Ni kweli hakuna aliye juu ya Sheria nchini?

Ni kweli hakuna aliye juu ya Sheria nchini?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Nimeshasikia hivyo tokea nikiwa mdogo, lakini kama si sahihi kwa asilimia mia moja.

Kwenye nchi hii, kuna watu ambao ni kama vile hawagusiki, haijalishi watakachofanya! Hapo siwaongelei viongozi, bali vigogo wanaoweza kuonekana kama vile wameiweka Serikali mfukoni.

Kikatiba, Rais wa Tz hashtakiwi akiwa madarakani na hata baada ya kutoka madarakani!

Kama ndivyo, hata akiamua kufanya kosa la jinai hatachukuliwa hatua zozote za Kisheria?

Chukulia kwa mfano, Rais aliyeko madarakani akiamua kumpiga mtu risasi hadharani kuna mtu atakayethubutu kumchukulia hatua?

Hivi kwa mfano, Rais mstaafu, Kikwete, akigombana na mtu, labda jirani yake, na (Kikwete ) akaamua kumtukana, anaweza kuchukuliwa hatua zozote?

Nimeuliza kwa sababu ninataka kufahamu! Naomba nisituhumiwe kuwa ninauliza maswali mepesi. Majibu yake yana umuhimu mkubwa sana kwangu.
 
Popote pale duniani, wakubwa kamwe hawawezi kuguswa.
Sheria zimetungwa ili kuwatumikia wakubwa, wakubwa ndio waliotunga sheria kwa maslahi yao, hautaona vigogo kamwe wakiguswa popote pale duniani.
Fikiri kwa kina
 
Popote pale duniani, wakubwa kamwe hawawezi kuguswa.
Sheria zimetungwa ili kuwatumikia wakubwa, wakubwa ndio waliotunga sheria kwa maslahi yao, hautaona vigogo kamwe wakiguswa popote pale duniani.
Fikiri kwa kina
Siyo kweli mkuu!
Naamini ulishasikia kesi za hawa:
1. Jacob Zuma - South Africa
2. Ramaphosa - South Africa
3. Donald Trump - USA
 
Siyo kweli mkuu!
Naamini ulishasikia kesi za hawa:
1. Jacob Zuma - South Africa
2. Ramaphosa - South Africa
3. Donald Trump - USA
Wako wapi sasa hivi? Muda mwengine mgongano wa kimaslahi upo, tangu azali.
"When the plot against emperor fails, the plotters were always given the chance to let their families keep their fortunes" - THE GODFATHER
 
Back
Top Bottom