Ni kwanini watu wengi hawapendi kuitwa majina yao halisi na watoto wao?

Ni kwanini watu wengi hawapendi kuitwa majina yao halisi na watoto wao?

SubTopic

Member
Joined
Sep 15, 2021
Posts
95
Reaction score
175
Kwa mfano baba anaitwa Juma hatotaka mwanae amuite wee Juma Ila atataka amuite baba au mama anaitwa Esta. Hatoruhusu mtoto wake amuite Esta Ila amuite mama.Je Kuna shida gani mwanao akikuita jina lako?
 
Kwa mfano baba anaitwa Juma hatotaka mwanae amuite wee Juma Ila atataka amuite baba au mama anaitwa Esta. Hatoruhusu mtoto wake amuite Esta Ila amuite mama.Je Kuna shida gani mwanao akikuita jina lako?

Zoeza wanao wakuite kwa namna yoyote tofauti na ilivyozoeleka ila wafundishe wakija kwenye jamii wafuate protocol.
 
Unaonekana we ni kijana mdogo almaarufu Gen Z, kuita baba/mama/shangazi/mjomba inaweka heshima kati ya mzazi na mwanae, bila hivyo hapatakuwa na heshima, jina/namna unavyoita mtu inaleta picha halisi unamueshimu mtu kwa kiasi gani...
...
mfano, mfanyakazi kumuita mwajiri wake Jacob ni anamkosea heshima lakini akimuita Bosi Jacob/mkurugenzi inaleta heshima kuonesha yupi mkubwa yupi mdogo.
HESHIMA ndio sababu mkuu
 
Unaonekana we ni kijana mdogo almaarufu Gen Z, kuita baba/mama/shangazi/mjomba inaweka heshima kati ya mzazi na mwanae, bila hivyo hapatakuwa na heshima, jina/namna unavyoita mtu inaleta picha halisi unamueshimu mtu kwa kiasi gani...
...
mfano, mfanyakazi kumuita mwajiri wake Jacob ni anamkosea heshima lakini akimuita Bosi Jacob/mkurugenzi inaleta heshima kuonesha yupi mkubwa yupi mdogo.
HESHIMA ndio sababu mkuu
Hapa kwa mwajiri umekosea sana. Ni huku Afrika ndiko kwenye huu ujinga. Majuu bosi unamwita jina lake, tena la kwanza.
 
Kwenye simu amekusevu jina lako halisi Mtemaganya
 
Ukiachana na hayo!

Mwanaume unaitwaje "Baba Amina" "Baba Rose" Baba Queen" Baba Suzy"[emoji16][emoji16][emoji16][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] umewaza nn?
 
Back
Top Bottom