Ni kujichanganya kama unapenda nchi lakini hupendi Katiba mpya wala Demokrasia

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
7,823
Reaction score
10,857
Ni kujichanganya kama unapenda nchi lakini hupendi katiba mpya wala demokrasia. Kwa wale wanaosema wanapenda nchi ni wazalendo lakini hawataki katiba ambayo itasaidia nchi yetu kuwa nchi bora zaidi.

Lakini cha ajabu hawataki Watanzania wengine wawe na Uhuru na Demokrasia. Sasa ni kweli watu wa hivi wanapenda nchi au wanajali maslahi yao tu. Wale watu ambao wanajali nchi bila kuweka maslahi binafsi ndiyo wazalendo wa kweli sio machawa au hawa ambao wanatetea vitu vya kuwasaidia wenyewe tu.

Sasa kwa wale ambao hamtaki Katiba mpya wala Demokrasia je mnazuia na kupinga kwa maslahi ya naini hasa.

Soma Pia: Bila katiba mpya nzuri, wawekezaji watatukimbia!
 
Je, unaifahamu misingi ya Itikadi ya Tawala za Kikomunisti/Ujamaa??

Ukomunisti/ujamaa ni unyama kama siyo ushetani kabisa.
 
Tatizo la Tanzania kuna vigogo wengi sana wa juu ambao ni walaji na wala rushwa. Huu utamaduni hauwezi kupenda wazalendo ambao wanapenda haki na kupinga rushwa. Yaani wanataka ndugu zao na maslahi yao ya kirushwa yasichunguzwe.

Tatizo ni kwamba hawa vigogo ni wengi sana. CP Salum Rashid Hamduni ameshidwa kazi maana alikuwa anahujumiwa na hao hao maboss wake! Yaani wanataka naye awe fisadi au wanatafuta njia ya kumtoa. Rushwa ikiendelea pia tatizo lote ni kwake, akifanya kazi vizuri na kutojali maboss amashushwa cheo!!!! sasa ni ngumu sana kuwa mzalendo serikalini




 
Kweli kabisa hata Jerry Silaa naye amelipwa kichwa

Hata Makonda kaminywa hutamsikia kutetea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…