Ni kosa gani alilolifanya Aboud Jumbe kustahili 'kifungo cha maisha'?

Ni kosa gani alilolifanya Aboud Jumbe kustahili 'kifungo cha maisha'?

Kwanza naomba tuheshimiane,

Mie ni mtanganyika pure born and bread huwezi kunitoa Tanganyika maana nimezaliwa tanganyika wazazi wangu watangayika huna vya kunibadilisha. Kama nilivyosema katika post zangu wazanzibar nimekaa nao na kwakweli nawasupport wanalolifanya kwani ukoloni mamboleo uliofanywa na Tanganyika mnajifanya hamuufahamu ni bora mkaufahamu vizuri sana. Labda nikuulize wewe je wazanzibari sio watanzania?

Wewe ni mzanzibari uliyejivika kofia ya "utanganyika!" Hata kauli zako zenye chuki zinaonesha! Pia hakuna ukoloni wowote uliofanywa kwa Wazenj na Watz! Wanaajiriwa tu kwenye Wizara ambazo si za Muungano, hebu tuambie mtanganyika yeyote aliyewahi kuajiriwa na SMZ!
 
Hebu tuelezee maana yake unaonyesha kulishupalia hili, ulinzi wa kiongozi maana yake nini kama utawakuta walinzi halafu upite tu bila kuhojiwa.

Mie niliwahi kusikia kutoka kwa mtu aliwahi kupita pale ilikuwa kama umepita kambi ya jeshi na unasema yule ni kiongozi but tunapafahamu kwa Mwinyi na mkapa watu wanaishi nao majirani na hakuna no fly zone kama kwa huyu mzee Jumbe utafikiri ulikuwa unapita kambi ya jeshi kule Arusha. Walikuja kuregeza masharti wakati wa mkapa but before the former president ilikuwa kama no fly zone kuenda kwa mzee huyu.
 
What is excatly the title of that book? and where can I possibly find?

Mkuu siko karibu na computer yangu sasa hivi ila kitabu chake kinaitwa The Partnership kitafute nikirudi June mwaka huu naweza kukipost ila unaweza kukisaka vilevile online kama kipo ukakisoma.
 
anaejua ukweli wa alichofanya mzee huyu aweke hapa ili tupime mapungufu ya baba wa Taifa, kwani hata yeye mwenyewe alikiri kua kamabinadam woote walivyo ana mazuri na mabaya yake ila tuige na kuyaenzi mazuri sasa wajibu wetu kuyajua mabaya yake pia
 
Wewe ni mzanzibari uliyejivika kofia ya "utanganyika!" Hata kauli zako zenye chuki zinaonesha! Pia hakuna ukoloni wowote uliofanywa kwa Wazenj na Watz! Wanaajiriwa tu kwenye Wizara ambazo si za Muungano, hebu tuambie mtanganyika yeyote aliyewahi kuajiriwa na SMZ!

Mkuu pitia katika Profile niliwahi kusema karibia miaka miwili nyuma sababu kwanini nawatetea wazanzibari, kwanza historia tuliyoisoma madarasani wakati Nyerere nilikuja kukuta ni tofauti nilipokuwa zanzibar kikazi nikawa nasoma vitabu vya historia kutoka kwa waandishi waliokuwa zanzibar. Nachokushauri kavisome na wewe utawaunga mkono hawa ndugu zetu waswahili wana msemo wanasema jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza. Kama hupendi unapenda huo ni msimamo wangu nitawatetea hawa ndugu zetu.
 
Mie niliwahi kusikia kutoka kwa mtu aliwahi kupita pale ilikuwa kama umepita kambi ya jeshi na unasema yule ni kiongozi but tunapafahamu kwa Mwinyi na mkapa watu wanaishi nao majirani na hakuna no fly zone kama kwa huyu mzee Jumbe utafikiri ulikuwa unapita kambi ya jeshi kule Arusha. Walikuja kuregeza masharti wakati wa mkapa but before the former president ilikuwa kama no fly zone kuenda kwa mzee huyu.

Yawezekana umechanganya mambo, ulinzi wa enzi za Mwl JK ulikuwa lazima uongezewe uzibiti kwa kuwa tulikuwa na maadui wengi, mambo kama cold war, makaburu etc. Huoni kama maadui wetu wa enzi hizo wangeweza muua Jumbe halfu wautumie kama mtaji wa kuidhoofisha serikali. Kwa mtazamo wako wewe nani wanafaidi zaidi matunda ya muungano znz au tanganyika angalia wakati uliopo, na toa maoni kwa thati ya moyo wako si unafiki. Fanya hivyo kama utapenda si kulazimishi.
 
Tunapenda kusahau ukweli kuwa kikulacho ki nguoni mwako....mbona hakuna mtu wa pande ya pili anayemzungumzia Abood Jumbe? Inamaana ni Nyerere tu ndiye aliyekuwa sababu la anguko lake na siyo wanasiasa wengine wa Zenj!
 
Kwanza naomba tuheshimiane,

Mie ni mtanganyika pure born and bread huwezi kunitoa Tanganyika maana nimezaliwa tanganyika wazazi wangu watangayika huna vya kunibadilisha. Kama nilivyosema katika post zangu wazanzibar nimekaa nao na kwakweli nawasupport wanalolifanya kwani ukoloni mamboleo uliofanywa na Tanganyika mnajifanya hamuufahamu ni bora mkaufahamu vizuri sana. Labda nikuulize wewe je wazanzibari sio watanzania?

Sawa mkate!

Amandla.......
 
Mie niliwahi kusikia kutoka kwa mtu aliwahi kupita pale ilikuwa kama umepita kambi ya jeshi na unasema yule ni kiongozi but tunapafahamu kwa Mwinyi na mkapa watu wanaishi nao majirani na hakuna no fly zone kama kwa huyu mzee Jumbe utafikiri ulikuwa unapita kambi ya jeshi kule Arusha. Walikuja kuregeza masharti wakati wa mkapa but before the former president ilikuwa kama no fly zone kuenda kwa mzee huyu.

Kumbe hata mzanzibari mwenzake alimminyia? Bado mnamlaumu Nyerere! Kweli hamna maana!

Amandla......
 
Hoja yako naiunga mkono kwa saana tu.

Hakika kosa linodaiwa kufanya kumfanya huyu mzee wetu atumikikie jela maisha yote bila hata kukum bukwa kwenye PAROLE ya raisi siku za sikuku si kwamba labda alikwiba cha mtu wala kutenda kosa la kubaka oisipokua tu ni kwamba alidiriki kutenda kosa la KUENDEKEZA MAWAZO YA KIKATIBAKATIBA HIVI kwa enzi hizo ikawa taabu.

Na wala sitoshangaa endapo alichokiamini miaka hiyo kutumia mfumo wa serikali ya shirikisho kama ambavyo inavyotumika hivi sasa Marekani ikaja ikaonekana kuwa ni suluhisho bora zaidi wa namna ya kuboresha serikali kati ya bara na visiwani!!!

Na kwa sababu huyu 'mzee muona mbali' alidiriki tu kutenda kosa la kimawazo ambalo leo hii sisi wajukuu zake 'kosa' hilo hilo ndilo limekua wimbo mojawapo wa aina ya mabadiliko tunayotakataka kuona hapa chini ambao pengine huenda hata ikatuvuruga kabisa na baadhi ya wale ving'ang'anizi wenye fikra mgando wa mwaka wa 47, mie naona bora babu aachiwe huru mara moja, jeshi imjengee nyumba mahala atakapochagua na kupewa haki zake zote kwa utumishi uliotukuka kuliko kodi zetu zilazimishwe kuifanyia malipo kampuni za kitapeli kama Dowans.

Kwa kweli kwa uchungu mkubwa sana nami nimekua nikijiuliza mno kila ninapomuona huyu mzee wetu akisuguana bega na vibaka pale kwenye MV Alina akijikokota kwa shida kweli kweli na ligari la zamaniiii rangi ya krimu manjano hivi kila anapotoka au kurejea kule kifungoni kwake naanihii , si kule Robben Islandi; aggrr, samahani kule Kigamboni.

Hofu yangu tu ni kwamba kwa kuwa kule Pemba alizuiliwa kufika tangu zamani sana, leo hii ambapo kuna umeme mote huko alikozaliwa Pemba akirudi leo hii hatopotea kabisa vijiji?? Nyumbani jaamae, nyumbani kutamu hata kama ni misitu tuu!!

Je, endapo mtu yeyote mwenye dhamana atasikia sauti zetu dhaifu hizi lakini zenye nguvu kisirisiri, yule Mzee wetu MSTAARABU PEKEE WA SIASA NCHINI TANZANIA, Dr Ali Mohammed Shein, walau atajitolea vyombo vya usafiri wa aina zote kupereka ziarani hadi kule penye kilimo baharini huyu mzee wetu kuliko tu wanasiasa kuja kummiminia sifa za kinafiki baada mara baada ya kumsogelea muumba wake?

Je, Mwamnyanye ataona busara ozote kwenda na vijana wake kwenda kumjenge huyu mzee wetu mji kule Pemba kama ambavyo walivyomfanyia Mwalimu Nyerere kule Butiama badala ya kuja tu kusubiri mamba yaharibike kwa mzee wetu ndio waende KUPIGIA MIZINGA YA 'HESHIMA' kaburi???

Taifa letu linafuatilia kwa kiasi gani ustawi mzuri wa familia za wazee wetu wa bara na visiwani waliotutumikia hadi kuondoka ofisini bila KASHFA ZA UFISADI??? Wengi wao tunawaona mijini nyuso zao zikililia taifa hili KILAANA KABISA na hata kutoa taswira kama vile 'UADILIFU WANGU WA KUPIDUKIA KUTUMIKIA TAIFA LANGU NDILO LIMENIFIKISHA HAPA.

Mama yetu Anna Makinda, hebu iwekeni vizuri swala hili huko bungeni ili kodi zetu kuwasaidia waliotutumikia KIUADILIFU kusiwafikie tu kama hisani hisani vile. Mama nili ulimtembelea Prof Apiyo kwa mara ya mwisho? Mama Hawa Ngulume je, Banduka wako wapi na wanaongoza maisha ya aina gani, Joseph Rwegasira, Bob Makani, Edwin Mtei, Mama Shirima, Wazee wa Afrika Mashariki, familia ya Moses Mnauye, Bibi Titi, Mwalimu Nyerere, Dr Slaa, Chifu Mkwawa na wengine wengi tu??

Mama mbali na kazi bungeni tunataka kuona sura ya umama kweli na wakati wopte bila ubaguzi katika initiatives za kuyashughulikia haya.
 
Kumbe hata mzanzibari mwenzake alimminyia? Bado mnamlaumu Nyerere! Kweli hamna maana!

Amandla......

Kwani nani aliyemrithi Aboud Jumbe alipoondoshwa madarakani? Unadhani kwanini Mwinyi aliwekwa pale baada ya Aboud Jumbe na Nyerere? Sasa unadhani atakuja kubadilisha maamuzi ya aliyemweka madarakani?
 
Kwa kweli kuna mambo mengi ya kihistoria katika nchi yetu ambayo hatuyajui.....
 
Kwani nani aliyemrithi Aboud Jumbe alipoondoshwa madarakani? Unadhani kwanini Mwinyi aliwekwa pale baada ya Aboud Jumbe na Nyerere? Sasa unadhani atakuja kubadilisha maamuzi ya aliyemweka madarakani?

Mbona Mkapa aliweza? Yeye si alifanyiwa hata kampeni na Nyerere? Unafik, tu, mkuu. Hakuwa amefungwa ndiyo maana Mwinyi hakuona sababu ya kumuachia!

Ukweli ni kuwa wazanzibari wamekuwa wakipewa hifadhi bara kuanzia Sultan Sayyid Sir Jamshid bin Abdullah Al Said, Babu, Aboud Jumbe na wengine pale wanapokosana na wenzao.

Amandla......
 
JokaKuu,
Mkuu umekuwa mkali sana siku hizi kwa hawa wazanzibari.

Mimi nafikiri wako hapa Tanganyika kwa sababu kuu ya muungano.
Lakini katika makala moja ulishauri ulipotoa rai ya kuvunja muungano, kuwa kwa udugu uliopo tokea enzi wa Watanganyika na wazanzibari basi hata ikitokea muungano kuvunjika ulishauri watu wapewe fursa ya kuchagua uraia au umeshasahau mkuu.

Lakini pia kama unafuatilia historia za marais wa zenj wanachaguliwa bara na Mzee Jumbe na Ali Mwinyi ni wazaliwa wa Tanganyika.marais wazanzibari ambao kilugha unaweza kusema wazawa ni Marehemu Idrisa Abdul Wakil na Salmini Amour,
Hata karume alitokea Malawi. Hii haiwaondoshei kuwa wao ni watanzania na wazanzibari pia.

Lakini pia kama utapitia historia vizuri, mwambao wa pwani kwa kilomita kumi kutoka Kenya hadi Msumbiji ilikuwa Zanzibar.

Kwa kauli hizi kali za kuhoji hawa wazanzibari wanaoishi Dar, jee kuna tofauti gani na mtu anaetokea Arusha, Mbeya kwa mamtiki yako Dar ni ya Wazaramo na watu wa Pwani.

Nafikiri kauli ya Mwalimu kuhusu ubaguzi inafaa kuzingatiwa, itatutafuna.
Wazaramo wakisema wachaga na wote wenyeji wote wasio wa mwambao wahame Dar, patakalika hapo?
 
Mbona Mkapa aliweza? Yeye si alifanyiwa hata kampeni na Nyerere? Unafik, tu, mkuu. Hakuwa amefungwa ndiyo maana Mwinyi hakuona sababu ya kumuachia!

Ukweli ni kuwa wazanzibari wamekuwa wakipewa hifadhi bara kuanzia Sultan Sayyid Sir Jamshid bin Abdullah Al Said, Babu, Aboud Jumbe na wengine pale wanapokosana na wenzao.

Amandla......

Fundi Mchundo,

Tuseme uko sahihi sasa vp inakuwa wazanzibar wanamlilia halafu yeye aogope au kukataa kuja kuishi zanzibar wakati alikuwa Rais wa Zanzibar??
 
JokaKuu,
Mkuu umekuwa mkali sana siku hizi kwa hawa wazanzibari.

Mimi nafikiri wako hapa Tanganyika kwa sababu kuu ya muungano.
Lakini katika makala moja ulishauri ulipotoa rai ya kuvunja muungano, kuwa kwa udugu uliopo tokea enzi wa Watanganyika na wazanzibari basi hata ikitokea muungano kuvunjika ulishauri watu wapewe fursa ya kuchagua uraia au umeshasahau mkuu.

Lakini pia kama unafuatilia historia za marais wa zenj wanachaguliwa bara na Mzee Jumbe na Ali Mwinyi ni wazaliwa wa Tanganyika.marais wazanzibari ambao kilugha unaweza kusema wazawa ni Marehemu Idrisa Abdul Wakil na Salmini Amour,
Hata karume alitokea Malawi. Hii haiwaondoshei kuwa wao ni watanzania na wazanzibari pia.

Lakini pia kama utapitia historia vizuri, mwambao wa pwani kwa kilomita kumi kutoka Kenya hadi Msumbiji ilikuwa Zanzibar.

Kwa kauli hizi kali za kuhoji hawa wazanzibari wanaoishi Dar, jee kuna tofauti gani na mtu anaetokea Arusha, Mbeya kwa mamtiki yako Dar ni ya Wazaramo na watu wa Pwani.

Nafikiri kauli ya Mwalimu kuhusu ubaguzi inafaa kuzingatiwa, itatutafuna.
Wazaramo wakisema wachaga na wote wenyeji wote wasio wa mwambao wahame Dar, patakalika hapo?

Ebu fafanua hapo kwenye Nyekundu, mwaka gani hiyo Historia, Maana tokoea hii mipaka ya Africa iwekwe haijawai kubadilishwa au una-undugu na Museveni wa Uganda anaye dai kisiwa cha Kenya kuwa chake.
 
Back
Top Bottom