Wakuu, naomba kufahamishwa ni kosa kuwapiga picha askari wakiwa kazini kwa mtu ambaye si mwandishi wa habari? Naomba kujuzwa kama ni kosa sheria inasemaje? Mfano wakati wanamkamata mwizi mtaani, wakituliza vurugu nk. Watu wengi hupenda kupiga picha wakati wa matukio ambazo mara nyingi hawana matumizi nazo zaidi ya laisure au kuweza kuwaonesha rafiki zao badae, askari wanakua wakali sana pindi wapigwapo picha wakiwa wanatekeleza majukumu yao Naomba kuwasilisha.