeba mgongoni unafika ng’ambo unasema, ‘limgongo lake linanuka…!’ Si watu hao. Zikitokea kasoro tunapeana ukweli humo humo kwenye grupu zetu na kwa uwazi na mwisho wa siku zile kasoro zinaondoka.
Yapo mengi tuliyowashauri TMT kama kampuni. Nao kwa uchanga wao wanaendelea kujifunza mengi. Nao siku na wakati ukifika kulingana na malengo yao wamepanga kuwa broker hapa nchini. Kama wamekuwa wa kwanza kutuletea elimu hii kwa uwazi, tuwatakie heri pia wafanikiwe kuwa broker wa forex hapa nchini ili hii huduma iwe rahisi zaidi nay a uhakika zaidi na karibu zaidi.
HITIMISHO
Forex ipo na itaendelea kuwepo. Kama hatuwezi nasi kuwa hao broker, sembuse kuleta elimu hii kwa wengi na kwa uwazi, tuwaunge TMT mkono katika kufanikisha haya. Tuone kuwa forex inakuwa sehemu ya ajira kwa vijana wengi ambao ajira imekuwa changamoto. La msingi ambalo TMT wakishirikiana na wadau wengine wanapaswa kufanya ni kutoa elimu sahihi kuhusu forex. Kwamba forex sio a get rich quick scheme. Kwamba forex sio bahati na sibu. Kwamba forex ni uwekezaji kama uwekezaji mwingine. Forex inahitaji muda kujifunza kama zilivyo taaluma zingine.
Tumpe moyo kijana mwenzetu, mtanzania mwenzetu Sirjeff ambaye ameiona fursa ilipo akaona sio vibaya kuwapa na wengine fursa hii. Tukiweka nidhamu katika kuifanya forex kulingana na misingi na taratibu zetu, basi lengo na kusudi la mwenzetu huyu litatimia – kuwezesha wengi kujiajiri. Lakini tukianza pupa na kutaka kutajirika na kuwa na ulafi na mwisho kujenga chuki na kuchafuana, forex itaonekana ni blah blah (kitu ambacho si sahihi kabisa) na mwisho lengo la mleta fursa halitatimia.
Tena wahenga wakaendelea, usidharau nazi. Embe tunda la msimu. Uzuri itafika siku na wale wote waliokuwa na nia mbaya na hawa jamaa (TMT) watarudi kuwa sehemu ya TMT. Wako watakaorudi kimya kimya na wako watakaokiri hawakuwa sahihi kutupa jongoo na mti wake. Hivyo basi natoa wito kwa wale ambao kwa namna moja au nyingine walikatishwa tamaa na hoja nyingi mfu zilizoletwa humu jukwaani waone tena sababu ya kujitafakati tena na kuichangamkia fursa hii. Kwa wale ambao hawaijui TMT na mahali ilipo, ni Oyaterbay karibu na kituo cha mbuyuni barabara ya Ali Hassani Mwinyi. Jingo linaitwa Jangid Plaza.
Dah! Niseme tu sioni kipya kwenye kauli zako. Mimi hapa nasema na ninawataarifu wadau kuwa TMT wanaendelea na kozi yao fupi pale Jangid Plaza, Oysterbay. Tarehe 24 kutakuwa na classes so unaweza kuja kupata fundamentals za forex. Kingine ni mentorship ya lifetime, ila kama itafika wakati ukaona unaweza kusimama kwa miguu yako mwenyewe unaruhusiwa kuaga na kwenda kuwa independent trader.Time is coming... you will tell me..!! Kikubwa as i stated ni concrete evidences, then legal and illegal procedures will follow...!! Kikubwa ni kufanya business halali na kutofanya scamming ktk hizo businesses.. Bahati nzuri watu tukikaa kimya sio kwamba hatujui, tunajua sana but we are waiting certain stage ili upate kila kitu to take action..
TMT ulufukuzwa mwaka gani? Natumia neno ulifukuzwa maana hata lugha unayoongea ni ya ukakasi. Nitakujibu kwa ufupi tu. Hata hao brokers unaowaamini wewe leo kuna watu walipita huko na wakaumia pia. Hadi leo huwa nasoma reviews za broker wengi na unakuta clients wanalialia sana, so wakati mwingine ni suala la subjectivity. Kama wewe vile, unaonekana wazi kabisa kuwa ni mtu wa mambo ya uharaka haraka. Hata kama ulikuwa unakosoa ni wazi kuwa ulikuwa unatumia lugha ya ukakasi. Kama unatumia lugha sahihi ni wazi kabisa ungekuwepo hadi leo. Mimi ni mmojawapo wa wakosoaji wakubwa wa mambo ninayoyaona hayaendi sawa, na ninatumia lugha ya hekima. Sasa wewe, hata sijui umri wako ni wazi una mbwembwe katika ukosoaji na ndio maana unatupiwa virago.
Suala la IB liko wazi. Inaelekea hata wewe baada ya kujua jua kidogo analysis tokea TMT ukaona ni fursa ukakimbilia kwa hao wanaokupa link ili na wewe upate kamisheni kwa kila atakayetumia link yako. Sio mbaya ila ufanye kwa staha na sio tena kurudi kuanza kutukana ulikotoka ili upate na wewe vichwa.
Mwisho nasema wewe ndio uache UNAFIKI kwa kuwa unaongea mambo ya TMT kwa namna ambayo huijui kwa kuwa ulufukuzwa na hauko tena. Hata katika taasisi yoyote mfanyakazi au mteja akiwa kihrehere na mzandiki atafukuzwa tu maana kwa u-moja wako huongezi wala kupunguza kitu. TMT ipo na itaendelea kuwepo. Wanaendelea kupokea maoni na kuboresha kilichopo na mwisho wa siku usishangae na wewe ukajivuta tena TMT kisa tu kila kitu kinafanyikia hapa bongo. Kwa heri
TMT walituletea JP Markets. Tunawajua TMT na ofisi zao tunazijua. Kwa tatizo lolote ofisi zao ziko wazi, hivyo hakuna namna yoyote unaweza kufanya miamala yako na broker akashindwa kukulipa halali yako wakati TMT tuko nao.
Naomba nikujibu kwa mkupuo kama ifuatavyoHii statement umeandika Only kwa sababu hauijui vizuri sheria ya Contracts ilivokaa. Labda kwa kukusaidia naomba ukatafute Law Of Contract Act CAP 345 R.E 2002. Kasome vizuri Parties as an important element in a contract. Then uje unijibu kwamba TMT anaingiaje kwenye contract yako ww na JP markets?
Mosi; suala la IB na tutor ni kweli lina conflict of interest kama broker ni market maker. Kama sio basi hata trader akiunguza hela zinaingia moja kwa moja sokoni na si kwa market maker. Hii pia haizuii broker kuwa na namna zake za kupata sehemu ya hizo hela zinazoingia sokoni. Ninajua pia kuwa brokers wana access na baadhi ya setup za platform wanazotumia, kama mt4. Kwa muktadha huo hakuna aliyesalimika %100 bila kujalisha ni broker toka wapi. Ndio maana unasisitiziwa kuwa na risk management na kuchunga sana margin call.
Pili; ishu ya contract sitaki kuingia sana ila mimi ni third party kati ya hawa watu wawili. Kwa lugha nyingine mimi ni mdau. Nasema hivyo kwa maana CEO mwenyewe wa JP Markets amejoin grupu letu/zetu kuja kutoa ufafanuzi ambao tulihitaji kujua. Japo umesema contract ni kati ya JP na TMT umeona sasa nasi tumehusika. Bila clients hakuna huyo JP au yeyote yule.
Unajua, wakati forex inakuwa introduced hapa hatukuwa tunamjua broker yoyote [wengi wetu]. Sasa alipokuja TMT na ambaye ni IB alifanya hayo kwa niaba yetu. Tulijiunga na JP kwa kupitia TMT ambaye anatoa mafunzo pamoja na maelekezo mengine. Kwa lugha nyingine TMT wanahusika sana kuprotect interests za clients kwani hata deposits zingine zinapitia pale. Ikifika wakati ukawa independent trader si lazima kuwa chini ya TMT. Unaweza kuwatafuta mwenyewe kwa njia zako ukadeposit, ukatrade na kuwithdraw. Hapo TMT hawahusiki kwa vyovyote. Kwa utaratibu wa sasa TMT wako liable kwa lolote litakalotokea. Hii naona iko sawa maana TMT iko registered hapa bongo. Ila pia ikifika wakati na wao wakawa broker, itapendeza zaidi kwa kuwa tunawajua1. Conflict of interest is just conflict of Interest no matter ni aina gani ya broker
2. It seems like haufahamu jinsi market maker brokers wanamake hela.
3. Inaonekana ni wazi hauijui flow ya money kuanzia kwenye Interbank mpaka inamkuta Retail trader.
4. Unaposema brokers wana access na setup za platform mfano ni setup zipi? Na wao kuwa na hiyo access how is it going to affect you?
1. Yaani contract umeingia ww na Jp markets, halafu ww uwe Third party tena?
2. Hakuna sehemu nimetaja contract kati ya Jp markets na TMT
3. CEO kuwa ndani ya Group is not a big deal na ni kwa sababu nyinyi ni clients wake.
4. Swali lilikuwa kama leo hii umezuka mgogoro let say Jp markets wamekataa kuwalipa hela. Mkaamua kufungua Kesi mahakamani maana migogoro ndio inayowapeleka watu mahakamani. Kesi yoyote lazima iwe na parties wawili, Part ya kwanza ni ww na part ya pili ni Jp markets. Now tell me TMT anaingia wapi?
Hujausoma uzi wewe. Tatizo unasoma tu vichwa vya habari na kukimbilia kuandika. Sio nzuri kiafyaWabongo kwa majungu bwana utasema tumelogwa! Ontario ana make money nyie kazi kubwabwaja tu. Tudownload pesa bwana na tutafute skills zaidi za kudownload hela hapa mjini. Mtaongea na kufungua nyuzi kibao za ontario lakini yeye anawachora tu maana mtaishia kusemasema tu halafu hakuna kinachoendelea! KAMA KWELI MMEONA UMUHIMU WA FOREX KATIKA MAISHA YENU KWA NINI MSIACHANE NA ONTARIO MKAPIGA ZENU PESA!? TUFANYE KAZI YA KUDOWNLOAD BWANA NA KWA WALE MAGWIJI FUNGUANI NYUZI ZA KUELEMISHANA ZAIDI SIYO HIZI ZA MAJUNGU YA KISWAHILI SWAHILI!