Ni Kitu gani ushawahi kudanganya watu wanaokuzunguka kwa dhumuni la kujipatia kipato

Kifaru86

JF-Expert Member
Joined
Apr 22, 2017
Posts
1,734
Reaction score
3,822
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hebu hebu kila mmoja atoe ushuhuda ni Kitu gani alishawahi kudanganya watu wanaomzunguka kwa nia ya kujipatia kipato.

Mimi upande wangu niliwahi kudanganya nadaiwa ada enzi hizo nipo chuo kumbe napokea mkopo asilimia kama zote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kipindi life limenipiga nishawah danganya mi nimganga wa kienyeji na mdau wangu maeneo flani hivi tulikula kuku sana enzi za mkwere sio huyu jiwe


Baada ya kushtukiwa tulitafutwa kama wezi ni mwendo wa kukimbia tu




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Write your reply...nilidanganya ntamuoa binti yao na yule Dada alinielewa kwelikweli wakaniingiza kwenye baadhi ya kamati ya mchango kama msimamizi niliwaambia sina kitu baba mkwe akaniambia nisitoe chochote ni simamie matumiz ya michango kufanikisha ndoa nikaishia kukimbia na mchango nikawaacha kwenye mataa ila yule mzee alishikwa na kisukari ghafla ila nashkuru hali yake ikawa sawa


ila ule mkoa sirudi tena Mzee siraji kama unasoma hapa unisamehe tu mi ni yule kijana mwambie Aisha anisamehe pia kuwatafuta na simu siwez nimesajili laini mtanipata kiharaka maana nimeskia mlifungua kesi polisi mnisamehe tu nilikuwa sina kitu
 
mkoa wenyewe ni kigoma mkuu.
 
Ningeandika uwongo wangu hapa tatizo niliowadanganya wanapitaga humu hawachelew kuchukua kama ushaidi ila niliwapiga kama m30 hivi bila maumivu na mpaka leo hawajastukia mchezo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…