Ni juisi gani ambayo unapendelea kuitumia/kunywa kwa wingi?

Ni juisi gani ambayo unapendelea kuitumia/kunywa kwa wingi?

Shida na raha

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2014
Posts
3,773
Reaction score
3,471
Habari za majukumu wakuu.

Napenda tushee kwa pamoja hili suala maana kila mmoja kuna kitu anapenda na akikiona roho yake inatamani hapa nazungumzia kwa upande wa juisi tu.

Mimi binafsi hata kama nipo kwenye usafiri nikiona juisi ya miwa lazima nisimame na kupata glass mbili sijui kwanini roho yangu inapenda sana ile kitu.

Kwamfano nitoke kwa Azizi ally nimekunywa basi nikifika ferry nikiona tena lazima ninywe, nikivuka kwenda Kigamboni nikiona tena nakunywa yaani naona natamani kuendelea kunywa tu.

Yaani ni sawa sawa na baadhi ya watu humu na pombe yaani hawezi kuacha hata kama alikotoka amekunywa lazima apashe tena mbeleni akiona bar.
Nawakilisha.
 
mchicha,avocardo, mint, ndizi mbichi.


Mtakula Mboga za kondeni. Siwezi kula mchicha mbichi au matembere mabichi ila ukiwa juice balaa sana.
 
mwili wetu umetengenezwa uwe Alkaline, hii kitu au michanganyiko ya aina hii hasa ukinywa kabla ya kula chochote huwezi kubaki kawaida. magonjwa madogo madogo utayasikilizia jf tu.
nipe hatua ya kutengeneza juic hii na je mbadala wa mint unaweza kua upi? ahsante
 
nipe hatua ya kutengeneza juic hii na je mbadala wa mint unaweza kua upi? ahsante
point kuu.
mchicha/spinach/mboga za majani mbichi ni kitu tofauti kabisa na zilizopikwa.
kwa sababu ni vigumu kuzitafuna unazichanganya na juice inakuwa Bomba.

Bado najifunza.
ila mfano juzi nimechanganya...
Nyanya mbili
Nusu Kitunguu.
Mnafu/Chinese kidogo kama robo ya fungu.
Karoti moja.
na embe moja kuleta radha ingawa hapo radha ni kipaumbele cha mwisho.

Osha vizuri, ongeza maji safi Blend kwa pamoja, kunywa kisha unaendelea na mishemishe za siku.

unaweza kujifunza zaidi katika vipindi vya afya vya Dr esperence Kilonzo Youtube


anza Day 1. Kwenye kila video kuna vipondi Vitatu (Afya, Ndoa na Mahubiri).
angalia AFYA maana anafanya practical hapohapo mkuu. Huwezi kutoka kapa.

Badala ya Mint unaweza kuweka hata ndimu au limao.
 
Tangawizi napenda chai yake na mchai chai.

Ila kwa juisi, kila juisi lzm niweke kipande cha ginger.
Mkuu ulisha kunywa juice ya upupu...!!??
[emoji126][emoji126][emoji126][emoji126][emoji126]
 
Tembele na mchicha unatengenezaje juisi yake? Nataka jaribu.
concept iko hivi mkuu.
Mungu alimwambia Adam na hawa watakula Mboga za Kondeni.
Hakuwaumbia jiko la kupikia ila alitegemea watafune wapate first class nutrients.

sasa wewe badala ya Kutafuna majani mabichi kitu ambacho sio momba kiutamaduni unazitafuna kwa njia ya Juice.
Kuna formula unaweza kuzipanga ukawa unakula breakfast bila kuwasha moto na ukawa na afya tele tu.

ndizi mbichi iliyopikwa ni kitu tofauti na ndizi mbichi ukiila katikati ya juice.
Kiazi kibichi ni habari tofauti na kiazi kilichopikwa.
matembere,mchicha,kabichi mbichi ni vitu toafuti kabisa na hivyohivyo vikiwa vimepikwa (palatable but less nutritious ).


jaribu mkuu. Juice ya matembele sio kwa wenye upungufu wa damu tu. unaweza kuyafanya kama ingredient ya juice yako home.
 
Habari za majukumu wakuu.

Napenda tushee kwa pamoja hili suala maana kila mmoja kuna kitu anapenda na akikiona roho yake inatamani hapa nazungumzia kwa upande wa juisi tu.

Mimi binafsi hata kama nipo kwenye usafiri nikiona juisi ya miwa lazima nisimame na kupata glass mbili sijui kwanini roho yangu inapenda sana ile kitu.

Kwamfano nitoke kwa Azizi ally nimekunywa basi nikifika ferry nikiona tena lazima ninywe, nikivuka kwenda Kigamboni nikiona tena nakunywa yaani naona natamani kuendelea kunywa tu.

Yaani ni sawa sawa na baadhi ya watu humu na pombe yaani hawezi kuacha hata kama alikotoka amekunywa lazima apashe tena mbeleni akiona bar.
Nawakilisha.


Juice yangu pendwa ni maziwa ya kina Mama tu.
 
Hii utakuwa unatengeneza mwenyewe aiseeee hebu tupe procedures
nimeweka video sample za mama Dr mkufunzi wa hiyo makitu. Lecture zake ziko kama 11 hivi akifafanua kwa kina.

hakuna procedure za ajabu mkuu.
Hakikisha ni safi, changanya brend kunywa usiweke sukari wala usichuje.
mwili wako ukiwa unatembelea kwwnye alkalinity magonjwa mengi utayaepuka na utakuwa imara.

unaweza kujipa hata wiki kila asubuhi unakula hiyo sharubati (juice) na NUTS(karanga/korosho/almond) utaurudisha mwili katika viwango vyake na ni usafi wa ndani utakaopunguza Bills nyingi za hospitali.
 
nimeweka video sample za mama Dr mkufunzi wa hiyo makitu. Lecture zake ziko kama 11 hivi akifafanua kwa kina.

hakuna procedure za ajabu mkuu.
Hakikisha ni safi, changanya brend kunywa usiweke sukari wala usichuje.
mwili wako ukiwa unatembelea kwwnye alkalinity magonjwa mengi utayaepuka na utakuwa imara.

unaweza kujipa hata wiki kila asubuhi unakula hiyo sharubati (juice) na NUTS(karanga/korosho/almond) utaurudisha mwili katika viwango vyake na ni usafi wa ndani utakaopunguza Bills nyingi za hospitali.
nafikiri constipation na tumbo kujaa gesi vitakua historia pia
 
Juice ya Ndizi.
Unachukua ndizi mbivu kama mkungu mzima,Majani flani hivi magumu. Unaweka kwenye beseni unakamua kwa kutumia majani. Inatoka juice yenye ladha nzuuuri ya majani na ndizi.
 
Back
Top Bottom