Ulifanya jambo jema sana hasa kama hukuwahi kuhusiana kimwili na mtu mwingine kabla yake. Wengine hayo yalitushinda na kwa kweli nimeshaona baadhi ya madhara yake. Nasema ni nzuri kawa sababu kimsingi unakuwa huna yardstick ya kumpima/linganisha (kwa maana ya tendo la ndoa!)....huo ndio ulikuwa mpango wa Mungu.
Kuingia kwenye ndoa wakati umeshaonjaonja mara kadhaa sehemu zaidi ya moja wakati mwingine kunaleta matatizo kwa sababu tayari unakuwa unajua 'mema na mabaya' na hivyo unashindwa kurizishwa na mmoja!
Si kila ndoa watu wanapendana, wengine wameoana just bcoz wamezaa wanaogopa watoto wasije wakapa taabu!!JADILI..
Hii ni mada inayojadiliwa Star TV.Mawazo yanayotolewa yanatisha..
Hata mimi ningetaka ningeweza kukudanganya hivyo hivyo;Ni kweli,lakini kwa maelezo ya Gaijin......ni mlokole kwa sababu alivumilia mpaka mwisho!..............
Ndoa tunachukulia kama ni kutimiza wajibu zaidi kuliko ukweli kuwa ni kitu ambacho kinataka wakati wote kifanyiwe kazi ili kiweze kutoa matunda yaliyokusudiwa. Kwa bahati mbaya huwa hatutafakari sana ndo inahitaji nini zaidi ya kuchukulia mapenzi ya haraka haraka tunayopfanya. Watu wengine wanaweza kuwa wapenzi wazuri kama b/f na g/f lakini hawawezi kuwa wana ndoa wazuri. Ni watu wa kufurahiana kama wanachukua na kufanya hiki na kile kisha kila mtu anaenda na zake lakini sio kulala na kuamka kitanda kimoja day in day out. Mnachokana mapema na maudhi yanakuwa kibao.Kama hujafunga ndoa...angalia machungu mwenzio anayokupa kabla hamjaoana...tafakari uyawaze..jiulize mkishaoana utaweza kuyavumilia?
Ikiwa unaona utaweza kuyavumilia ( tamaa ya pesa/mali,lugha mbaya, ulevi, uongo, kutokua mwaminifu, uchafu, uvivu,kutokuwa na huruma, kutokuwa na kauli nzuri/tamu, kutokusema samahani, kutokujua kubembeleza, ubinafsi,uchoyo, ) BASI KAFUNGENI NDOA na hii ni kwa wote wanawake kwa wanaume.
To me Love has nothing to do with sex. Ndo maana nilimpenda mamito wangu kwa zaidi ya miaka mitatu ndo tukasex. Niliposex tu, hapo hapo nikatangaza nia. I got what I wanted!!
Kweli dada. G atueleze kulikuwa na sababu gani wakaamua kusubiri, na iliwachukua muda gani kusubiri? Lazima kulikuwa na motivation ya kufanya hivyo.
Halafu itakuwa vizuri akitueleza walikuwa na umri gani kabla ya kuoana na kama wote wawili waliwahi kuwa na mahusiano mengine kabla ya kukutana!
Hata mimi ningetaka ningeweza kukudanganya hivyo hivyo;
Laiti mioyo ingekuwa transparent, Laiti Kuta zingekuwa zinazungumza...................
Sasa na hizi artificial love (za kichina china) zinatokea wapi?
Halafu kuna mambo umekuwa ukizungumzia (mf. kupika, usafi etc), mimi kwangu sikuyapa uzito hata kidogo ingawa niliomba niyapate na nimepata kweli. Mimi nilikuwa namtafuta rafiki wa kweli (tunayependana na kuridhishana) na hayo mapungufu yake nilikuwa tayari kuyabeba isipokuwa yale ya hatari kama ulevi, uongo na kugawa chakula cha mwenyewa kwa vijizi!
Ni kweli,lakini kwa maelezo ya Gaijin......ni mlokole kwa sababu alivumilia mpaka mwisho!..............
kuvumilia mpaka mwisho ina maana aliolewa akiwa virgin?
hakuna sababu ya kusema uongo.................ningelikuwa nimefanya ningesema nimefanya, hakuna ninaemuogopa humu ati. na mengineyo niliyoyafanya nasema nimefanya sana tu, na najutia ............lakini hilo sijafanya.
but unaweza kuchukulia vile unavyopenda wewe....................haina dhara kwangu wala kwako
nyamayao naona mshangao wako mkubwa mno .................kwema?
niliolewa nikiwa 28 na mwanamme ana 31. na tulisubiri kwa mwaka na nusu mpaka kuoana. hatukufanya kwa sababu mimi niliamini ni dhambi na nilipohama kwetu kuishi nje ya nchi i was 19, mama yangu aliniusia nifanye yote lakini sio kitu hicho coz kitamfanya sad sana na atajutia kuniachia kuishi mwenyewe kama siwezi kujihifadhi.
so i needed to keep my promise to God and to her .......i guess
naweza kusema kitu kimoja ambacho kilisaidia ni kuwa huyo mwanamme tunajuana tokea ni watoto lakini urafiki hasa wa kufika kupendana tuliuanzia huko huko tulikokuwa tunaishi.
but nilikuwa siendi kumtembelea mjini kwake hata iweje................yeye ndio anakuja, na akifika afikie hoteli.
bila ya shaka yeye aliwahi kuwa na uhusiano na watu wengine, but mie ndo huyo huyo one and only .........
nyamayao kwani vimasuala vya aina ile si nasikia inakuwa mwaka wa kwanza tu?! baada ya hapo mna cruise kama kawaida au?
ushauri wangu kwa wanaotaka kuepukana na masuala yanayokumba jamii ...........always be a trend setter ( watu wakufate wewe), ukiwa wewe mfataji trend tu utawaka.
Si kweli WOS wengine waliingia kwenye ndoa kwa sababu ya fashions na wao waonekane wanandoa :A S-rose:
Wengine waliingia kwenye ndoa kwa kujilazimisha = 30%
Wengine walibeba mimba ikawalazimu kuingia kwenye ndoa = 5%
Wengine wamefata pesa au mali ndani ya ndoa = 15%
Wengine wanajiegesha jua litulie kisha waendelee na safari = 20%
Wengine wapo kwa ajili ya heshima ya wazazi. = 5%
wengine ni kweli wanapendana.. = 20% - Kama Mr and Mrs Obuntu
NK. Nk. = 5%
Dah! Haya, naona umeamua kuusemea moyo wake.Ni kweli,lakini kwa maelezo ya Gaijin......ni mlokole kwa sababu alivumilia mpaka mwisho!..............
mie niliulizwaga mwanzoni kabisa..bfnd/galfrnd, lakini nilipokuwa ndani sasa, yule mwanaume alieniacha(mana niliachwa) ikatokea tupo mji mmoja kwenye kutafuta maisha, akaanza usumbufu wa hapa na pale, mpaka mr akahic kitu fulani hivi, nikasema ngoja nijitoe kimasomaso kumwelezea kwamba mhucka alikuwa ni huyu na sasa anaanza kusumbua fulani hivi(lilikuwa kosa kubwa kusema) nilikuwa siendi mahali bila mr/mtu wa ziada, nilikuwa cna uhuru/amani kabisa, mpaka ikatokea cku moja ishu imeniletea kasheshe, mana alieniacha alikuwa anacctiza mie nilikuwa chaguo lake sema shetani alimpitia so kwa gharama yoyote ananirudisha kwenye himaya yake, sasa hapo ilikuwa nikitoka ofcn huyu hapa, cku moja natokea supermarket mie cjui kama mtu ananiwinda mara huyu hapa kaanza kunivuta akitaka apate hata dk chache tuongee kdgo, mr yupo parking anaona kila kitu...nickuelezee kilichotokeaa, ctaki kukumbuka kabisa.
Hahahaha! dada yangu bana...... Ulimpa nini huyu mtu mpaka akakuganda hivyo. Si lazima usemee hapa, twende kwenye PM.mie niliulizwaga mwanzoni kabisa..bfnd/galfrnd, lakini nilipokuwa ndani sasa, yule mwanaume alieniacha(mana niliachwa) ikatokea tupo mji mmoja kwenye kutafuta maisha, akaanza usumbufu wa hapa na pale, mpaka mr akahic kitu fulani hivi, nikasema ngoja nijitoe kimasomaso kumwelezea kwamba mhucka alikuwa ni huyu na sasa anaanza kusumbua fulani hivi(lilikuwa kosa kubwa kusema) nilikuwa siendi mahali bila mr/mtu wa ziada, nilikuwa cna uhuru/amani kabisa, mpaka ikatokea cku moja ishu imeniletea kasheshe, mana alieniacha alikuwa anacctiza mie nilikuwa chaguo lake sema shetani alimpitia so kwa gharama yoyote ananirudisha kwenye himaya yake, sasa hapo ilikuwa nikitoka ofcn huyu hapa, cku moja natokea supermarket mie cjui kama mtu ananiwinda mara huyu hapa kaanza kunivuta akitaka apate hata dk chache tuongee kdgo, mr yupo parking anaona kila kitu...nickuelezee kilichotokeaa, ctaki kukumbuka kabisa.