Ni kweli Fumanizi mara nyingi humarisha ndoa...!

Ni kweli Fumanizi mara nyingi humarisha ndoa...!

You are unique kwa hilo

Nakupongeza

sio rahisi "kusamehe" ndi mana nikasema kama una roho ndogo "usijaribu" ilinichukua muda sana kusamehe, kila wakati inanijia kichwani, lakini kwa jitihada alizoonyesha kuniondoa hapo mwishowe alifanikiwa, na nilikuwa namwambia kabisa hii kitu hainitoki rohoni, Mungu kaumba binadamu na kusahau, tunafiwa na wapendwa wetu tunasahau, pia hili utalisahau tu, japo "inaumiza sana"
 
Mimi napenda sana kufumania, kwa sababu kuna ukweli uliojificha na ambao huwa atupendi kuuongelea sana, kwamba katika hasira za kufumania swali la kwanza huwa ni kwanini umefanya hivi, pamoja na kuwa linakuwa limeghubikwa na hasira lakini ukweli ni kwamba huwa kuna kiu ya kutaka kujua sababu ya kwanini mwenza wako amefanya hivyo, ndipo nawe utataka kufanya ufundi pengine uliosahaulika mliokuwa mnafanya mwanzoni mwa mahusiano yenu au kudadisi mbinu za ziada ili kumuonesha kwamba hujachuja na kwa kufanya hivyo mnajikuta mnafanya tendo la ndoa katika kasi ya ugeni!

Pia katika somo moja wapo nililosoma (linapatikana kwenye mtaala wa taaluma niliyosoma mimi) mwandishi wa somo hilo anaeleza ni jinsi gani binadamu alivyokuwa (Begging Animal) tuchukulie ulaji kama lengo la kula ni mtu ashibe apate nguvu na kuendelea kuishi kujimudu na kufanya majukumu yake, kwanini kuwepo aina tofauti za mapishi kwa kila mlo? ni kwa sababu ya kuwa na uchovu wa hisia kwamba huwezi kula kwa mfano wali kila siku,ila ubwabwa, pilau, biliani nk nk. Na hata katika mavazi hakuna anayeweza kuvaa aina moja ya nguo kwa wiki achilia mbali mwezi, lazima itachokwa na kubadilishwa kwa nyingine.

Tunachosahau ni kuwa ubongo unao control vitu vya nje kama chakula, mavazi na hata kutopenda kukaa sehemu moja bila kutembea au kuhamia kabisa sehemu nyingine, ndio ubongo huohuo unao control na hisia za matamanio ya kujamiiana. Maelezo haya au mfano huu unaelekeza kwamba itakuwa vigumu ndoa kudumu miaka mingi bila kuibiana/ kutoka nje ila tu tunapokuwa hatujakamatwa/ kufumaniwa kila mtu ni mwaminifu katika ndoa yake. Na pia si kweli kwamba huyo aliyetoka nje ya ndoa yake anakuwa amefuata mapenzi hapana ni ngono tu kubadilisha mazingira huku akiwa mapenzi kayaacha kwa mwenza wake nyumbani. Ukiona mtu mnakutana kwa ngono na kisha akakwambia nakupenda kuliko mke wangu au mume wangu NI MUONGO NA KWELI HAIMO NDANI YAKE KABISA.
 
hapo kwenye kuchunguza tatizo, sio wote watokao sababu ya matatizo,wengine hawaridhiki na mwanamke mmoja toka tumboni mwa mama zao, kama wangu alitoka coz ya ujinga wake, mama yake na mdogo wake wa kike, eti mama analazimisha nibebe mimba, mtoto ana mwaka na nusu nibebe mimba nyingine kisa kumridhisha mama? hell no, mwanaume akaanza vituko, mama akaona poa tu, dada mtu akiniletea pozi/mdomo, nikasema hawamjui mmarangu hawa, ndio yakatokea na kutokea, siku ya usuluhishi mwanaume mzima anasema mama yake alimshauri azae watoto chap chap, so aliona bora ajipumzishe huko nje,mana mkewe hakumtimizia alichotaka, sasa nikamwambia japo tumesuluhishwa, mtoto mwingine ni mpaka mie niamue, kutokana na ulivyonisumbua hakuna cha wewe, mama/dada yako, ni maamuzi yangu mie kubeba mimba kama vipi pita kushoto au jifunge salifeti ulale.
Hapa naona kama ulikiuka kiapo cha ndoa vile! manake katika kiapo cha kwetu sisi ninakoabudu huwa kinaambatana na sala isemayo "ndoa yenu na iwe na baraka tele mpatiwe uzao wa watoto waizunguke meza yenu" sasa ikiwa ndio lengo kuu na pia uzazi unao na wanaotaka uzae wapo si ingekuwa heri ukayatenda hayo?
 
Hapa naona kama ulikiuka kiapo cha ndoa vile! manake katika kiapo cha kwetu sisi ninakoabudu huwa kinaambatana na sala isemayo "ndoa yenu na iwe na baraka tele mpatiwe uzao wa watoto waizunguke meza yenu" sasa ikiwa ndio lengo kuu na pia uzazi unao na wanaotaka uzae wapo si ingekuwa heri ukayatenda hayo?

wanaotaka? oohhh puliiiiz! hiyo red tayari umeshasema unakoabudu, ninakoabudu mie hakusemi hivyo.
 
Dah!

Pole aisee

KAma hiyo ndio ilikuwa sababu ya kutoka nje, kweli ilikuwa haki yako kumtesa vile
Ni bora mtu hata aeme alipitiwa kuliko aliamriwa na mama yeke, kama teen.

usitake ukumbane na mwanaume "mtoto wa mama", nimempeleka kijeshi sasa hivi kawa "mtoto wa baba"
 
Kwa swala la kufumania... mke akifumaniwa anakuwa katika hali mbaya zaidi na kulaumiwa.. tofauti na mwanaume akifumaniwa.. ndo sababu mwanaume anaweza kuoa wanawake wanne lakini mwanamke hawezikuolewa na wanaume wanne... katika maandiko ya Biblia .. Biblia imeruhusu talaka kwa pande zote kuachana... Uzinzi pekee ndio unaoweza kuvunja ndoa kinyume na hapo .... mpaka kifo kiwatenganishe Kumb 24 ;1 -4, Marko 10:4 - 12 Math 5 ;31 - 32
 
Inaboa sana

Inakufanya mke ushindwe kucheza na nafasi yako kwa uhuru

khaa, ilipitiliza aise, kitu kidogo mama atafikiria hivi atahisi hivi atachukulia hivi kasema hivi,alaa siku hizi hamna hizo tena.
 
Mm nimiwazaga tu kufumania naumwaga na roho balaa thatha sembuse nifumanie afu nisamehe....haitatokea aiseekea kwangu itavunja ndoa instead ya kuimarisha.
 
argument.jpg


Fumanizi husababisha hisia zenye maumivu, hasira, kutokuaminiana, woga, aibu na kujilaumu. Lakini kufumania au kufumaniwa hakupaswi kuwa sababu ya kuwa mwisho wa ndoa yenu, ingawa kunaweza kuwa pia.

Baada ya fumanizi, inabidi ujitahidi kuelewa na kuweza kujenga tena ndoa yako, pengine sasa ikiwa ni ndoa imara zaidi. Hata hivyo hii inataka kujituma kwingi na uvumilivu na subira. Ndoa inaweza kuendelea hata baada ya fumanizi kwa kutumia ushauri, kupeana muda na kushirikiana. Kuna ndoa ambazo zimeweza kudumu zaidi baada ya fumanizi kutokea.

Pale kutoka nje kwa mwanandoa mmoja kunapogundulika hupelekea hisia kali kwa wanandoa wote, mshtuko, aibu, kujilaumu, kujiona mkosaji, hasira kali na wasiwasi. Kutokana na hisia hizi zote mara nyingi wengi hufanya maamuzi yasiyo mazuri kama kutengana au kuachana kabisa. Badala ya kufanya hivyo katika kipindi kile cha muda mfupi baada ya fumanizi, tunahitaji kuwa watulivu sana ili tuweze kuchukua hatua zinazofaa.

Kupata msaada:
Kwa uzima na afya yako mwenyewe, tafuta msaada kutoka kwa familia, rafiki, mchungaji, shekhe au mshauri yeyote unayemwamini wewe na kujihisi huru kwake. Kuongea kuhusu hisia zako kwa wale unaowapenda sana itakusaidia wewe kupunguza nguvu za hisia za maumivu ya tukio hilo. Kuongea na watu wengine kunaweza kukupa wewe uwezo wa kuelewa zaidi hisia zako na kupata mtazamo mwingine kuhusu tukio.

Pengine aliyetoka nje inawezekana hatosheki katika mahusianao katika ndoa yake au hawajibiki vizuri katika ndoa. Au pengine hawezi kudhibiti mihemko yake. Mabadiliko ya maisha kama kuzaliwa mtoto au upweke wa aina fulani, unaweza kuwa ndio sababu ya kutoka nje. Inabidi haya yatazamwe kabla mtu hajaamua lolote.

Kwa hiyo kujua sababu ya mwingine kutoka nje ni muhimu sana na hii inaweza kukupa ahueni, kwani unaweza kubaini kitu ambacho kinaonesha kwamba, kwako pia kuna matatizo. Hatua zitakazokusaidia kujenga upya ndoa yako baada ya fumanizi ni nyingi. Lakini hizi ni baadhi tu ambazo kwa mazingira yanayokukabili, zinaweza kukusaidia.

Kuacha kutoka nje ya ndoa:
Hatua ya kwanza ni kwa mwanandoa kuacha tabia ya kutoka nje ya ndoa kiukweli.

Kukubali kuwajibika:
Kama umetoka nje ya ndoa, kuwa tayari kuwajibika katika vitendo vyako.

Onyesha nia ya malengo yako:
Kuwa na uhakika kuwa wote wawili mko tayari kujenga upya ndoa yenu.

Onana na mshauri wa wanandoa:
Mtafute mshauri wa ndoa ambaye atakusaidia kujenga upya ndoa yako kama itakuwa inahitajika. Onana na mshauri wa ndoa ambaye alishawahi kukutana na kusaidia kutataua matataizo ya fumanizi. Mwepuke mshauri ambaye anaamini kufumania au kufumaniwa ndio mwisho wa ndoa yenu.

Kuchunguza tatizo:
Kufumania au kufumaniwa huzua matatizo katika ndoa. Chunguzeni kwa makini mahusiano yenu ili uweze kujua nini kilichosababisha au kilichopelekea kutoka nje ya ndoa na nini mfanye ili kuzuia kutoka nje ya ndoa tena

Kila mmoja apewe nafasi:
Kila mwanandoa anahitaji kupumzika kwa ajili ya kuondoa msongo na wasiwasi kutokana na tukio la fumanizi, hii ni kwa sababu huwa ni vigumu kusikiliza ushauri wakati mihemko iko juu sana.

Pata muda:
Epuka kujua undani zaidi kuhusu fumanizi la mwenzi wako kwa wakati wa mwanzoni. Ahirisha mjadala huo kwanza mpaka uzoee ile hali ya kumfumania mwenzi wako.

Mwisho wa ndoa au hapana ?
Siyo kila ndoa iliyoguswa na suala hili la fumanizi ni lazima imalizike kwa kutokuachana. Wakati mwingine kunakuwa na uharibifu mkubwa na wanandoa hawana budi kuachana na pia kama wanandoa hawako tayari kuwa pamoja tena.

Lakini kama wote mko tayari kujenga upya ndoa yenu, basi suala hili huwa rahisi sana na uhusiano utaendelea kuwa mzuri na wa amani zaidi.
Uongo
 
Back
Top Bottom