Ni kweli Simba walipe vile viti lakin ukweli zaidi ni kuwa hakuna kiti cha tsh 200,000 pale

Sodoku

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2016
Posts
1,271
Reaction score
2,903
Nmeangalia ofisin kwangu nikauliza kwa jamaa yetu wa manunuzi zile office chair ambazo bado ni nzuri kabisa na comfortable tsh ngap. Akanambia tsh 150,000. Nikajiuliza vile viti vya uwanja wa Taifa kweli kimoja ni tsh 200,000? Aaahh jaman tuwe na aibu.

Yaani hata kama tunataka kupigia humo humo isiwe mpaka watu watushtukie sasa. Tungeongeza 30,000 tu kwa kila kiti bado ingelipa sana tu. Tungepata cha juu.ila hapo tumeongeza mpaka simba nao watashtukia dili.

Ila simba nanyi mlipe bwana achaneni na hasira za namna hiyo.
 
Hata wangesema 600 kwa kila kiti ni sawa tu ili ck nyngne wasirudie upuuz km huo
 
Waache kuibeba yanga hapo tff kila mechi ya yanga na simba lazima simba wapewe kadi nyekundu inamana huyo refa ni wayanga waache kuibeba yanga tumewashtukia bwana
 


Yaani kiti kimoja kiwe sh. laki nne (400,000?-) na pia adhabu nyingine zitolewe kama ifuatavyo:

-Wale waliovunja viti hivyo watafutwe popote walipo (kwa kupitia video zilizopo) na kufikishwa mahakamani kwa uhalifu.. Hata wakikamatwa 50 tu wanatosha ili wawe mfano kwa wengine
- Simba icheze bila mashabiki kwa karibu mechi 10 mfululizo (ikumbukwe kuwa hii siyo mara ya kwanza kwa wana-Simba kuvunja viti uwanja wa taifa)
- Nahodha wao Jonas mkude naye afungiwe kucheza mpira kwa kipindi kirefu kama miezi sita hivi...Hapa sijui sharia za TFF zinasemaje kwa adhabu ya mchezaji anayemsukuma refa mpaka anadondoka, lakini hilo ni shambulio ambalo linapaswa kuwekewa adhabu kali..
 
Simba buana kuharibu mliona raha eeh mbona hamkulalamika wakati mkiving'oa😛
 
kwani nyie wamkopesho hivyo viti mnataka mvitumie kwenye kitchen party au?
 
Mpira hapa bongo ni upuuzi mtupu, hawa marefa ndiyo wakufunga kabisa, TAKUKURU hebu na nyinyi amkeni kidogo, mpo tu kama miti, hawa marefa wa bongo wanakula rushwa na wachezaji pia, ni lazima muwe na mbinu za kutambua dalili za rushwa, ikibidi muajiri maofisa wanaoweza kutambua rushwa michezoni kama vp hata mkodishe maofisa wa kazi hizo. Kila siku kuna rushwa michezoni lakini TAKUKURU ipo mnalipwa mishahara minono na mnatuaminisha kuwa akili zenu zimegota kubaini mbinu za kukomesha hizi rushwa.
 
Kutafuta watu lolote walipo sahau hiyo mkuu!
 
wengine hawa hapa.
 

Kushavurugwa Wewe Mkodisho FC aka Vyura FC
 
HAWA SIMBA WATAJANG'OA VITI VYA NDEGE HAWA KABLA NDEGE HAIJATUA.OHOOOOO
 
wanaitwa wazee wa ning'oe viti ,yaani goli wafungwe wanang'oa viti wakifunga goli pia wanang'oa viti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…