Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
Hamjambo wote!
Majukumu ya Baba yapo bayana. Ushaambiwa Ubaba ni cheo cha juu zaidi Duniani.
Na hakijawa cheo cha juu burebure, hivihivi au kirahisi. Ni kwa sababu ya majukumu makubwa aliyopewa Mwanaume ndiye Baba.
MAJUKUMU YA MSINGI YA MWANAUME AU BABA.
1. Kutafuta Fursa na kujijenga kimaisha.
2. Kutiisha Mazingira yake.
3. Kuunda Connections zenye Tija kwake na kwa kizazi chake.
4. Kuandaa Mifumo ya uzalishaji kwa kizazi chake.
5. Kuandaa Urithi WA watoto wake na kizazi chake.
Sio useme Urithi WA mtoto ni Elimu.
Elimu haijawahi kuwa Urithi mahali popote pale.
Na haupo kwenye Sheria za mirathi.
6. Kuwatafutia watoto Kazi za kufanya na connections za uhakika.
Huyo ndiye Baba na mwanaume.
Majukumu hayo ndio humfanya mwanaume yoyote Makini kutokuwa na Muda WA kufikiri mambo ya kijingajinga au kupoteza Muda kwa mambo yasiyo na Tija.
Baba au mwanaume anayejielewa huwezi msikia akiwambia watoto wake wakatafute Kazi za kufanya.
Ila yeye mwenyewe kama Baba anakuwa ameshaandaa mfumo wa vijana kuwa na Kazi au Kupata Kazi.
Labda mtoto mwenyewe aamue kufanya Kazi zingine Nje ya mfumo wa Baba yake.
Ndio maana familia zote kubwa za Watawala, wafalme, wafanyabiashara Wakubwa, matajiri na watu wote wenye kujua Kanuni hiyo mara zote wazazi hasa Baba huhangaika Kufa kupona kuwaweka watoto wao katika nafasi nzuri za kiuchumi.
Kumpa mtoto Elimu haimsaidii chochote kama hukumpa connections na mfumo wa Kazi.
Wanasiasa wote Duniani hujua Jambo hili tangu Duniani kuumbwa.
Wafanyabiashara na matajiri wote huwezi sikia wakiambiwa watoto wao wakatafute Kazi au wawaache watoto wao wajitafutie malisho kama mayatima wasio na Baba.
Baba husema, mwanangu David umeshakua Mkubwa sasa, chukua Ng'ombe hawa watano, eneo la malisho lipo pale.
Mwanangu Kipeto, kuna shamba heka tano lile la Kule Turiani. Tangu mdogo umekuwa na Mkono wa Kulima. Nenda kalime Mwanangu.
Mwanangu Kibadeni, umesoma Udaktari, utaenda katika hospital ya Plus Tune. Fulani atakupokea. Sasa uende ukanitie aibu huko.
Dunia ilianza na connections na itaisha kwa connections.
Hapa Kati wanadamu walitaka kujidanganya kwa kujaribu kujifunza mambo yasiyo ya Asili.
Hii itupe changamoto kama vijana wa Leo tujue yakuwa Sisi kama Wanaume na Wababa wachanga tunaowajibu wa kupambana Sana. Sana tena Sana kwaajili ya Kesho yetu na kizazi chetu.
Usije ukapotoshwa.
Mzazi ndiye mwenye jukumu la kumuwekea mtoto wake mifumo ya kuishi.na sio vinginevyo.
Mzazi wako akishindwa unaasilimia 80% ya kushindwa katika Maisha.
Wewe ukishindwa maisha kuna asilimia 80 ya watoto wako nao kushindwa.
Sio serikali Wala mtu yeyote mwenye jukumu la kukufanikisha.
Mwenye jukumu Hilo alikuwa Baba yako, na kama ameshindwa Basi jukumu Hilo limebaki juu yako MWENYEWE.
Mama unajukumu la kuhakikisha Baba anasaidia watoto kufika Kule anakotaka.
Wanawake bahati nzuri wanaijua hii natural.
Ndio maana ukishaoa hata kama ndio mpo mwaka wa Kwanza na bado vijana utakuta Mkeo anakushinikiza tujenge mapema kwaajili ya watoto wetu.
Tuanzishe miradi kwaajili ya watoto wetu
Ni jukumu letu kama wanaume au Wababa kutengeneza channel kwa watoto wetu. Huo ndio Ubaba wenyewe.
Taikon Master
Kwa sasa Dar es
Majukumu ya Baba yapo bayana. Ushaambiwa Ubaba ni cheo cha juu zaidi Duniani.
Na hakijawa cheo cha juu burebure, hivihivi au kirahisi. Ni kwa sababu ya majukumu makubwa aliyopewa Mwanaume ndiye Baba.
MAJUKUMU YA MSINGI YA MWANAUME AU BABA.
1. Kutafuta Fursa na kujijenga kimaisha.
2. Kutiisha Mazingira yake.
3. Kuunda Connections zenye Tija kwake na kwa kizazi chake.
4. Kuandaa Mifumo ya uzalishaji kwa kizazi chake.
5. Kuandaa Urithi WA watoto wake na kizazi chake.
Sio useme Urithi WA mtoto ni Elimu.
Elimu haijawahi kuwa Urithi mahali popote pale.
Na haupo kwenye Sheria za mirathi.
6. Kuwatafutia watoto Kazi za kufanya na connections za uhakika.
Huyo ndiye Baba na mwanaume.
Majukumu hayo ndio humfanya mwanaume yoyote Makini kutokuwa na Muda WA kufikiri mambo ya kijingajinga au kupoteza Muda kwa mambo yasiyo na Tija.
Baba au mwanaume anayejielewa huwezi msikia akiwambia watoto wake wakatafute Kazi za kufanya.
Ila yeye mwenyewe kama Baba anakuwa ameshaandaa mfumo wa vijana kuwa na Kazi au Kupata Kazi.
Labda mtoto mwenyewe aamue kufanya Kazi zingine Nje ya mfumo wa Baba yake.
Ndio maana familia zote kubwa za Watawala, wafalme, wafanyabiashara Wakubwa, matajiri na watu wote wenye kujua Kanuni hiyo mara zote wazazi hasa Baba huhangaika Kufa kupona kuwaweka watoto wao katika nafasi nzuri za kiuchumi.
Kumpa mtoto Elimu haimsaidii chochote kama hukumpa connections na mfumo wa Kazi.
Wanasiasa wote Duniani hujua Jambo hili tangu Duniani kuumbwa.
Wafanyabiashara na matajiri wote huwezi sikia wakiambiwa watoto wao wakatafute Kazi au wawaache watoto wao wajitafutie malisho kama mayatima wasio na Baba.
Baba husema, mwanangu David umeshakua Mkubwa sasa, chukua Ng'ombe hawa watano, eneo la malisho lipo pale.
Mwanangu Kipeto, kuna shamba heka tano lile la Kule Turiani. Tangu mdogo umekuwa na Mkono wa Kulima. Nenda kalime Mwanangu.
Mwanangu Kibadeni, umesoma Udaktari, utaenda katika hospital ya Plus Tune. Fulani atakupokea. Sasa uende ukanitie aibu huko.
Dunia ilianza na connections na itaisha kwa connections.
Hapa Kati wanadamu walitaka kujidanganya kwa kujaribu kujifunza mambo yasiyo ya Asili.
Hii itupe changamoto kama vijana wa Leo tujue yakuwa Sisi kama Wanaume na Wababa wachanga tunaowajibu wa kupambana Sana. Sana tena Sana kwaajili ya Kesho yetu na kizazi chetu.
Usije ukapotoshwa.
Mzazi ndiye mwenye jukumu la kumuwekea mtoto wake mifumo ya kuishi.na sio vinginevyo.
Mzazi wako akishindwa unaasilimia 80% ya kushindwa katika Maisha.
Wewe ukishindwa maisha kuna asilimia 80 ya watoto wako nao kushindwa.
Sio serikali Wala mtu yeyote mwenye jukumu la kukufanikisha.
Mwenye jukumu Hilo alikuwa Baba yako, na kama ameshindwa Basi jukumu Hilo limebaki juu yako MWENYEWE.
Mama unajukumu la kuhakikisha Baba anasaidia watoto kufika Kule anakotaka.
Wanawake bahati nzuri wanaijua hii natural.
Ndio maana ukishaoa hata kama ndio mpo mwaka wa Kwanza na bado vijana utakuta Mkeo anakushinikiza tujenge mapema kwaajili ya watoto wetu.
Tuanzishe miradi kwaajili ya watoto wetu
Ni jukumu letu kama wanaume au Wababa kutengeneza channel kwa watoto wetu. Huo ndio Ubaba wenyewe.
Taikon Master
Kwa sasa Dar es