Ni kwanini Serikali ya awamu ya tano inatumia propaganda ya kuminya Demokrasia katika kivuli cha kuleta maendeleo?

Ni kwanini Serikali ya awamu ya tano inatumia propaganda ya kuminya Demokrasia katika kivuli cha kuleta maendeleo?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Tumekuwa tukiwasikia sana watetezi wa utawala huu wa awamu ya tano wakitetea sana uminyaji wa demokrasia unaofanywa na serikali hiyo kuwa ni sahihi kwa madai ya kutumia kivuli cha kuleta maendeleo ya nchi hii.

Mifano mikubwa wanayotoa hao watetezi wao ni kasi ya maendeleo wanayodai inafanywa na watawala wa serikali hii, kama vile ujenzi wa reli ya SGR, ujenzi wa bwawa la umeme la Stiegler's Gorge na ununuzi wa ndege za Bombardier unaofanywa na serikali hii.

Nipende kuwauliza hao watetezi wa awamu hii kuwa hivi kama kweli wanaamini kuwa serikali hii inawafanyia maendekeo makubwa wananchi wake, ambapo hakuna mwananchi asiyeyaona, si wangeacha wananchi wenyewe waamue kuchagua viongozi wao wanaowataka kupitia sanduku la kura katika uchaguzi ulio huru na wa haki?

Mfano halisi ni namna serkaki hii ya awamu ya tano kwa namna ilivyouviruga uchaguzi uliopita wa serikali za mitaa, ambapo vyama 8, kikiwemo chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema kulazimika kujitoa katika kinyang'anyiro hicho.

Kama wanachoongea ni kweli kuwa hata kipofu anayaona maendeleo yanayofanywa na serikali hii ya awamu ya tano, iweje sasa serikali hii hii iogope kupita kiasi kufanya chaguzi zilizo huru na haki?

Hivi ni kwanini hawawachi wananchi wenyewe ndiyo wachambue mchele na pumba?

Ni kwanini basi watawala ndiyo wanaowachagulia wananchi viongozi wao wanaowawakilisha?

Hivi tukiangalia kwenye nchi za wenzetu zilizoemdelea kama vile Taifa kubwa kiuchumi duniani la Marekani, ni kwanini wao hawaminyi demokrasia na badala yake wanahimiza izidi kupanuliwa?

Na hizi propaganda zao hawa CCM kuwa Maendeleo hayawezi kuja nchini kwa kuimarisha demokrasia ni mawazo potofu sana.

Huu mfumo waliouchàgua hawa CCM wa kurejea kwa nguvu kwa mfumo wa chama kimoja ni mfumo wa kidekteta na ambao utatuletea machafuko nchini kwetu na ni mfumo unaovunja kwa makusudi mfumo ulioanishwa ndani ya Katiba ya Jamburi ya muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 3(1) ambayo nainukuu "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itafuata mfumo wa kidemokrasia na ni nchi yenye mfumo wa vyama vingi" mwisho wa kunukuu.

Nakaribisha maoni yenye maslahi mapana na itakayoonyesha dira ya mustakabali mwema wa taifa letu.
 
Magufuli ameishiwa mbinu, na Wala hana team ya watu competent
Kwa mbinu hizi za kitoto kabisa anazotumia, natabiri kuwa atafika mahali, ni lazima ata-surrender!
 
Magufuli ameishiwa mbinu, na Wala hana team ya watu competent
Ningependa kumuuliza Magufuli na wale "Praise and worship team for Magufuli" hivi haya maendeleo ya nchi yetu yaliyoletwa na viongozi wa awamu zillizopita, wao wamefumba macho na hawayaoni??
 
Ningependa kumuuliza Magufuli na wale "Praise and worship team for Magufuli" hivi haya maendeleo ya nchi yetu yaliyoletwa na viongozi wa awamu zillizopita, wao wamefumba macho na hawayaoni??

Matendo ya Mitume 12

21 Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao.
22 Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu.
23 Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho.
 
Hivi katika bara hili la Afrika kuna nchi inayoizidi Afrika Kusini kwa maendeleo ya miundo mbinu??

Mbona dunia nzima iliwatenga enzi zile za ukaburu na uminywaji wa demokrasia??

Ni lazima watawala wetu wafahamu umuhimu wa wananchi wake kuwachagua viongozi wanaowataka wenyewe katika maeneo yao

Hiyo ndiyo njia pekee, ya kuhakikisha Amani na Utulivu unadumishwa nchini

Hii njia waliyoamua kutuchagulia wananchi, ya "kututeulia" viongozi wetu wanaotuwakilisha, italeta chuki kubwa sana ndani ya jamii na kuhatarisha amani na usalama wa nchi yetu
 
Magufuli ameishiwa mbinu, na Wala hana team ya watu competent
Sio Magufuli bali ni CCM kwa ujumla wameishiwa mbinu, uchaguzi wa 2015 uliwashitua sana na sababu zilizofanya upinzani uongezeke ni baada ya JK kuwapa Uhuru upinzani kuanzia Bungeni mpaka nje ya Bunge ikapelekea upinzani kuimarika na kuleta ushindani mkubwa kipindi kile kwa hiyo sasa hv wameamua kuviminya wakiogopa kupoteza Utawala wao nchini
 
Sio Magufuli bali ni CCM kwa ujumla wameishiwa mbinu, uchaguzi wa 2015 uliwashitua sana na sababu zilizofanya upinzani uongezeke ni baada ya JK kuwapa Uhuru upinzani kuanzia Bungeni mpaka nje ya Bunge ikapelekea upinzani kuimarika na kuleta ushindani mkubwa kipindi kile kwa hiyo sasa hv wameamua kuviminya wakiogopa kupoteza Utawala wao nchini
Wamechelewa sana........

Kwa kuwa hivi sasa hawa CCM hawawezi tena kuuwa upinzani nchini, kwa kuwa hivi sasa upinzani siyo vyama vya upinzani bali upo ndani ya mioyo ya mamilioni ya wananchi!
 
Awamu hii iliandaliwa kuua upinzani! Tumeona jinsi wabunge na viongozi wa upinzani wanavyowekwa ndani, kuteswa na kupotea.

Tusitarajie kuwa kutakuwa na mabadiliko maana Rais aliyepo amelikamata jeshi kama kinga yake, anawaonyesha mapolisi kama yeye ndo mkombozi wao.

Amewachukua walimu wa vyuo vikuu ambao aliogopa watampinga na kuwapa vyeo vya kisiasa mpaka ubunge wa kuteuliwa. Wote wamekuwa Brainwashed hawana cha kufanya zaidi ya kupiga makofi na kushangilia kila linalosemwa.

Vyombo vya habari vya serikali na vile vinavyoshahadidia kilichopo kama TBC aliyeteuliwa kuwa mkurugenzi sasa amekuwa bubu kabisa Lyoba wanayemfahamu akiwa mlimani siye yule sasa.
Vipa umbele vimekuwa kwenye miundombinu na usafiri badala ya kununua madawa, kuongeza mishahara wafanyakazi wa serikali, kuajiri vijana wanaomaliza vyuo, kutafuta soko la mazao badala ya kujichukulia sheria ya kujiingiza kwenye mazao kama korosho.

Wale wanaojiunga ccm kuunga mkono wanafanya hivyo kulinda maslahi yao kama alivyofanya Lowasa.
 
niah,
Kusema ukweli ni kuwa watawala wa awamu hii wanafanya kila wawezalo, kuurejesha mfumo wa chama kimoja nchini.............

Kinyume cha Katiba yetu ya nchi ambayo inasema kuwa nchi yetu ni ya mfumo wa kidemokrasia na ni wa vyama vingi
 
Kusema ukweli ni kuwa watawala wa awamu hii wanafanya kila wawezalo, kuurejesha mfumo wa chama kimoja nchini.............

Kinyume cha Katiba yetu ya nchi ambayo inasema kuwa nchi yetu ni ya mfumo wa kidemokrasia na ni wa vyama vingi
Inavyoonekana tusahau vyama vingi. Naona sisi tulioishi tangu tupate uhuru mpaka 92, tulishazoea utawala wa kiimra. Kama umemsikiliza Mzee Lwaitama ameeleza kila kitu. Tusubiri ila yajayo yanasikitisha. Tutakuwa kama Zimbabwe soon.
 
Huyu hapa anayeminya demokrasia ,achana na serikali
tapatalk_1574414219590.jpeg
 
Hiyo miradi itawakondesha sana zaidi ya hapo hamieni kenya!
Ninchouliza Mkuu Kipara kipya, ni kwanini Serikali yetu ya awamu ya tano inamimya Demokrasia kwa kutumia kivuli cha kufanya maendeleo makubwa?

Hivi si wangewaachia wananchi wenyewe waamue kwa kuyaona maendeleo hayo makubwa?

kwani Serikali hii haijasikia ule msemo maarufu wa wahenga unaosema kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza?
 
Back
Top Bottom