Kiwango kikubwa kabisa cha ujinga wa Imani kwa aishie kwa Imani.
Kiko wapi?
Kwangu Imani ni upungufu wa Maarifa.
Mtu yoyote smart hajadili mambo kwa maoni binafsi bali kwa kuangalia namna jamo lilivyo kwa uhalisia wake,hatujadili maoni binafsi hapa kijana kama hujui maana ya imani ungeuliza kwanza na sio kuja hapa na "mambo binafsi" ya kusema "kwangu mimi"
Imani ina maana yake na kama huijui ni vyema ukauliza
1÷1 =2 kwa nini niseme nina imani ni 2?
Sijakuelewa...
Kitabu kimeandikwa na binadamu na binadamu ndiye kaandika upendo na Mungu hivyo binadamu kwa vyovyote vile ndiye kamuumba Mungu kisha kutujengea imani ili tuamini alichoandika hata kwa reference.
Ni sawa na useme mtu aliyeleta habari za ajali kutokea mahali fulani mtu huyo atakuwa ameiumba ajali hiyo na kwasababu hiyo haipo
Hivi unafikiria kwa namna gani wewe?
Beleshi si kijiko kikubwa bali Beleshi period.
Yaani wewe mawazo yako yamejifunga kwenye kijibox kidogo kiasi kwamba unafikiria kuwa kila mtu ametookea mkoa wa Kilimanjaro
Kilimanjaro ndio wanatumia neno Beleshi badala ya neno Koleo,sasa wewe unaandika hapa Beleshi ukifikiria kila mtu atakuelewa.Makosa ya kuweza kuona tatizo hili dogo yanakufanya uonekane huwezi kabisa kujadili masuala unayodhani unaweza kuyajadili
Turudi kwenye familia una watoto 5. Upendo ulio nao kwa watoto wako ambao unajua watakosea basi umuue mtoto mmoja ili abebe dhambi za wengine ni ujinga uliokubuhu. Siwezi kuwa na upendo wa aina hiyo.
Siwezi kukushangaa wewe kushindwa kuelewa nilichokiandika na matokeo yake unaandika unachokifikiria wewe kujibu kile ambacho umekisoma na kushindwa kukielewa
Nani kasema wapi kuwa dhambi za watoto zilifutwa kwa mtoto mwingine kufa?
Aliua watu wote wakabaki 8 kisha wametoka kwa safina huyu aliyeokolewa na watoto wake anamlaani mtoto wake na vizazi vyake vyote kwa upendo alionao.
Hii inahusiana namna gani na hiki nilichokileta hapa kwenye mada hii?
Huyu Mungu wenu sadaka anayopenda ni sadaka ya damu lazima kiumbe kife ndio afurahi?
Aliekuambia kuwa sadaka hii ya damu ni kwaajili ya Mungu ni nani?
Rudia kusoma tena nilichoandika maana hujakielewa bado....
Huyu mungu wenu ni mchagga nini? Anapenda nyama na damu kuliko mboga na mimea kwa sadaka? Nao ni UPENDO? HEBU AMKENI NA MFUNGUE AKILI ZENU.
Yaani mtu alielala anawaambia walioamka waamke,hili ni ajabu la 90 la dunia..
Wewe hujuii kitu kabisa na huwezi kujua mpaka utakapokubali hujui....
Hamjui imani ilikuja kwa ajili ya kutawala Afrika?
Hakuna kitu kibaya kama kujidai unajua mambo na kuanza kuyaelezea wakati huyajui,huo ni kama ugonjwa fulani hivi....
Hujui imani ni nini lakini unajidai kutaka kuielezea,ungejua imani ni nini wala usingeihusisha na mambo ya kutawala.....
Mlifundishwa kusali mkifunga macho mlipofungua mlikuta biblia na bunduki mkononi muuane na kufarakana kwa jina la Yesu. Wao wamechukua mali wanaishi kama peponi ninyi mtasubiri maisha mazuri mkifa.
Hizi hadithi tulikuwa tunasimuliwa zamani sana wakati tuko watoto....
Naona leo umezileta tena...
Kwa upendo wake alimuua mwanae abebe dhambi za wanadamu hivyo ameruhusu wanadamu wafanye wajuavyo kwani makosa yao yatasamehewa kwa kifo cha mwanae UJINGA WA CHUO KIKUU HUU
Unaonekana umekuruouka kuandika bila hata kusoma nilichoandika,huwa sijadiliani na watu wa namna hii maana ni kupoteza muda....
Soma uandike vitu vyenye akili kama unataka kupata shule....