Ni lazima mwanangu akikua ajue coz ninajuta kumpenda baba yake

kuna mtu naplan kumfanyia kama ulivyofanyiwa wewe,make nishamwambia home hawamtaki yeye hatk kuamini,wait...
Sometimes matatizo mengine mnajitakia wenyewe!

Si useme tu we ndio humtaki, eti hm hawamtaki, kwani wao ndio wanaishi nae? watu mnapenda sana kuumiza wenzenu ila tu ukumbuke hilo unalotaka kumfanyia mwenzio lazima siku moja litakurudi hata ipite miaka mingapi, we tamba tu sasa ila wakati wako waja
 
dah pole mdada mzuri Mungu yupo atakusaidia nimeona umejoin jf soon tarehe 29 mwezi jana sijui ndo ulikuwa unataka ushauri au. Naomba nichukue fursa hii kukukaribisha humu ndani
Wageni mna mbwembwe
 
Reactions: Mbu
Maty hawa viumbe sijui wakoje, kuna wakati wanasahau kabisa raha na tabu zote mlizopitia, wanageuka wanyama, eti home hawamtaki, kwani ukimuoa unawaolea ndugu zako?
 
pole dadangu mtoto atakua tu maana aliye muumba aliyajua hayo u just work hard umfanye mtoto asimic vitu vya msingi
 
pole sana shost kwani huo ushauri hapo red ulikuwa hujui ilo? Wanaume ni sooo mwaya ISHI KIMBAYU WAYU
 
dah...haya mapenzi huwa siyaelewi,uliacha chuo ukafanya nini?mtoto anahaki ya kumjua babake,yeye ndio ataamua huko mbele!pole lakini
 
dah...haya mapenzi huwa siyaelewi,uliacha chuo ukafanya nini?mtoto anahaki ya kumjua babake,yeye ndio ataamua huko mbele!pole lakini


fabinyo you made my day bana dahhh...hahahahahahaaaa---huyu mkaka ni mweusi vipi, lol!...?
 
Kwanini hukujifungulia Dar, km ni mtu wa kukusaidia alie huko Kaskazini now angekuja yeye Dar?????? Pole though...
 
Pole sana mdada.

Do you nkow what. You cant be a mother and a father at the same time .You can only be the best mother in the world for your baby.
Tulia tafakari maliza uzazi rudi kazini lea na tunza mtoto wako.
usijaribu kumtafuta huyo mwanaume hata dakika moja, hope you have support from your family.
Mpotezee kwa kumaanisha mlee mtoto kea mapenzi yote ukiwa unazungmza naye mtoto mwambia baba yupo kuna siku utamjua dont create any hatred
 
KINACHONIUMA.
~nilimpenda kupita kiasi
~nilipoteza vitu vingi ikiwa ni pamoja na kuacha chuo ajili yake.

Pole kwa yote..Ila hilo la kuacha chuo kwa ajili ya mwanaume haikuwa uamuzi wa burasa, ungeahirisha hata masomo siyo kuacha chuo kabisa, nadhani ni funzo tosha umepata...next time, fikiria mara mbili kwenye suala kama hili!!
Mpe mtoto malez bora, baba yake akitaka kumfahamu mwanae mpe nafasi..hata kama umemchukia usisambaze hiyo chuki kwa mtoto wenu.. Chukianeni ila mtoto apewe haki yake bora ya kimalezi!!..
najua ni ngumu ila tenganisha hisia zako za chuki, halafu jitahidi uwe na amani ili uweze ku-focus mbele maisha yako vizuri. Hujazaliwa na huyo mwanaume hata kama unampendaje, kwahiyo utaweza kuishi bila yeye na kufanikiwa vyema maisha yako ukituliza akili!
Pole na mlee mtoto vizuri..
 
Reactions: Mbu
Nimesoma kote sijaona mahali ambapo mlifunga ndoa, kwa hiyo si mumeo. Unalalamika nini? Umeyataka mwenyewe. We unadaka mimba ya mwanaume ambaye hajakuoa halafu unakuja kulalamika hapa? Sikupi pole hata kidogo maana huu upuuzi naupinga kwa nguvu zote. Ona sasa mwanao unavyokuja kumsababishia unyanyapaa kwa tamaa zako mwenyewe. Nakuhakikishia kwa uzoefu, utakapomweleza mwanao haya yote, atasikitika kwa sababu wewe ni mamake anakupenda, lakini bado ataona aibu sana kuzaliwa katika mazingira ambayo mama alijiaibisha kiasi hiki. Na atakulaumu sana tu. Acheni kujibebesha mimba za ngono zinzi, mnawaharibia watoto wenu na kuwapa maumivu ya kudumu katika akili zao.&nbsp;<br>KILICHOPO kwako sasa, tulia umlee mwanao kwa hali zote bora iwezekanavyo afanikiwe katika maisha haya angalao itampunguzia maumivu. Achana na suala la kuendeleza bifu kwa mtoto utaumia zaidi. Huyo mtoto akikua atamtafuta babake na atapewa story tofauti kabisa, na uamuzi wa ipi aiamini kati ya hiyo utakayompa na ile atakayopewa na babake ni wa kwake mwenyewe. Anaweza kumwambia kwa mfano "Mwanangu haya mambo sikutaka kujadili lakini kama mamako kakuambia hivyo bora nami nikuambie ukweli. Nilimfumania mamako akiwa na mwanaume chumbani kwangu ndio ikawa mwisho".
 
pole sana mpz nakuapata kinoma mana nina rafiki yangu kaumia sana juu ya mtu ila anampenda sana na ndio bado anampigania ni noma yani
 
Mwanaume kweli umpende kwa kiasi fulani, na pia uwe na moyo wa ujasiri unapopata matatizo kwenye uhusiano wenu, sio pacha wako huyo, useme ushee naye kila ishu kuhusu maisha yako na maendeleo yako kwa ujumla, dah, yaani naona kama kila binadamu haaminiki, mtu unatakiwa kuwa makini siku zote, trust no one!, pole sana my Sister, Mungu atakuongoza.
 
Pole sana Kintakuntai;

Nadhani kwa sasa kuna mengi sana yanapita kwenye mawazo yako na hasa woga wa kukabiri maisha yenu (wewe na mtoto).

Nikisoma message yako bado nashindwa kukubali kama ndani ya miaka hiyo 6 uliweza kumjua vizuri huyo jamaa. Nisingependa kuuliza kwa nini ndani ya miaka 6 hakutaka kujifunga kwako kwa ndoa.. Majibu yangu ya haraka haraka ni kama vile huyo jamaa ni kicheche na inawezekana vijihela vya pale Ardhi vinamzingua na anashindwa kujua ni vya kupita tu..

Challenge (changamoto) kubwa siyo kulea mtoto au maisha yako ya baadaye, changamoto kubwa ni jinsi gani utaweza kumsamehe akija tena na kumuamini ya kwamba yeye ni baba wa mtoto wako. Kuwa baba mtoto siyo kitendo cha kumtia mtu mimba, ni kitendo cha kukubali kwa vitendo majukumu ya kuwa baba. Kintakuntai, unao mtihani mkubwa uko mbele, kwani nadhani huyu jamaa atakuja kupiga magoti na kuomba msamaha...

Wanawake mlivyo na huruma unaweza kukuta unamsamehe bila kujiuliza kama ni kweli unajua tabia yake (kiundani).. na kama ukikurupuka na msamaha bila kufikiri, kuna uwezekano mkubwa unakaribisha bomu ambalo litaripuka baada ya miaka mitatu au minne ijayo..yaani kabla hata kijana hajamaliza shule ya msingi.. Yaani atakupa maumivu ambayo yatakurudisha nyuma..back to square one!

Ushauri wangu.. Tuliza akili, kuna wazazi wengi wamefanikiwa kulea watoto peke yao, wewe binafsi hutashindwa.. Kwa sasa lazima uwe uwe makini sana na huyo jamaa ili asikuumize kwa mara ya pili... na mwisho amini Mungu yupo!
 
bora umeuliza. hii tabia siipendi! kwani huyo baba wa mtoto hahusiki na pocess nzima ya kuleta mwanae duniani? kuna mtu anajifungulia kwao anakaa akirudi kwake baada ya siku 2 anaanza kazi! hivi kwa nini wanawake hawapendi the convinience of their homes? na angekua kajifungulia kwa mama mkwe angerudi kwake baada ya wiki!
Kwanini hukujifungulia Dar, km ni mtu wa kukusaidia alie huko Kaskazini now angekuja yeye Dar?????? Pole though...
 
Yaloyopita si ndwele tugange yajayo - ila uliacha shule kwa sababu yake? Why Girl why? What for?


Jua thamani yako,he doesn't deserve you. Achana naye songa mbele. Utapata mwingine. Mtoto siyo doa wengine hawa mind mambo hayo.

Kaa kimya. Usimtafute. Silence is the weapon u should use. He will be so uncomfortable where he is and he will wonder as to why you are not calling him. Just ditch him. Najua ngumu ila jaribu.

Elewa saikolojia ya wanaume,garbage in garbage out (samahani sana). Hana habari na mtoto anajua atazaa tena. Adui wa mwanamke ni mwanamke. Nimeshaona mtu anatazama mwenzie wa watoto 5 anaondolewa aingie yeye. So cheap kwa kweli anatia kinyaa.

Ni PM kwa maelekezo zaidi. Pole. Forge ahead and God be with youm
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…