Ni kweli Simba ina thamani ya bilioni 20?

Hivi Rage aliwaitaje wana Simba?
Naye Hans Poppe aliwaitaje?
Hayo sass ni dhahiri!
 
Mwanafalsalfa, Albert Einstein alishawahi kunena.. "If you can't explain to a six-year-old, you don't understand it yourself".

Sasa kama Mo anashindwa kutuelewesha lengo lake ni nini hasa.. Ina maana hata mwenyewe hajui anachotaka kukifanya.
Hichi nimesha kisema kama kuna watu hawata muelewa mo na watatafuta kila la kusema ili nia ya mo isifanikiwe.
Lakini mm nawaambia kama munataka kufurahi wana simba kaeni na mo au tafuteni mtu mwenye nia kama za mo.
Kama timu za ulaya zinauzwa leo nini kinakwamisha kwa timu za tanzania?
Kama humuelewi mwiteni mumuuluze yale musiyo muelewa awaeleweshe.
Lakini sidhani kama kumchukuwa Prof akafundisha chekechea ndio watoto watafaulu.
Mo ana zingumzia jambo kubwa sana tena la kisomi kwanyie watu waina yako sidhani hata ushinde nae wiki nzima kama utamuelewa.
Nivyema mukatafuta washauri wa biashara na sheria mukakaa nao wakawasaidia na si vibaya mukatumia FIFA kuwasaidia ktk hili analo zungumzia mo.
 
Nitalia na simba had I kesho naona simba inatoka kwa masikini wa kitanzania walioifikisha hapa kwa raha na shida na kuipeleka kwa matajiri ambao hata mpira hawajui
Akili matope hizi.. Eti simba inatoka mkononi mwa maskin hebu niambie faida waliyokua wanapata hao maskin. Kama mlitegemea kuishi kwa kutumia mgongo wa club tafuteni kazi zingine
 
Nitalia na simba had I kesho naona simba inatoka kwa masikini wa kitanzania walioifikisha hapa kwa raha na shida na kuipeleka kwa matajiri ambao hata mpira hawajui
Mkuu hao masikini wa simba sasa wanatoka ktk umaskini tena wanatoka ktk umaskini kwa mgogo wa simba.
Maana leo mo akikubaliwa watakuwa na hisa za 20b bila kuzinunua watapewa bure kabisa na wataruhusiwa kuziuza wakipenda.
Matajiri wengi tu wamenunu timu huko ulaya na wanachama wake wako pale pale na timu zinafanya vizuri.
Muhimu ni mikataba tu iwe mizuri na isimamiwe vizuri tajiri hajui mpira lakini ataajiri wanaoujua mpira na wanaojua biashara.
Na hata ma dr wataajiriwa watu kama ww wenye kichwa cha kubebea nywele kiweza kubeba na akili.
 
Mo anaweza kuwa na malengo mazuri na simba na mipango yake ni mizuri kabisa.... Ila napata wasiwasi mkubwa kwa nini Anatumia nguvu kubwa kuimiliki simba?!!!....
 
Akili tatu umekosea hesabu zako na kufanya mada yako pumba tupu.

Hizo Billion 20 unazosema ni kidogo ni kwa ajili ya 51% ya club,hiyo 49% ya wanachama kwa hyo thamani ya simba itakua around Billion 39.

Halafu kwani vipi?kama unamjua mtu mwenye dau zaidi ya hilo au wewe unayo mseme ili sisi tunaoitakia klabu yetu mema tuuze timu iendeshwe kitaalamu sio kijadi.
 
Nitalia na simba had I kesho naona simba inatoka kwa masikini wa kitanzania walioifikisha hapa kwa raha na shida na kuipeleka kwa matajiri ambao hata mpira hawajui
Sasa Hiyo Simba na umasikini wake unakusaidia nini wewe, acheni ichukuliwe nunueni hisa na hata ikiwezekana muifanye public kabisa na hata tusio wanachama tununue hisa kwa sababu za kibiashara
 
Naamin Mo ana malengo mazuri na Club ya simba..Anachotaka kukifanya ni kuifanya Simba ijiendeshe kama Kampuni kama vile ilivyo club kubwa barani Ulaya..Atachotakiwa anakifanya yeye kama nmiliki wa club kwa kuwa na share nyingi atahikikisha club haishuki thamani kwa kuifanya iwe club ya Ushindani nje na Ndani ya Africa.
 
Mkuu haya nimesema huku nyuma kuwa kunawatu wataanzisha viji maneno ili kukwamisha hii nia ya mo.
Mtu anathubutu kusema eti 20b nu ndogo.
Simba ina mali nyingi mali gani inawachama na eti wapenzi wengi.
Wanachama wengi na wapenzi wengi wanaisaidia nini simba?
Leo miaka mingapi simba haina ubingwa haijashiriki mashindano yeyote ya afrika?
Hawa watu wapo simba kwa maslahi yao wapewe vihirizi wakafukie uwanjani wapate kula yao tu hawajali simba kufanya vibaya.
Mm nilikuwa simba zamani nimetoka kwa kuchoka na mbinu chafu za kishirikina na kuhonga marefa na timu pinzani.
Unarundo la wanachama na wapenzi lakini timu haina mafanikio hata chembe faida yake nini?
 

Sasa nyie mnaojifanya mna mapenzi ya dhati na Simba huu ni mwaka wa ngapi hamjapata Ubingwa wala kushiriki michuano ya kimataifa?? Mmesaidia nini nyie wenye mapenzi kindakindaki
 
Mo anaweza kuwa na malengo mazuri na simba na mipango yake ni mizuri kabisa.... Ila napata wasiwasi mkubwa kwa nini Anatumia nguvu kubwa kuimiliki simba?!!!....
ame focus mbali,simba tayari ina fanbase kubwa sana,hivyo kibiashara haitampa shida sana...pia ni Chama lake
 
ame focus mbali,simba tayari ina fanbase kubwa sana,hivyo kibiashara haitampa shida sana...pia ni Chama lake
Hata Mzee bakhresa ni mwanachama hai Wa simba mpaka sasa na aliwahi kufanya hivyo anavyotaka kufanya MO kabla ya kuianzisha AZAM FC... Baada ya kubaniwa na wanachama Wa simba hakung'ang'ania.. Hapo ndipo ninapopata HOFU kwanini MO anaforce?? Kwanini asianzishe timu yake kama alivyofanya bilionea mwenzake Mzee Said B.
 
Kwenye Biashara kuna kitu kinaitwa Cost and Benefit analysis, Inawezekana kuanzisha Timu nyingine kama alivyofanya Mzee Said B ni gharama kubwa na haitoleta Faida kwa siku za Usoni.Simba iko na jina na ni brand kubwa na uwekezaji utareta matunda Mapema.
 
kuna kipindi madrid ilikuwa inachukua makombe lakini ilikuwa na hali mbaya kipesa mpaka uefa ilikuwa inataka kuifungia mpaka alipokuja rais wa sasa akaamua kuuza kiwanja cha mazoezi na kuirudisha timu yake katika hali nzuri,ac milan imechukua mataji mengi ulaya ni yapili kwa madrid angalia thamani yake wakianza kupanga thamani za timu ulaya inaelekea ujue chochote kuhusu namna gani wanathaminisha vilabu jaribu hata kugoogle utaelewa
 
Sasa nyie mnaojifanya mna mapenzi ya dhati na Simba huu ni mwaka wa ngapi hamjapata Ubingwa wala kushiriki michuano ya kimataifa?? Mmesaidia nini nyie wenye mapenzi kindakindaki
FisadiKuu unachotakiwa kujua ni kuwa pamoja na mafaniko hayo unayosema lakini ni vema tukaangalia aina ya uwekezaji wa MO,Binagsi nilibahatika kuhuduria ile Press yani unaona kabisa kuna kitu huyu jamaa anakitafuta kupitia nia yake ya kuwekeza na hiyo pesa,pia hiyo pesa jamani ni NDOGO kulinganisha na klabu ya simba,bilioni 20 ni pesa halali inayotosha kuinunua klabu kama Mbeya City,Toto Afrika na NK,simba inahadhi sawa na kina Enyimba huko,Tp Mazembe huko leo hii useme eti unaiuza kwa mtindo wa hisa kwa thamani ya bilioni 20?
 
okay nimekusoma vyema...kwahyo wewe unahisi kuna nn labda mzee mwenzangu?
 
povu jiingi kumbe tatizo uelewa tu
 
Kama hujitambui basi utakuwa umepigwa jiwe la utosini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…