Ni kipi kilifanya Juma Nature kuwa spesho kuliko wasanii wengine wa kipindi chake?

Ni kipi kilifanya Juma Nature kuwa spesho kuliko wasanii wengine wa kipindi chake?

Miaka ya 90 mwishoni na 2000 mwanzoni kuliibuka vichwa hatari sana kwenye muziki wa Rap/Hiphop, hiki binafsi nakiona kama kizazi cha dhahabu kama ilivyokuwa timu ya Barcelona iliyomtetemesha SAF pale Wembley kwenye fainali za UEFA mwaka 2011.

Tukiachana na Records label nyingine, Ulikuwa ukienda tu pale Bongo Records kwa Majani utakutana na vichwa vikali kama Prof Jay, SoloThang, JayMo, Afande Sele, Ngwea, na wengine wengi, lakini pamoja na vichwa hivyo Sir Nature Kiroboto alikuwa treated kama mtoto mteule/mtoto mpendwa pale BongoRecords ama kwa jina jingine tunaweza muita 'The Special One', hata wasanii wenzake walilijua hilo kiasi cha kufikia kupeana maneno ya chinichini kwamba Majani anampendelea Nature, yaani Sir Nature akitaka kurekodi ngoma muda wowote ilikuwa ruksa, huku kina Fid Q wakipigwa danadana kwa zaidi ya miaka miwili.

Nadhani hii Majani hakuifanya kwa sababu ya urafiki wake na Nature tu, ni kwamba yeye kama mfanyabiashara alimuona ni mtu mwenye potential kubwa that's why akaamua kuinvest zaidi kwake, na kwakweli alifanikiwa maana show zote zilizowakutanisha wasanii wengi nilizofanikiwa kuzihudhuria enzi za 'uvulana' wangu kukiwepo jina la Juma Nature basi jua huyo ndie atakayefunga show, pamoja na vichwa kama Prof Jay kuwa na Hits kali, lakini wakikutana na Sir Nature kwenye show walikuwa wanasalimu amri tu hamna namna.

Je, ni kipi unadhani kilimfanya Sir Nature kuwa 'The Special One'? Ni zile Chorus zake kali? Flow yake? Sauti yake? Uswahili wake? Beat za Majani? Mashairi yake?[emoji2][emoji2][emoji2] Ila hapo kwenye lyrics namfananisha na mswahili mwenzake Inspector Haroun, siwezi muweka kwenye kundi la hao wakali hapo juu...View attachment 1483153
1. yuko real sana cz hta kwenye nyimbo zake huongelea vitu vya kitaa ambavyo tunaishi
2. mtaalamu wa kujiongeza (wewe mpe chorus ndio utamjua vizuri ) ana sauti zaidi ya tatu
3. anafanya aina tatu za mziki; bongo flave, hip hop na rap cartoon
4. hana maringo kuanzia kwa fans hadi kwa wasanii wenzake
5. ana NYOTA kali sana
 
No offence:
Mimi binafsi naonekanaga mpinzani
sikuwahi kuona ukali wake hata naonaga kawaida tu...Nature yuko overrated

Haujakosea. Muziki wa Juma Nature ulikuwa ni muziki wa kisela zaidi. Muziki wa kiume. Warembo wengi ule ulikuwa sio muziki wenu. Nyie enzi hizo mlikuwa mnamshobokea MB Dog, Lady Jay Dee na Mr. Paul.
 
Haujakosea. Muziki wa Juma Nature ulikuwa ni muziki wa kisela zaidi. Muziki wa kiume. Warembo wengi ule ulikuwa sio muziki wenu. Nyie enzi hizo mlikuwa mnamshobokea MB Dog, Lady Jay Dee na Mr. Paul.
Mkuu Tofautisha usela na mziki wa kiume
mbona mimi huyu nilikua shabiki wa Wana hiphop wengi sana wakina Langa /wateule nk nao walikua wanaonekana wagumu kipindi hicho, tatizo ni kutokua shabiki wa kitu anachoimba msanii.
Nature kwangu atabaki kuwa msanii wa kawaida tu kama wengine Akina Chege /Dully nk kwa sababu sikuwahi kuona kitu extra kwa upande wangu kwakweli.
 
1. yuko real sana cz hta kwenye nyimbo zake huongelea vitu vya kitaa ambavyo tunaishi
2. mtaalamu wa kujiongeza (wewe mpe chorus ndio utamjua vizuri ) ana sauti zaidi ya tatu
3. anafanya aina tatu za mziki; bongo flave, hip hop na rap cartoon
4. hana maringo kuanzia kwa fans hadi kwa wasanii wenzake
5. ana NYOTA kali sana
Namba 5 Hapa ndio sababu yenyewe
jamaa ana nyota tu
 
Mkuu Tofautisha usela na mziki wa kiume
mbona mimi huyu nilikua shabiki wa Wana hiphop wengi sana wakina Langa /wateule nk nao walikua wanaonekana wagumu kipindi hicho, tatizo ni kutokua shabiki wa kitu anachoimba msanii.
Nature kwangu atabaki kuwa msanii wa kawaida tu kama wengine Akina Chege /Dully nk kwa sababu sikuwahi kuona kitu extra kwa upande wangu kwakweli.
Hii nayo roho mbaya
 
Haujakosea. Muziki wa Juma Nature ulikuwa ni muziki wa kisela zaidi. Muziki wa kiume. Warembo wengi ule ulikuwa sio muziki wenu. Nyie enzi hizo mlikuwa mnamshobokea MB Dog, Lady Jay Dee na Mr. Paul.
Na Top In Dar
 
Ile pumzi na spidi ya ku rap.kwenye hili.game..hakuna msanii anayeweza kufanya vile kwa sasa..hawa kina joh makini anaimba maneno.mawili anahema ..necha alikua next level.. bana hebu sikiliza ile chorus ya niko gado.na zay b? Alivuta pumzi halafu akaachia then skiliza kilichofuata... stive b necha venture ni mafundi wa kukeshaaa halafu halafu anapiga kamluzi... mtu.mmoja mambo milioni.moja achana kbs na yule mndengereko... kingine necha alikuwa anaupenda tu muziki na alikuwa hafanyi kibishoo mpaka watu wanashangaa star mkubwa yupo simple namna ile.. necha akiwa star kbs alikuwa anatembea kwa miguu toka temeke mpaka kkoo..jamaa alikuwa wa kipekee yule.. na alikuwa yupo tayari kuimba na yoyote bila zengwe.. kifupi kwa tabia kama zile lazima uwe tu mtu wa watu
 
1. Anajua kuimba
2. Hardworker
3. Kiki
4. Wanawake
5. Good Performer (jukwaani)
6. Anajua watu wanataka nini kwa wakati gani
7. Collabos na wasanii wakubwa
Umetisha aisee!! nakubaliana na uliyoyaorodhesha hapo. Na mie cha kuongezea tu ni kwamba, jamaa pia yuko na "connections" sahihi za wadau wa muziki TZ.
 
Ile pumzi na spidi ya ku rap.kwenye hili.game..hakuna msanii anayeweza kufanya vile kwa sasa..hawa kina joh makini anaimba maneno.mawili anahema ..necha alikua next level.. bana hebu sikiliza ile chorus ya niko gado.na zay b? Alivuta pumzi halafu akaachia then skiliza kilichofuata... stive b necha venture ni mafundi wa kukeshaaa halafu halafu anapiga kamluzi... mtu.mmoja mambo milioni.moja achana kbs na yule mndengereko... kingine necha alikuwa anaupenda tu muziki na alikuwa hafanyi kibishoo mpaka watu wanashangaa star mkubwa yupo simple namna ile.. necha akiwa star kbs alikuwa anatembea kwa miguu toka temeke mpaka kkoo..jamaa alikuwa wa kipekee yule.. na alikuwa yupo tayari kuimba na yoyote bila zengwe.. kifupi kwa tabia kama zile lazima uwe tu mtu wa watu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mkuu Tofautisha usela na mziki wa kiume
mbona mimi huyu nilikua shabiki wa Wana hiphop wengi sana wakina Langa /wateule nk nao walikua wanaonekana wagumu kipindi hicho, tatizo ni kutokua shabiki wa kitu anachoimba msanii.
Nature kwangu atabaki kuwa msanii wa kawaida tu kama wengine Akina Chege /Dully nk kwa sababu sikuwahi kuona kitu extra kwa upande wangu kwakweli.
Taja wasanii wako watano (5) wa enzi hizo ambao uliokuwa unawakubali wewe.
 
Nakumbuka one day Mshua alinikuta nasikiliza "Hili Game" akaniuliza wimbo unahusu nini, nimtajie mistari miwili mitatu nikabaki 😳😳😳
 
Rap katuni style... iliyojikita zaidi kureflect maisha halisi ya watu wa hali ya chini na low life class ambao ndiyo walikuwa wengi zaidi kwenye bongo Flava fan base kwa wakati huo.

Mfano, East Coast Team wao walijikita kurepresent life style fulani ya kidown-town, waliimba maisha fulani ya 'ushuani' a.k.a mboga saba. That's why ilikuwa kukiwa na mpambano kati ya ECT na Sir Nature Kiroboto, ilikuwa ni lazima Kiroboto aibuke kinara!

Huwa siisahau mwaka 2003 siku tunazindua album ya UGALI by Sir Nature. Diamond Hall ilitapika!!! Moto ulikokwa stejini, fugo la chungu likatengwa, tukapakua ugali mixa mapochopocho manjari na nyanya masaro live bila chenga!! Mpishi mkuu P Funk Majani.

Live long Sir Kiroboto. 'Hili gemu' umelitoa far away.

-Kaveli-
 
Hawezi kueleweka Sasa hivi nchi ipo uchumi wa Kati upepo umeshabadilika na nyimbo ni za kiuchumi wa kati
Wakimpa promo kama analopewa leo Jide na Clouds anajaza uwanja vizuri tu, sema Nature sio kaliba ya wasanii wa kuperform Mlimani City, yeye ni huku kwa wananchi wa dola moja per day
 
Nature ana mistari adimu pia uwezo wake wa ku ghani mashairi, lazma ukimsikiliza utacheka tu maana anaimba kihuni huni na ana represent maisha ya uswahilini typical ambayo ndio yalikuwa maisha common kwa watu wengi kitambo kile.

Nadhani majani alikuwa anainjoy ile style ya rap katuni na wepesi wa Nature kuflow ukimpa beat. Ule uswahili uswahili wa nature na uhuni uhuni ile feeling itakuwa ilikuwa inamvunja mbavu sana bila shaka tofauti na wale wasanii waliokuwa wana rep ushua ushua ambayo ndo maisha ya P.Funk toka utotoni.
 
Haujakosea. Muziki wa Juma Nature ulikuwa ni muziki wa kisela zaidi. Muziki wa kiume. Warembo wengi ule ulikuwa sio muziki wenu. Nyie enzi hizo mlikuwa mnamshobokea MB Dog, Lady Jay Dee na Mr. Paul.
Ongezea unique sisters
 
Back
Top Bottom