Ni kituko gani cha ugomvi ama ngumi hutokisahau?

Ni kituko gani cha ugomvi ama ngumi hutokisahau?

KENZY

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2015
Posts
32,529
Reaction score
76,691
Maisha yetu hupitia mengi ya maana na vituko ndani yake,tunaweza kushea vituko vya ugomvi tulivyopitia huko tulipotoka.. Binafsi mara ya mwisho kupigana ni enzi za ukindakinda huko japo si mtu wa ugomvi lakini inapobidi lazima Ni ukunje tupambane,bila kusahau pia kwenye mbio nipo vyema..😂

Nakumbuka darasa la tatu nilivamia mchezo usionihusu!,nilikuta mzozo kama Kuna hujuma imefanyika so mi nikaingia nauliza kiubabe lkn nilikuwa natania! Na aliekuwa akicheza alikuwa ni rafiki yangu so alipooana nimekuja kiubabe akaona huyu ndo mtetezi!!! Asalalee sijakaa vizuri yule aliekuwa anacheza huo mchezo ambae alikuwa ni mpinzani wa rafiki yangu nikaona anavua kibegi chake na shati tena huku akisapotiwa na rafiki zake!.. Sasa kijamaa kilikuwa kinaringia kifua kilikuwa kimejazia sijui kilikuwa kinafanyishwa mazoezi na Kaka zake..😅

Mara tukaachiwa uwanja,marafiki zangu wakataka nami nivue shati nikagoma nikawapa begi tu.. tukaupanga so wakati tumeupanga mi huku nishaharibikiwa kisaikolojia maana kijamaa walikuwa wanakisifu kina kifua na tumsuli so mpk tunaupanga ushindi ulikuwa umeelemea kwake!.. hapo komamanga mapigo ya moyo yanapiga kwa spidi isiyofahamika..!

Sasa kile kijamaa kilivyokishenzi sasa pamoja na yote hayo kiliyonayo kikaona hayatoshi wakati anakuja kunishambulia aliaanza kupiga mikelele kana kwamba anakuja kumaliza duh!.. ni kama vile muvi star sasa ndo anakuja kuuwa jambazi muvi iishe wakati ndo tunaanza!.. aisee zile kelele za kijamaa zilinifanya niogope zaidi mi nikaona haya yote yanini..? Kabla hajanifikia nikageuka nikala mbio za maana..😂

Aisee nilichekwa vibaya lkn kugeuka nyuma kijamaa kipo na bado kinapiga kelele huku kikinifata!.. baada ya mbio kadhaa kikaacha nilikuwa nimekizidi mbio kikasimama nami nikasimama so baada ya hapo hasira zikanishika Sasa nikakarudia bila kuangalia ubaunsa wala nini!.. nilikitwikwa mingumi mchezo ukaenda vyema walionicheka wakabadili gia,marafiki zangu nikawapa matumaini wakaanza kunishangilia.. nilipiga kile kibaunsa uchuro mpk kikalia..😂
Japo kilinikwangua na mikucha yake lkn hakikufua dafu..

Nashukuru niliivunja aibu na sifa zilitapakaa darasa kwangu mpk na madarasa mengine nikapata na mpambano mwengine!.. huo sitaki simulia maana nilikabwa kabali inaitwa "USIEMPENDA KAJA!!"😂😂 Ningekufa kama nisingesaidiwa kutoka pale vimtu vyengine kama vichawi tu..😂😂

Karibuni tushee kwa pamoja walau tucheke tuongeze siku za kuishi..
 
Ninachokumbuka kipindi nipo shule, kila mwaka nilikuwa ni lazima nipigane na rekodi yangu miaka yote nilishinda. Katika mpambano mmoja tu mpinzani wangu alinipiga chupa ya kichwa na kunimaliza nguvu! Lakini ushindi hakuupata kwa vile ye mwenyewe baada ya kufanya vile alikimbia kwakuwa ilikuwa ni kinyume na mchezo.
Rekodi yangu ni nzuri sana kwani nimeshinda mapambano kwa miaka yote na nimedroo mara moja tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chengine nilimtukana rafiki yangu tusi zito kinyama huku nikijihami huyu mbio haniwezi!.. na hapo nafahamu kabisa kwenye ngumi simuwezi.. jamaa akaanza nifukuza mi nikaona hiyo ligi ndogo tu tukakontonza vya kutosha.. Sasa kila nikiangalia nyuma kijamaa kipo isipokuwa matumaini ya kunipata ndo hakuna!…Sasa ubovu ukawa kwangu uelekeo niliokuwa nimekamata ilikuwa ni uelekeo wa nyumbani!!..

Nikifikiria jamaa nimemtukana tusi zito Sasa nikikimbila nyumbani si ataenda kusema huyu mi nitiwe mi mboko ya maana!.. nikaona isiwe tabu nikasitisha mbio nikakaa chini kijamaa kikaja kikanipiga mateke ya maana nilipigika bila hata kujitetea alivyoona imetosha akaniacha nikarudi zangu nyumbani mapema tena walishangaa kuwahi kurudi ilikuwa jioni nikaingiza Bata bandani nikaoga nikatuliza mshono.. skani hawakujua kilichojiri maana sikuwa na kovu wala nunge.. ila nilikoma ndo nikajua "Mwana kulitaka ndie mwana kulipata"
 
Ninachokumbuka kipindi nipo shule, kila mwaka nilikuwa ni lazima nipigane na rekodi yangu miaka yote nilishinda. Katika mpambano mmoja tu mpinzani wangu alinipiga chupa ya kichwa na kunimaliza nguvu! Lakini ushindi hakuupata kwa vile ye mwenyewe baada ya kufanya vile alikimbia kwakuwa ilikuwa ni kinyume na mchezo.
Rekodi yangu ni nzuri sana kwani nimeshinda mapambano kwa miaka yote na nimedroo mara moja tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu wengine tuna uoga lkn nilikuwa nashangaa sometimes nikiushinda nikaamua kupigana nilikuwa nashinda vizuri tu.. nilishawahi pata sifa mtaani ilikuwa ni kwa rafiki yangu na dada zake walikuwepo Sasa tulikuwa tunacheza karata kuna jamaa akaanza kuniletea maneno ya shombo nikamvumilia lkn haichi dadeki nikaweka karata pembeni.. nilimtapakaza ngumi halafu yule rafiki yangu ambae tunapopigania ndio kwao akawa anasema "Waacheni"😂 Jamaa alitaka kuanza hadi kulia ndo wakatuamua ila baada ya ugomvi kuisha nilipata ujiko haswa kwa wadada wa rafiki yangu walikuwa furu shangwe,hawakuamini ngumi nilizozitoa mpk wakawa wanaigiza nilivyokuwa nikimtwanga jamaa..😂
Bahati yao walikuwa wananizidi umri alasivyo ningebeba mmoja maana si kwa kusifia kule..😜
 
Kwa ambao hatuna wako kupigana tu nakaa kimya au??
😂 Chakorii ulivyomkorofi huwezi kukosa ugomvi wewe! We sema ulitolewa meno mangapi kwani Kuna mtu atakumeza hapa...😜
 
😂 Chakorii ulivyomkorofi huwezi kukosa ugomvi wewe! We sema ulitolewa meno mangapi kwani Kuna mtu atakumeza hapa...😜
Kwa mbaaaaali...naona kuna mtu anatafuta timbwili la asha ngedere.🤪
 
Mkuu wengine tuna uoga lkn nilikuwa nashangaa sometimes nikiushinda nikaamua kupigana nilikuwa nashinda vizuri tu.. nilishawahi pata sifa mtaani ilikuwa ni kwa rafiki yangu na dada zake walikuwepo Sasa tulikuwa tunacheza karata kuna jamaa akaanza kuniletea maneno ya shombo nikamvumilia lkn haichi dadeki nikaweka karata pembeni.. nilimtapakaza ngumi halafu yule rafiki yangu ambae tunapopigania ndio kwao akawa anasema "Waacheni"[emoji23] Jamaa alitaka kuanza hadi kulia ndo wakatuamua ila baada ya ugomvi kuisha nilipata ujiko haswa kwa wadada wa rafiki yangu walikuwa furu shangwe,hawakuamini ngumi nilizozitoa mpk wakawa wanaigiza nilivyokuwa nikimtwanga jamaa..[emoji23]
Bahati yao walikuwa wananizidi umri alasivyo ningebeba mmoja maana si kwa kusifia kule..[emoji12]
Uoga ni ugonjwa hatari sana, nishawahi kupigwa kwa kuchangiwa hadi marafiki zangu wakaja huku nikiwa niko hoi, ila tuliendeleza mapigano hadi wapinzani wakasalimu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
😂😂 Dada sema ukweli tu usikimbilie self defense za vitisho..
Achana na story za miaka hiyo ya MEMKWA blaza..
Chakorii wa shule ya vidude si huyu kijana...
Kuwa makini sana lisije likakukuta tukio kaka mkubwa😆😆😆😆😆
 
Achana na story za miaka hiyo ya MEMKWA blaza..
Chakorii wa shule ya vidude si huyu kijana...
Kuwa makini sana lisije likakukuta tukio kaka mkubwa😆😆😆😆😆
Nyie ndo mnaopigwagwa mpk maji mnaita mma..😅

Kuna siku jirani kuna rafiki yangu nilikuta amamshughulikia ndugu yake wa kutoka kijijini huko jamaa kashikilia na mwiko kabisa anamnyunda hata sijauliza kisa nini namkuta jamaa anamuuliza kwa machungu "Yani unaniita mimi mchawi Mimi..?!!"😂😂 Badala ya kuamua ugomvi ikabidi nianze kucheka tu maana alieitwa mchawi hata hafananii sijui nae aliemuita hivyo hakuona jamaa anafanana na jambazi au alitumia tafsida..😂 Jamaa ilimuuma sana kuitwa mchawi..😅
 
Nyie ndo mnaopigwagwa mpk maji mnaita mma..😅

Kuna siku jirani kuna rafiki yangu nilikuta amamshughulikia ndugu yake wa kutoka kijijini huko jamaa kashikilia na mwiko kabisa anamnyunda hata sijauliza kisa nini namkuta jamaa anamuuliza kwa machungu "Yani unaniita mimi mchawi Mimi..?!!"😂😂 Badala ya kuamua ugomvi ikabidi nianze kucheka tu maana alieitwa mchawi hata hafananii sijui nae aliemuita hivyo hakuona jamaa anafanana na jambazi au alitumia tafsida..😂 Jamaa ilimuuma sana kuitwa mchawi..😅
Chizi kabisa wewe😆😆😆mfano gani sasa huo....kwendraaaaaa
 
Chizi kabisa wewe😆😆😆mfano gani sasa huo....kwendraaaaaa
Nakwenda ila nasubiri siku uje upate msala utaniita tu kuja kutoa msaada na vile hujui hata kurusha ngumi unajua kuuma tu! 😂
Sijui Sana..😅
 
Nakwenda ila nasubiri siku uje upate msala utaniita tu kuja kutoa msaada na vile hujui hata kurusha ngumi unajua kuuma tu! 😂
Sijui Sana..😅
Mimi na ugomvi ni vitu viwili tofauti blaza..
Ni sawa na mafuta na maji..najitenga kabisaaa...sasa usitegemee nipate msala bulaza
 
Enzi hizo primary tunapigana darasa na darasa kila siku tukitolewa mapumzko tu, sasa kuna kitoto kimoja kinajifanya kibabe sana akiniona anataka tupigane daily yule mtoto nilkua simuwezi sasa kuna day nisharudi mapumzko naenda darasani namkuta yupo ktk mti wa mchungwa ananisubiri , mm nikasema ndo hapa hapa nikaokota jiwe na kumpiga nalo la kichwa.

Ghafla namuona mtu kaanguka chini na kuanza kulia, nilivo ona vile nikasema huu ushakua msala sasa nikaingia darasani na kubeba begi yangu na kutoroka mpaka home.

Tangu siku hio ikawa heshima
 
Kipindi Niko la tano!Kuna bro alikuwa anapenda kunionea Sanaa akikutana na Mimi makwezii dah!alafu mbaya zaidi alikuwa anachukua dada anguu siku moja Niko na nunua mandazi kwa mama aminaa....jamaa Kama kawaida akanitandika bongee la konziii ile kushuka chini kuamka nikaa amkaa na karai la mandazi na kimwagiaaa....jamaa aliliaa vibaya na alikwivyaa na mafutaa....dah yani Hadi leo nikimuonaa nimemtengenezea kilemaa Cha kudumu
 
Back
Top Bottom