Katika hali ya kushangaza, Leo katika story na washikaji kuhusiana na maswala ya mahusiano, mapenzi na ngono kuna mshikaji ametuambia kuwa kuna njia mbadala ya kuzuia mimba na ameshauri kuwa pindi mkimaliza kufanya tendo la ndoa we na mwenza wako pasipo kutumia kinga, basi mwenzi wa kike anatakiwa ameze panadol 2 au vidonge vingine vinavyo fanana na panadol.
Kwa mujibu wa mtoa mada hiyo amesema kuwa kwa kufanya hivyo vidonge hivyo huingia mwilini na kuharibu nguvu za mayai ya kiume na hivyo kudhohofisha uwezo wa utungaji mimba.
Sasa mimi si daktari na sina sana utaalam na hayo mambo, nimeshindwa kubisha na nimeshindwa kukubali moja kwa moja ndo maana nimeleta hii thread hapa ili nipate uthibitisho na elimu juu ya hili.