Ni kweli maisha ya Messi wa Simba yako hivi?

Ni kweli maisha ya Messi wa Simba yako hivi?

labda nikusahihishe mshahara wake ni milioni moja na nusu aliongezewa ndio pale panaleta mgogoro maana simba wanasem,a walipo mbadilishia mshahara na mkataba uliongezwa inawezekana kuna watu wanapiga pesa kupitia mgongo wake na ndio hao wanachochea utambi
 
Yale ya Shafii Dauda bila shaka ni kuongeza chumvi kwenye issue yenyewe. Hilo halina ubishi. Hoja ya msingi kijana anaonewa. Si mara ya kwanza huo ujanja ujanja wa viongozi kuwakomoa wachezaji.

Afadhali wachezaji wawe na mawakala wa kuwasimamia tena wasajiliwe TFF kabisa. Hatua ya kwanza, mchezaji mwenyewe awe na mkataba na wakala ili hoja zake zitambulike rasmi TFF!
Mkuu, kuna thread nyingi sana zimeanzishwa kuhusu uhalisia wa ile mikataba, na mimi sijataka nizungumzie mambo ya mikataba kwani yameshazungumzwa sana. Hapa nazungumzia kipato cha Messi vs picha alizopiga gheto na jinsi alivyojielezea kuwa 'maskini'. Ni vyema ukajikita katika mada kama unalo la kuchangia
 
labda nikusahihishe mshahara wake ni milioni moja na nusu aliongezewa ndio pale panaleta mgogoro maana simba wanasem,a walipo mbadilishia mshahara na mkataba uliongezwa inawezekana kuna watu wanapiga pesa kupitia mgongo wake na ndio hao wanachochea utambi
Kama ni 1.5 M basi ni kwamba unazidi kuchochea mada, maana kwa mujibu wa habari picha ya ile blog, ni kwamba Messi ana kipato kidogo sana
 
huyu bwna mdogo pia inawezekana hajielew.. elimu ndogo au anauswahili mwingi sana asije akadanganywa then baadaye akajikuta anapotea ktika soka. kama simba wamemfanyia uhuni kwenye mkataba wake hili si jembo jema hata kidogo na siwezi liunga mkono. la msingi sasa wakae watatue jambo hili wakishindana kuna mtu ataathirika...
 
Mkuu, kuna thread nyingi sana zimeanzishwa kuhusu uhalisia wa ile mikataba, na mimi sijataka nizungumzie mambo ya mikataba kwani yameshazungumzwa sana. Hapa nazungumzia kipato cha Messi vs picha alizopiga gheto na jinsi alivyojielezea kuwa 'maskini'. Ni vyema ukajikita katika mada kama unalo la kuchangia

Simba hawana pesa ya kuwalipa wachezaji kama mtoa mada alivyo ainisha wengi wao wanajitolea kwa mapenz yao binafsi na klab. Kama kweli hzo pesa zote zilizoainishwa hapo juu angekuwa analipwa vizr hata muonekano wake ungekuwa nadhifu sasa anaonekana kama mchezaji wa mchangani, viongozi wa simba wangepinga kwa hoja na ushahidi kama kweli messi haishi ktk mazngira hayo,sasa mbn wapo kimya na hawapingi hlo jambo halafu watu wanataka eti waisapoti simba wakati wanawapa wachezaji ahadi hewa.
 
Sakata kama la mesi ndio mambo yanayoharibu mpira wa tanzania.

kitu chochote unapokiendesha kwa mifumo isiyo na usawa hauwezi kupata mafanikio. kuwa na viongozi wababaishaji katika sekita yoyote ndio mwanzo wa sekita husika kuporomoka.

kanuni ya mshahara kwa mfanyakazi au mchezaji ni lazima mshahara uendane na mchango wa mwajiriwa katika kuingiza mapato hasa kwa biashara ambayo juhudi za mtu ndizo zinazoteka soko.

unakuta mchezaji ni tegemeo katika timu lakini kwa kuwa yeye hakuwa mjanja wakati wa kuingia mkataba basi analipwa kidogo huku kuna mchezaji ambaye mchango wake ni hafifu analipwa vizuri sana. kiongozi anayeweza kulea tofauti kama hizo katika timu yake ajue hajui maana ya uongozi maana tofauti kama hizi ndizo hupelekea wachezaji kuwa na uwezo mkubwa lakini kwa tathmini ya jinsi wanavyolipwa wanafanya migomo baridi kwa kuacha kujituma.

kama timu inataka kupata mafanikio itaboresha maslahi ya mchezaji yeyote anayejituma ili yaendane na hadhi ya kiwango chake na hilo huhamasisha wote kwenye timu kuongeza juhudi ili waongeze vipato.

lakini timu zikianza kuona eti huyu tulimsaidia kitu fulani huko nyuma hivyo tunatakiwa kumlipa kidogo hao hawajui wanachokifanya. timu inapofanikiwa kutengeneza star ni kutafuta mbinu zote za kumtumia kufanya biashara kupitia kwake uwanjani na nje ya uwanja lakini ukisikia haya tunayoyasikia basi unajua tuna safari ndefu.

yawezekana yaliyosemwa hayakuwa sahihi lakini kwa kuangalia ni wazi kuwa huyo alitaka kufikisha ujumbe na ujumbe wenye haukueleweka ila yeye alitaka kusema malipo ambayo timu inamlipa mchezaji huyu hayaendani na mchango wake kwenye timu wakilinganisha na jinsi inavyofanya kwa baadhi ya wachezaji wengine.

Ni nadra sana kunikuta najadili maisha ya mtu binafsi. Lakini kama mjadala huo utakuwa unahusiana na jambo lolote linalogusa public interests, basi huwa sina budi kujadili

Wiki zaidi ya moja iliyopita kumeendelea kuwepo kwa mvutano wa Ramadhan Singano aka Messi wa Simba na klabu yake. Katika hali ya kushangaza, blogger mmoja maarufu nchini (nadhani mtakuwa mnamjua tu) amemshawishi mchezaji huyo wa Simba kuonyesha hali ya maisha yake anayoishi, pengine kwa lengo la kuuonyesha umma kwamba mchezaji huyo amekuwa ananyonywa na klabu yake kiasi kwamba maisha yake yamekuwa duni ukilinganisha na ukubwa wa jina lake. Mchezaji huyo alipigwa picha akiwa ndani na nje ya nyumba yake na kuonyesha vitu vichache anavyomiliki katika gheto alilizamia kwa kaka yake

Nimejiuliza maswali mengi kuhusu kipato alichonacho Messi na hali ile iliyoonekana. Baadhi ya vipato hivyo ni:
1. Hela ya usajili sh. milioni 13 yaani 13,000,000/= aliyopewa mwaka 2013
2. Mshahara kutoka Simba sh. 700,000/= kwa mwezi take home usioguswa na kodi yoyote
3. Gari aina ya Suzuki Carry 4WD la kubeba mizigo alilopewa mwaka 2013 bure na shabiki wa Simba Musley Luwah wa Oman, (kadiria mwenyewe kwa siku 'hesabu' yake ni shilingi ngapi anayoletewa na dereva. Kwa uthibitisho wa hili gari, soma hapa: Messi wa Simba azawadiwa gari - Global Publishers
4. Posho za klabu yake ambazo hubadilika mara kwa mara (mapato mtakadiria wenyewe)
5. Posho alizokuwa anapata wakati akiwa mchezaji wa timu ya Taifa - kila siku ya kuwepo kambini sh. 50,000/= pamoja na posho nyingine za kucheza mechi
6. Tangazo la biashara analofanya ITV la magodoro ya Dodoma maarufu kama kwa mzee Mangungu (mapato mtakadiria wenyewe)
7. Hela anazookoa katika matumizi anapokuwa kambini na Simba na Taifa Stars (gharama za Hotel malazi na chakula ni juu ya timu). Jaribu kufikiria ni asilimia ngapi ya muda wake katika mwaka anakuwa yupo kambini akila na kulala bure
8. Hili lingine ni personal sana sitalizungumza kwa undani, ila kwa ufupi hana watoto, familia wala wazazi wategemezi so hela nyingi anabaki nazo yeye

Sasa wenye akili mjiulize, ungekuwa wewe ndio kijana unapata mapato hayo, maisha yako yangekuwa ya kichovu vile?
-Vijana wangapi wanahangaika lakini hivyo hivyo wanajitahidi kujitegemea na si kuishi kwa kaka zao?
-Messi kusema ana maisha duni, huku sio kumkufuru Mungu?
-Kama amejibana kwa kaka yake kwenye single room na kuna TV na kitanda na viti vichache, ina maana kaka yake alikuwa hana fenicha yoyote kabisa isipokuwa alikuwa anamiliki chumba tu kitupu?
-Ni kweli pale ndipo anapoishi Messi au ana makazi mengine?

Maswali hayo nawaachia, akili mlizoambiwa za huyo mmiliki wa blogu inabidi mchanganye na zenu, halafu muone kama huyu Messi amefanya usanii wa kutuonyesha chumba feki au ndio chumba chake halisi
 
Kama kweli hzo pesa zote zilizoainishwa hapo juu angekuwa analipwa vizr hata muonekano wake ungekuwa nadhifu sasa anaonekana kama mchezaji wa mchangani, ...
Mkuu, suala la unadhifu kwa wachezaji wa bongo sio kipaumbele kwao, wala lisikufanye upate taswira halisi ya maisha yake. Kama wewe ni mpenzi wa jukwaa la michezo humu, bila shaka utakuwa umeisoma thread moja humu iliyokuwa inamzungumzia golikipa Shabani Kado jinsi alivyovaa hovyo huku akijua anaenda kupokea tuzo muhimu sana kwa kumbukumbu ya maisha yake ya soka, yaani tuzo ya golikipa bora wa VPL 2014/2015. Picha za kumbukumbu zitaendelea kuonekana na mavazi hayo ya hovyo, huku akina Ronaldo, Messi, Etoo, Diouf na wengineo huwa wanatupia suti ya nguvu siku ya kupokea tuzo ya mchezaji bora.

Unataka kusema Kado hana kipato cha kununua suti? Unataka kusema Rama Singano Messi hana uwezo wa kununua walau nguo chache nadhifu za kuvaa kiofisi anapoitwa TFF au maeneo mengine ya wadhamini wake mbalimbali? Mbona watu wengi tu wanapoanza ajira, mshahara wao wa kwanza au hata ile hela ya kujikimu huwa tunaitumia kununulia mavazi nadhifu?

Wachezaji wengi (sijasema wote) wa bongo hawajipendi. Timu zao na ya Taifa zinaposafiri nje ya nchi kwa ajili ya mashindano au mazoezi huwa zinawapa suti lakini hawazivai kwenye matukio ya kiofisi, badala yake wanavaa kama Singano, pensi na T-shirt iliyofubaa
 
Dah hii aione shafii Dauda, hapa ndipo tunapowapima waandishi wetu, hawabalansi stori yaani apelekewe hii mada na atupe majibu yasiyo shaka.
 
Back
Top Bottom