Ni kwanini maeneo mengi ya mijini nchini yanakaliwa sana wamanyema kuliko wenyeji wa mikoa hiyo

Sijawahi kuona wamanyema bukoba na wala siwajui pamoja na kuishi bukoba.mjini Kati kuna wahindi na waarabu wengi na wahaya wamejaa tena Sana ndo maana kihaya kinaongeleka Sana mjini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuichunguza sana hao wanaojiita wamanyema ni wale ambao hawana utambulisho, wengi hawawajui baba wazazi wao hivyo kukosa asili, kichaka cha huwa ni kujiita wamanyema
 
Mleta mada hakuwa na maana ya kupotea lugha za asili za maeneo husika nadhani alimaanisha ongezeko la wamanyema Kila Kona ya Tanzania hata Mimi ni mhaya naamini tunathamini lugha yetu ya asili Kama yalivyo makabila mengine

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Moshi hao Wamanyema hawawezi fika hata 10 na wote lazima wawe wamachinga. Kuna miji huwez kusurvive kama sio mwenyeji
 
Hapana, hutujui, Wamanyema si Wabembe, usiwe kama hujasoma historia ya Tanzania, Hivi ukiskia Sheikh Amri Abeid Karuta, Sheikh Yahya Hussein, Sheikh Ramiya wa Bagamoyo, Idd Faiz, Idd Tosiri ambao wote ni wanachama wa mwanzo wa TANU walikuwa kabila gani kama si Wamanyema?, tena hilo linajulikana.
Wamanyema kwa kukufahamisha ni jamii iliyozaliwa kwa muunganiko wa makabila ya asili ya mashariki ya Congo huku Tanzania ambao nyumbani kwao hasa ni Kigoma-ujiji, jamii hizo ya kwanza kabisa kukanyaga Kigoma mjini ni Wagoma na ndo inasemekana paliitwa hivyo kwa jina Lao, Jamii zingine zilizounda Wamanyema ni; Wabwari, Wanyakaramba, Wakusu, Waruwa, Wasongye, Wabangubangu na Wabembe Wanyang'nja.
Sasa hao Wabembe unaowasema wa juzijuzi ni jamii inayojitegemea na huzungumza lugha ya kibembe na hutokea Wilaya ya Uvinza(Tongwe/Kigoma kusini) na si kigoma-ujiji.
Pia katika Wamanyema kwa zaidi ya 50% wengi ni wa asili ya wazoba(Wagoma na Wabwari) na wengine ndiyo Wakusu, Waruwa , Wabangubangu jumlisha Kariba zingine zaidi ya 15 ambazo ni mbali kiasili na Wabembe, sasa huwezi sema Wamanyema ni Wabembe.
 
Kwa akili hizi CCM itaendelea kudumu madarakani.
 
Uongo uongo kama huu umemsababishia boss wangu wa zamani bwana Kingwangala kuukosa uprofesa hivi hivi akiwa anaona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…