Pre GE2025 Ni kauli ya Kishamba mno aliyotoa Chalamila, kuwa tarehe 24, majeshi yetu yote yatakuwa yanafanya usafi jijini!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwani mkiandamana na majeshi yakifanya usafi, shida ipo wapi nyie CHADEMA?

Mbona Chalamila hajawalalamikia CHADEMA kutangaza maandamano ila CHADEMA mnamlalamikia Chalamila kufanyia usafi Mkoa wake kwa msaada wa jeshi?

Pale Soko la Mabibo, Chalamila aliwahi kuleta wanajeshi wakafanya usafi huku biashara zikiendelea bila bugudha wala mikwaruzano.

Kwa hiyo CHADEMA ninawasihi sana nyie andamaneni tu msiogope, ila mkifanya fujo ninadhani zoezi la usafi litasitishwa kwa muda.
 
Ikionekana inafaa usafi unaweza kufanyika hata mwaka mzima.

Itakuwa vizuri maana hawana kazi za kufanya hao JWTZ. Waendee wakazibue chemba za maji taka majumbani.
 

Big brain. Umetoa hoja kubwa Sana.
 
Jeshi letu ni madhubuti sana na linawedi wa hali yajuu sana kwenye medani ya vita, sema tu tuna baadhi ya wanasiasa w ajabu ajabu. Wala tusiliaumu Jeshi hata kidogo Jeshi letu linaheshims kubwa sana Duniani.

Ni aibu sana kwa kauli ya Chalamila. Amelitumia jeshi Kama scapegoat.
 
Kama dhamira ni usafi basi Waaze leo na sio kusubiri mpaka TAREHE 28
Mbona CHADEMA walisubiri siku Samia kaenda Hanang na wao ndiyo wakafanya ziara the same day?

Hii ni michezo yao hao wanasiasa wanajuana wasitupotezee muda.
 

Chalamila kaingia kwenye mtego wa CHADEMA mapema Sana. Huwezi jua huo mtego wa CHADEMA una maana gani, yeye kaingia kichwa.
 
Mbona CHADEMA walisubiri siku Samia kaenda Hanang na wao ndiyo wakafanya ziara the same day?

Hii ni michezo yao hao wanasiasa wanajuana wasitupotezee muda.

Kwa hivyo unakubali JWTZ wanatumika kisiasa na CCM.
 
Magu keshaenda zake. Tusonge mbele. Chala hafai hata kuwa mkuu wa kata.
 
Duh!
 
Kwani chalamila kazuia msiandamane
Wanaolalama humu sio waandamanaji au tuseme wabongo waoga kuandamana kama kawaida yao ndio maana kuambiwa tu jeshi litafanya usafi siku hiyo basi teyari washaogopa.

Hakuna waandamanaji hapo.
 
Aliyekwambia USAFI unaingiliana na MAANDAMANO YA CHADEMA ni nani? Wao si waendelee na maandamano yao wakati usafi unafanyika Shida iko wap? ACHA UOGA
MIMI NIPO NA MAJESHI YETU KUFANYA USAFI
 
Reactions: Tui
Hayo ni yako dhamira ni kufanya usafi ili kujiepusha na magonjwa ya mlipuko kama vile kipindupindu.
Mnafanya usafi kwa matukio. Ndio maana magonjwa ya kipindupindu hayaishi. Issue ndogo TU ya usafi wa mazingira imeishinda serikali na wananchi kufanya kama utaratibu wa kila siku hadi kipindu×2 kije ndio tunajua kufanya usafi. KWA KWELI MWAFRIKA NA UCHAFU NI KAMA CHAI NA SUKARI
 
Mkuu nimeelewa nini unamaanisha .

Nikijulishe mkuu kuwa ukimuona nyani kariakoo basi ujue kuna aliye mleta Kariakoo.

Hiyo kauli haikutoka kwa bahati mbaya au karopoka.

Huyo ni waya wa spika tu
 
Hayo ni yako dhamira ni kufanya usafi ili kujiepusha na magonjwa ya mlipuko kama vile kipindupindu.
Ccm mmekuwa ni waoga sana kwa cdm na mnakuwa wa kwanza kukimbilia kwa wanajeshi.

Ila lazima mjue kuwa kuna siku hata hao wanajeshi watakataa huo usanii wenu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…