Ni kweli maisha magumu, lakini tumia kanuni hii 50%+30%+20 kuyalainisha

Ni kweli maisha magumu, lakini tumia kanuni hii 50%+30%+20 kuyalainisha

Boran Jakutay

Senior Member
Joined
Apr 8, 2023
Posts
110
Reaction score
259
50% ya kipato chako fanya matumizi ya muhimu / ya lazima mfano kulipa kodi au ada ya mtoto.

30% ya mshahara au kipato chako tumia kwa matumizi yasiyo na ulazima, mfano kukunua nguo, radio, saa, kwenda beach, kwa kifupi mwagilia moyo, hivyo ni vitu ambavyo sio vya lazima yaani usipovifanya huathiriki na chochote.

20% ya kipato chako WEKA AKIBA, hiyo Ni lazima uweke akiba na akiba lazima uweke na malengo, la sivyo utatumia tu hiyo pesa, weka malengo naweka pesa hii baada ya miezi 6 au mwaka nitakuwa na kiasi hiki nitanunua kitu fulani iwe kiwanja, nyumba au gari, yale malengo yako yatakufanya kuiheshimu AKIBA uliyoiweka.

NYONGEZA TU

1. Usitumie pesa kwa kujionesha, upo na mademu unatumia fedha hovyo ili uonekane matawi ACHA HIYO TABIA.

2. Weka fedha ya dharura.

3. Usitembee na fedha nyingi mfukoni ambazo hujaziweka kwenye matumizi, mfano naenda Kariakoo kununua begi Sh 50,000 na nguo Sh 20,000, nauli Sh 2,000, jumla Sh 72,000, hivyo beba Sh 75,000, hiyo nyongeza Sh 3,000 ni ya dharura, kafanye matumizi, usibebe Sh 100,000, hautarudi na chenji.

4. Biashara usichanganye na urafiki, undugu wala mapenzi.

5. USIMKOPESHE FEDHA MTU AMBAYE HUWEZI KUMDAI, mfano mama mkwe, mpenzi
 
50% ya kipato chako fanya matumizi ya muhimu / ya lazima mfano kulipa kodi au ada ya mtoto.

30% ya mshahara au kipato chako tumia kwa matumizi yasiyo na ulazima, mfano kukunua nguo, radio, saa, kwenda beach, kwa kifupi mwagilia moyo, hivyo ni vitu ambavyo sio vya lazima yaani usipovifanya huathiriki na chochote.

20% ya kipato chako WEKA AKIBA, hiyo Ni lazima uweke akiba na akiba lazima uweke na malengo, la sivyo utatumia tu hiyo pesa, weka malengo naweka pesa hii baada ya miezi 6 au mwaka nitakuwa na kiasi hiki nitanunua kitu fulani iwe kiwanja, nyumba au gari, yale malengo yako yatakufanya kuiheshimu AKIBA uliyoiweka.

NYONGEZA TU

1. Usitumie pesa kwa kujionesha, upo na mademu unatumia fedha hovyo ili uonekane matawi ACHA HIYO TABIA.

2. Weka fedha ya dharura.

3. Usitembee na fedha nyingi mfukoni ambazo hujaziweka kwenye matumizi, mfano naenda Kariakoo kununua begi Sh 50,000 na nguo Sh 20,000, nauli Sh 2,000, jumla Sh 72,000, hivyo beba Sh 75,000, hiyo nyongeza Sh 3,000 ni ya dharura, kafanye matumizi, usibebe Sh 100,000, hautarudi na chenji.

4. Biashara usichanganye na urafiki, undugu wala mapenzi.

5. USIMKOPESHE FEDHA MTU AMBAYE HUWEZI KUMDAI, mfano mama mkwe, mpenzi
Nyongeza #3 ya kibabe sana. Tena na siku hizi kuna mobile transactions, matumizi yasiyopangwa ni kama kumsukuma mlevi.
 
Fafanua 😂😂😂😂
Umetunza hela umepiga namahesabu yako ya hamsini mara ngapingapi huko mara unamnyima mchepuko na mganga unamzurumu n.k Ile haujakaa sawa tu unapigiwa simu toka Kijijini unaambiwa bibi kameza chemli hivyo pesa ya matibabu inahitajika! Hapo Sasa utajua hujui...😂
 
Umetunza hela umepiga namahesabu yako ya hamsini mara ngapingapi huko mara unamnyima mchepuko na mganga unamzurumu n.k Ile haujakaa sawa tu unapigiwa simu toka Kijijini unaambiwa bibi kameza chemli hivyo pesa ya matibabu inahitajika! Hapo Sasa utajua hujui...😂
😂😂😂😂😂😂haya mambo aisee
 
50% ya kipato chako fanya matumizi ya muhimu / ya lazima mfano kulipa kodi au ada ya mtoto.

30% ya mshahara au kipato chako tumia kwa matumizi yasiyo na ulazima, mfano kukunua nguo, radio, saa, kwenda beach, kwa kifupi mwagilia moyo, hivyo ni vitu ambavyo sio vya lazima yaani usipovifanya huathiriki na chochote.

20% ya kipato chako WEKA AKIBA, hiyo Ni lazima uweke akiba na akiba lazima uweke na malengo, la sivyo utatumia tu hiyo pesa, weka malengo naweka pesa hii baada ya miezi 6 au mwaka nitakuwa na kiasi hiki nitanunua kitu fulani iwe kiwanja, nyumba au gari, yale malengo yako yatakufanya kuiheshimu AKIBA uliyoiweka.

NYONGEZA TU

1. Usitumie pesa kwa kujionesha, upo na mademu unatumia fedha hovyo ili uonekane matawi ACHA HIYO TABIA.

2. Weka fedha ya dharura.

3. Usitembee na fedha nyingi mfukoni ambazo hujaziweka kwenye matumizi, mfano naenda Kariakoo kununua begi Sh 50,000 na nguo Sh 20,000, nauli Sh 2,000, jumla Sh 72,000, hivyo beba Sh 75,000, hiyo nyongeza Sh 3,000 ni ya dharura, kafanye matumizi, usibebe Sh 100,000, hautarudi na chenji.

4. Biashara usichanganye na urafiki, undugu wala mapenzi.

5. USIMKOPESHE FEDHA MTU AMBAYE HUWEZI KUMDAI, mfano mama mkwe, mpenzi
Ni kweli ulichosema, japo kuna watu kipato chao hakitowaruhusu kugawanya hizo percentage
 
unaweza ukajipanga sana mwishowa siku ukangukia pua kikubwa wacha mambo yajiset yenyewe
 
Back
Top Bottom