Ni kweli kabisa hatupaswi kujilinganisha na nchi nyingine!

Ni kweli kabisa hatupaswi kujilinganisha na nchi nyingine!

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,836
Reaction score
6,303
Naungana kabisa na mheshimiwa Rais, kwenye suala la katiba hatupaswi kuwa na haraka kwa kujilinganisha na nchi nyingine.

Vivyo hivyo hata kwenye masuala ya ukusanyaji wa kodi hatupaswi kujilinganisha na 'wenzetu Indonesia, Japan, Austraria' nk maana ni kweli hatufanani!

Mara kadhaa tumekuwa tukiwasikia viongozi wa serikali wanapotaka kusisitiza jambo fulani husema, "kwa mfano wenzetu Marekani...!"

Hivyo basi ili kusudi suala hili likae sawa, si tu kwenye mabadiliko ya katiba kujilinganisha na wenzetu Kenya, bali hata kwenye masuala mengine ikiwa ni pamoja na njia za ukusanyaji wa kodi na makato mengine. Nchi yetu bado inahitaji elimu kabla ya utekelezaji!

Naomba kuwasilisha!
Ndimi mbunge ajaye!
 
Hata ubinafisishaji wa Bandari hatupaswi kujilinganisha na Kenya eti tukichelewa watatupita.
 
Kabla ya kuwaza kubadili katiba nzima ni bora tubadili vifungu baadhi maana kubadili katiba nzima sio jambo la kitoto maana tunaenda kutikisa mfumo mzima wa nchi.

Kwa mfano kwenye katiba pendekezwa ya Mzee warioba ilipendekezwa kwamba mbunge anapofariki ,yule aliyeshika namba mbili aendelee bila kufanyika uchaguzi kama ilivyo Sasa. Kifungu kama hiki wananchi waelimishwe vya kutosha Kwa sababu unapotaka mshindi wa pili achukue tu madaraka maana yake unatengeneza mazingira ya kuuana.

Kifungu ambacho kinachezea madaraka ya Rais kifutwe, niliwahi kusema kwenye Uzi Fulani kwamba sikubalini na mabadiliko ya katiba yenye lengo la kupora au kupunguza madaraka ya Rais unaweza kufanya marejeo kwenye Uzi huo.

Kwa hiyo kabla ya kusema tunaandika katiba mpya watu wafundishwe ya Sasa. Prof.Kabudi aliwahi kusema Katiba hii hii imetuvusha na kutusadia katika nyakati za mitikisiko na hatari. Kama iliweza kutusaidia kipindi hiko basi hata Sasa yafaa
 
Back
Top Bottom