Ni ipi ngeli ya neno MAITI?

Ni ipi ngeli ya neno MAITI?

Kuna tofauti gani kati ya neno UWANJA na KIWANJA ?
nimepitia kamusi mbili tofauti moja ni ya TUKI iliyo chapwa na Oxford latest version ambayo inasema ngeli ya maiti ni I-ZI lkn pia nimepitia kamusi ya Longhorn inayosema ngeli ya maiti ni A-WA wajuvi njooni mnijuze ni ipi ngeli halisi ya maiti?

Nawakumbusha pia ngeli ya uwanja ni U-ZI kwa maana hiyo wingi wa neno uwanja sio Viwanja.

Naomba turudi kwenye swali la msingi, msaada tafadhari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa wajuba kwa mfano marehemu ni A-Wa au I-Zi ??
Kwasabau sio kitu hai
Unaweza kusema marehemu ilikuwa mwizi sana
Unapozungumzia alichokifanya marehemu inakuwa unaongelea kitu alichofanya marehemu kipindi cha uhai wake, hivyo utakuwa unaongelea wakati wa uhai wake hivyo itatumika ngeli ya A-WA

ᴾᵘⁿⁱˢʰ ᵒⁿˡʸ ʰᵉ ʷʰᵒ ᶜᵒᵐᵐⁱᵗᵗᵉᵈ ᵗʰᵉ ᶜʳⁱᵐᵉ [emoji377]
 
Kwani ngeli ndo Nini[emoji41]

kelphin kepph
 
Kuna tofauti gani kati ya neno UWANJA na KIWANJA ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Uwanja kipande cha ardhi iliyowazi na kitatumiwa kwa kitu fulani na Kiwanja ni kipande cha ardhi, aghlabu kinachotumiwa kwa kujengwa nyumba.

ᴾᵘⁿⁱˢʰ ᵒⁿˡʸ ʰᵉ ʷʰᵒ ᶜᵒᵐᵐⁱᵗᵗᵉᵈ ᵗʰᵉ ᶜʳⁱᵐᵉ [emoji377]
 
Kwani ngeli ndo Nini[emoji41]

kelphin kepph
Ngeli ni kundi moja la majina yaliyo na upatanisho mmoja wa kisarufi unaofanana na viambishi vya umoja na wingi ambavyo ama hufanana au kulingana.

ᴾᵘⁿⁱˢʰ ᵒⁿˡʸ ʰᵉ ʷʰᵒ ᶜᵒᵐᵐⁱᵗᵗᵉᵈ ᵗʰᵉ ᶜʳⁱᵐᵉ [emoji377]
 
Maiti ni i-zi.

Ngeli ya a-wa, kwa ninavyojua mimi, kwa muktadha huu, ni ngeli inayotumiwa kwa vitu hai.

Kwa mfano. Tunasema meza imepatikana. Hatusemi meza amepatikana. Kwa sababu meza si kitu hai.

Tunasema njia imepatikana. Hatusemi njia amepatikana. Kwa sababu njia si kitu hai.

Tunasema kunguru anaruka. Hatusemi kunguru inaruka. Kwa sababu kunguru ni kitu hai.

Tunasema mtoto amepatikana. Hatusemi mtoto imepatikana. Kwa sababu mtoto ni kitu hai.

Inawezekana tunasema maiti amepatikana katika namna moja ya kuisitiri maiti, tunamuongelea mtu aliyefariki kama mzima, kwa kutumia tafsida ya heshima pekee kwa mtu (kama tunaposema amefariki badala ya amekufa), lakini, hususan kabisa ya maiti ni imepatikana, si amepatikana.

TEACHER.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Maiti ni i-zi.

Ngeli ya a-wa, kwa ninavyojua mimi, kwa muktadha huu, ni ngeli inayotumiwa kwa vitu hai.

Kwa mfano. Tunasema meza imepatikana. Hatusemi meza amepatikana. Kwa sababu meza si kitu hai.

Tunasema njia imepatikana. Hatusemi njia amepatikana. Kwa sababu njia si kitu hai.

Tunasema kunguru anaruka. Hatusemi kunguru inaruka. Kwa sababu kunguru ni kitu hai.

Tunasema mtoto amepatikana. Hatusemi mtoto imepatikana. Kwa sababu mtoto ni kitu hai.

Inawezekana tunasema maiti amepatikana katika namna moja ya kuisitiri maiti, tunamuongelea mtu aliyefariki kama mzima, kwa kutumia tafsida ya heshima pekee kwa mtu (kama tunaposema amefariki badala ya amekufa), lakini, hususan kabisa ya maiti ni imepatikana, si amepatikana.
Nimekuelewa vizuri sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngeli inayotumika hap ni A-WA kwa maana mtu hata kama akifa hadhi yake hubak hai hawez kufananishwa na vtu visivo na uhai japo kwa muda huo hatakuwa na uhai ila haiondowi hadhi yake ivo tunasema maiti atasailishwa na maiti watasafilishwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom