Ni kweli smart TV zinatumia Umeme Mwingi?

Ni kweli smart TV zinatumia Umeme Mwingi?

Flat screen zinakula umeme sana tu asikudanganye mtu.

Chogo ilikuwa ile kubwa i akuwa na watts 60. Ukiwasha masaa 10 flulizo kwa mtindo wa kitanzania tunaoacha mabeki 3 nyumbani wanashinda kwenye TV, masaa 10 ingekula 0.6 units.

Lkn hizo flat screen ni kitu kingine kabisa. Nina hisense ya kisasa kabisa toleo la mwaka 2022.

Inakula 150w per hour
Hii inahtaji masaa 6 tu na dakika 30 kula unit 1 ya umeme.

Nikimuacha house girl nyumbani akaiwasha masaa 12 tu mfululizo anapiga unit 2

Nikija usiku kuangalia taarifa ya habari imeisha hio. Hizi flat zinatumia bulb nyingi sana kumulikia picha. Ulaji wake sio Rafiki

Nna Sony nchi 32, ya kisasa pia inakula watts 60 per hour.

Naambatanisha energy lebel ya TV hii ya hisense ya 55" ipo rated bad karibu na worseView attachment 2689718

Angalia hapo ipo level 4 wakati worse ni level 5. Kwa ufupi flat screen hasa vioo vikubwa inakula umeme sana.

Ukitaka inayokula vema kisasi hata energy level 3 bei yake ni kali kwakuwa technology yake pia itakuwa sio hii ya LED pengine mini-LEDs ndio energy sever
Ukisema hivo unanikumbusha, hapa nilipo kuna dada mmoja anaishi na mume wake, huyu dada huwa anashinda nyumbani hapo muda wote na Tv yao ya hisense huwa inawaka muda wote kuanzia ule muda anaoamka ( saa 4 asubuhi) hadi usiku saa 4 au 5 ndiyo anazima tv. Sasa kwa hali hiyo umeme hauendi mwingi? Maana mwenye nyumba kashaanza kulalamika na kutuongezea bei ya kuchangia umeme
 
Siwafundishi tena, Ukiteswa na bando, Huo ni uzembe wako, kwa halotel Pata GB2 kwa 3000, Gb3 kwa 4000, GB5 kwa 5000, Gb7 kwa 7000, Gb10 kwa 10000, Gb15 kwa 14,000, Gb20 kwa 19,000, Gb25 kwa 23000 na Gb30 kwa 26000 tu mwezi mzima. 0618370992.
 
Hem fikiria, mfano TV yako inatumia 100W kwa saa na unaiwasha tuseme 8hrs(msaa nane) kwa siku.

Haya tujumlishe na kuzidisha, kugawanya na kutoa;
100W x 8hrs ni sawa na 800Whr za power consumption kwa siku moja, sasa kwa vile units za umeme zinapimwa kwa kilowatt inabidi tugawe kwa 1000 ili iwe kwenye kWhr, kumbuka 1unit ni sawa na 1kWhr, hivyo 800Whr ni sawa na 0.8kWhr au 0.8units.

Hivyo, ukitumia TV yako masaa nane kwa siku, utakuwa umetumia 0.8units(haifiki hata unit moja)

Nimetoa mfano wa TV inayotumia 100W kwa saa, jaribu kuangalia ya kwako ina power consumption kiasi gani. Factors zote zinabaki constant (efficiency ya TV yako iwe 100% kitu ambacho sio)

Nikosolewe chap...
Hapo mkuu ume score 100% kwa maelezo kamili. Homework kwake aangalie tv yake Ina watts ngapi Kisha atumie mfano ulioweka.
 
Back
Top Bottom